Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

 

Email address: lingonetlindi@yahoo.co.uk
Phone number: +255 23 220 2630,0784860372
Street address: JENGO LA PRIDE,BARABARA YA JAMHURI,JIRANI NA BENKI YA CRDB,CHUMBA NAMBA 8&9

Mailing address: 

P.O.BOX 92 LINDI

Contact name:

KHAMIS CHILINGA
Contact title: KATIBU MTENDAJI

Lindi non governmental organisation network ilianzishwa kama Mtandao wa asasi za kiraia wa wilaya mwaka 2002 kufuatia warsha ya asasi za kiraia 13 za wilaya ili kubaini na kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazokabili sekta ya AZAKi katika kufikia malengo yao.kwa msaada mkubwa wa shirika la kigeni lijulikanalo kama THE CONCERN WORLDWIDE Lindi non governmental organisation network(LINGONET) ilianzishwa na kusajiliwa rasmi mwaka 2003 na kupata cheti cha ithibati(certicate of compliance) mwaka 2010

Saidi Kawanga, Mhasibu

                                                                            

 

 

 

 

 

                        Khamis Chilinga, Katibu Mtendaji

Bi Esha Salum ,Mwenyekiti wa LINGONET

.LINGONET inaendeshwa kwa taratibu za uanachama,asasi yoyote iliyosajiliwa katika sheria za NGOs inaweza  kuomba na kuingia uanachama wa LINGONET

malengo makubwa ya LINGONET ni kujenga uwezo wa asasi katika wilaya ya LINDI,kuratibu shughuli zao ili kuepuka muingiliano wa shughuli na kujenga uwezo wa jamii katika kuandaa,kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo na uchambuzi wa sera

LINGONET imefanya shughuli kadhaa katika kujenga sekta ya AZAKi katika wilaya ya Lindi tangu kuanzishwa kwake kwa ufadhili wa mashirika mbalimbali kama ifuatavyo;

(i) Mradi wa CODEP ambao ulilenga kujenga uwezo wa asasi za kiraia katika kushirikiana na kuboresha mahusiano na wadau wengine wakiwepo serikali kwa ufadhili wa THE CONCERN

(ii) Mradi wa kujenga mitandao ya wilaya katika mkoa wa Lindi mwaka 2006-2007 kwa ufadhili wa The Foundation for civil society

(iii) mradi wa kujenga uwezo wa AZAKi na wananchi katika ushawishi na utetezi juu ya     uchambuzi wa sera.mwaka 2009-2012 kwa ufadhili wa The Foundation for civil society

(iv) mradi wa haki na usawa wa kiuchumi unaofadhiliwa na SIDA kupitia kwa SAVE THE CHILDREN kwa miaka maradi ambao unalenga kujenga uwezo wa watoto katika kutambua na kudai haki zao kupitia mabaraza ya watoto yaliyoundwa katika kata na wilaya zote za wilaya za Kilwa ,Lindi  na Ruangwa mradi huu ni wa miaka minne

LINGONET inapata viongozi wake kupitia uchaguzi inaofanyika mara moja kila baada ya miaka mitatu ambapo viongozi wafuatao huchaguliwa

(1) Mwenyekiti

(2) Makamu mwenyekiti

(3) Katibu mtendaji

(4) Katibu msaidizi

(5) Mweka hazina

(6) Wajumbe saba(7)

LINGONET imeweza kuratibu uanzishwaji wa mtandao wa mkoa wa lindi LINDI ASSOCIATION OF NGOs(LANGO) kupitia mradi wake wa kujenga uwezo wa mitandao na kwa sasa inafanya kazi ya kujenga uwezo wa asasi ili ziweze kujiendesha kwa ufanisi na kufikia malengo yao katika kuhudumia jamii

LINGONET inaratibu mradi wa haki na usawa kiuchumi katika wilaya tatu za mkoa wa Lindi,mradi ambao unatekelezwa katika wilaya saba za Tanzania za Temeke,Kilwa,Ruangwa,Lindi,Same,Handeni na Arusha kwa ufadhili wa SIDA kupitia SAVE THE CHILDREN

Hadi hivi sasa LINGONET ina wanachama 23 na maombi kadhaa yanapitiwa kamati tendaji,LINGONET ni mtandao ambao umejijengea jina katika jamii.

Picha kubwa juu ni jengo ilipozaliwa LINGONET mwaka 2002,picha kubwa chini ni Mwenyekiti wa kwanza wa LINGONET Mr Said Kawanga,chini yake ni washiriki wa moja ya mafunzo ya LINGONET chini yake ni Mwenyekiti wa sasa wa LINGONET Bi Esha Salum na mwisho chini ni Katibu Mtendaji wa sasa wa LINGONET Mr Khamis Chilinga                                     

                                                                                

  

May 30, 2011
Next »

Comments (5)

[comment deleted]
Asasi za kiraia zinatakiwa kuwa kioo cha jamii kwa kubuni na kufanya kazi zake bila urasimu na ukiritimba,jamii ina imani kubwa na waaAZAKi kuliko wana siasa hivyo ni wajibu wa wana harakati kujibu imani ya jamii kwa vitendo
May 30, 2011
BEATUS PATRICK (DAR ES SALAAM) said:
Hello to you!
Congratulation for your work.
Hi to Mr. Chilinga, Mr. Kawanga, Bonamax, Sina and all other.
May 25, 2012
ISMAIL MPONDA (RUANGWA) said:
I appriciate LINGONET for your efforts but you have to ensure proper NGOS are observed for people to ask asistance for their social deveropment.
July 24, 2012
Ahsante kwa maoni na tunaahidi kuyafanyia kazi
January 27, 2013
kupitia mabraza ya wilaya ya tume ya mabdiliko ya katiba na yale ya AZAKi na makundi yanayofanana tunawahimiza wajumbe wote kutoa michango yao katika kupitia rasimu ya katibu ili kuiboresha na kubebe utaifa zaidi badala ya kuhakikisha maslahi ya kichama ,kidini au kikanda yanachukua nafasi ,hiinninchi yetu sote ikipata katiba mbovu ni sisi tutakaokuja kupata tabu na vizazi vyetu
July 22, 2013

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.