Envaya

watoto  wakiwa kituoni 

afisa habari wa shirika na mratibu wa mafunzo akihojiana na mmoja wa washiliki waliofanikiwa kuhuzulia mafunzo ya ukatili wa kijisia na kingono 

UKATILI WA KIJINSIA

Maana

Ni aina ya ukatili unaohushisha mwanaume na mwanamke, unaotokana na jinsi wanavyohusiana na hali ya kutokuwepo kwa uwiano kati yao. Ukatili huu hufanywa kwa mtu kwa sababu tu ya jinsi yake.

Ukatili wa kijinsia huathiri wanawake zaidi kuliko wanaume.

AINA ZA UKATILI WA KIJINSIA

a)       Ukatili wa kimwili

Ni kitendo anachofanyiwa mtu kinachohusisha kuumizwa mwili na huweza kuonekana moja kwa moja au mwathirika kuhisi maumivu bila watu wengine kutambua kitendo hicho. Mifano ya ukatili wa kimwili ni vipigo, shambulio la mwili, kuchomwa mwili moto, matumizi ya silaha, kuvuta nywele, kusukuma, kunyonga mkono au mguu, kumpiga kichwa ukutani/sakafuni na kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu yoyote ya mwili

b)      Ukatili wa kisaikolojia

Ni ukatili ambao mtu anatendewa na unamsababishia maumivu kiakili/kihisia ambapo mtu mwingine hawezi kutambua kuwa mwenzake ametendewa ukatili hadi mazingira yatakapojitokeza na mtendewa akajieleza. Mifano ya ukatili wa kisaikolojia ni matusi kwa njia ya maneno au ishara yenye lengo la kudhalilisha, vitisho na kutishia kufanya fujo, maneno ya kufedhehesha, kudharauliwa hadharani, kutishia kutoa siri, kuingiliwa faragha, kutishiwa kuuawa, wivu wa kupindukia, kunyang’anywa watoto kwa makusudi.

c)       Ukatili katika uhusiano wa kingono

Ukatili huu huambatana na vitendo vinavyohusiana na masuala ya ngono. Mfano unyanyasaji/bughudha za kijinsia, kujamiiana kwa maharimu, ubakaji ndaniya ndoa, ulawiti,utekaji na usafirishaji wa wanaume au wanawake na watoto kwa ajili ya ngono, utumwa wa kingono, mashambulio na kuingiza vitu vigumu kwenye sehemu za siri.  

d)      Ukatili wa kiuchumi

Ni aina ya ukatili ambao unamnyima fursa za kiuchumi mwanamke au mwanaume katika kujiongeza kipato na kuchangia katika maendeleo. Aina hii ya ukatili huwapata wanawake kutokana na hali yao ya kuwa tegemezi kwa wenzi wao . Mifano ya ukatili huu ni kunyang’anywa mali, ubaguzi katika fursa za kiuchumi na umilikiwa mali, ubaguzi katika fursa za kujipatia mahitaji muhimu ya chakula, malazi na mavazi, kunyimwa haki za kurithi, elimu duni na mianya finyu ya fursa za kujielimisha, kunyimwa sehemu ya mapato ambayo ni jasho lako na kukatazwa kufanya kazi.  

 

      

e)      Ukatili unaotokana na tamaduni au mila potofu

Huu unatokana na mila na desturi za jamii zetu ambazo zinakinzana na haki za binadamu hivyo kuchangia kuwepo kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia. Kwa mfano ndoa za kushurutisha, ndoa za utotoni, kutakasa wajane, kurithi wajane, ukeketaji, matambiko ya kingono kwa watoto, ndoa za maharimu, kufungiwa au kuwekwa ndani kwa shuruti, ndoa za ushirika, miiko ya chakula na ukatili utokanao na mahari

 

ATHARI ZA UKATILI WA KIJINSIA

a)       Athari kwa mtu binafsi

  1. Athari ya kisaikolojia
  2. Athari ya kimwili

b)      Athari katika ngazi ya familia

Ukatili wa kijinsia unaweza kusababisha madhara mengi katika familia. Baadhi yake ni kupotea kwa amani na upendo, kujenga uhamasa kati ya wanafamilia, watoto kutoroka nyumbani, kupoteza pato la familia kwa kutibu majeraha yanayotokana na vitendo vya ukatili, kupoteza wazazi au watoto. c) Athari katika ngazi ya jamii

Kupoteza nguvu kazi ya jamii, muda na mali katika kushughulikia maswala ya ukatili wa kijinsia, ongezeko la watoto wa mitaani, migogoro na umaskini.

d) Athari katika ngazi ya taifa

Madhara ya ukatili wa kijinsia hapa ni pamoja na kupoteza nguvukazi ya taifa, ongezeko la watoto mitaani, ongezeko la uhalifu, maendeleo duni, kupoteza rasilimali na kuongezeka kwa umaskini. Taarifa juu ya ukatili wa kijinsia inaweza kutolewa katika

-Afisa Ustawi wa Jamii

-Afisa maendeleo ya jamii

-Polisi dawati la jinsia

-Afisa mtendaji kata

-Paralegal

 

we open trainnig for prayer 

enjoyment we need to happen for the children all days

                             Lunch at the trannig of sexual harrasment 

THE HOPE RELIEF ORPHANS CHILDREN VILLAGE ORGANISATION

(HROV)

 

A BRIEF REPORT ON CHILDREN RIGHS TRAINING PARENTS AND GUARDIANS IN LUGEYE CENTRE

 

THE COLLABORATION BY LUGEYE CHILDREN CENTER

(HROV) DATE 30/08/2019

 

01. INTRODUCTION

The Hope Relief Orphan Children Village is an community Based organization (CBO) with Registration No. MDC/CBO/629 of 14 April 2014.

 

HROV management arrangement is as follow:-

-         General Assembly

-         Board

-         Management committee

-         Departments

-         Office Bearers

  • Chairman
  • General Secretary
  • Project coordinator
  • Treasures

 

02. HROV MAIN OBJECTIVES ARE

-         To promote life skills and Social accountability among community concern child development

-         To establish the orphans and most vulnerable children centre.

-         To provide quality and standard education for child in community

-         To proved health services to orphans and most vulnerable children

-         To mobilizing resources to facilitate child engagement in wealth creation for development

03. ACTIVITIES DONE

Parents and guardians who have children in the centre through HROVC getting training on children right and sexual harassment. These trading were done in the children centre (Lugeye store) these training have been given to more than thirty five (35) parents and guardians which included village local government workers.

 

The parent and guardian shared in details about

  • The concept of child
  • Children rights
  • Service to disability child
  • Sexual harassment

 

04. ____ FAST AND LUNCH

The all participants getting tea and lunch living proper time according to the time table, of curce enjoying very much delicision food which prepared by the HROV management

 

05. WAY OUT.

All participants after having training on children rights keep stralegic to protect children their environment (home, school and community). The plan setup include.

 

-         To report any issue of children harassment to the responsible authority even through to use government free number as 0800110017 for children protection.

 

-         To educate the all community concern children Right’s by public meeting and to the leaders.

 

-         To ensure that all parents and guardian to involve totally to bring children’s their right’s in education, health and other services

-         To make sure that all children keeping in the centre attend without missing the day of Saturday in order to take services which takes place.

 

06. THE WORD THANKS YOU.

The HROV Management committee thanking all participant to facilitate training parents and guardian at the children centre on children Rights.

 

 

Thank you again

 

“God Bless You

 

                                     By Shija Clement Kinyata

Executive Director

 

Cell No. +255(0) 767 970 757

Email: thehopereliefchildren@yahoo.com

Website: www.hvor.org/hrov