Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

TEYODEN YATOA MILINI SITA(6) KUSAIDIA VIKUNDI VYA WASICHANA WALIOJIFUNGUA KATIKA UMRI MDOGO.

Wasichana waliojifungua katika umri mdogo sasa wamepata fursa ya aina yake baada ya kukabidhiwa cheki zenye thamani ya milioni 2 kwa kila kikundi.

Akikabidhi cheki hizo mkuu wa wilaya ya Temeke katika ukumbi wa Amka youth aliwataka wasichana hao kuwa makini na pesa hizo na kwamba zitumike kwa miradi iliyokusudiwa ili kuwaletea tija katika maisha yao.katika risala yake mkuu wa wilaya ya Temeke aligusia pia suala la vijana kuwa na miradi ya kudumu ya kiuchumi na hasa masuala ya kilimo.Aliwataka vijana kutozarau kilimo na sio tu kilimo cha shambani kwa jembe la mkono lakini  kilimo cha kisasa ambacho kinatumia mbinu za kitaalam.Alisisitiza kilimo mfano cha nyanya ni sehemu ndogo tu ya ardhi inaweza kutumika na ikazalisha nyanya nyingi.Hivyo vijana hao wa kike wakaweza kujiajiri wenyewe.

Katika risala yao kupitia mwakilishi wao Zakia wasichana hao waliojifungua kabla ya umri walimuomba mgeni rasmi kuwa mlezi wa vikundi hivyo.Pia waliiitaka jamii kuwaangalia wasichana wenye umri wao kwa umakini wasije kutumbukia katika matatizo kama yao na kuwaweka katika changamoto za kimaisha kama wanazozipata wao.

Mradi huu umefadhiliwa na Population Council, unasimamiwa naTAMASHA na unatekelezwa na TEYODEN.

MRADI WA MABINTI WALIOPEMBEZONI WATEMBELEWA NA MGENI KUTOKA MADAGASKA.

Mgeni wa kutoka Nchini Madagaska, Bi. Marium Toure ambaye ni Ofisa kutoka UNICEF Madagaska ametembelea mabinti ambao ni walengwa wa mradi wa kujenga uwezo wa mabinti waliozaa katika umri mdogo  na kutulekezwa na wenzi/familia  zao.

Mradi huu unatekelezwa  katika kata 4 za Manispaa ye Temeke, kwa ushirikiano kati ya TEYODEN watekelezaji,TAMASHA wasimamizi na POPULATION COUNCIL wafadhili.Lengo hasa ni kuwezesha wasichana hawa kupunguza changamoto za maisha walizonazo na kuwaepusha na maambukizi ya V.V.U imeelezwa sana katika taharifa,magazeti na tafiti kwamba wasichana hawa wapo katika hatari ya kupata mimba nyingine na hata maambuziki ya ukimwi kwa kuwa katika mazingira hatarishi.

Katika mazungumzo ya kubadilishana mawazo na wasichana mgeni huyu ambae aliambatana na Richard Mabala ambae ni mkurugenzi wa TAMASHA aliwataka wasichana kutohuzunika kwa kuwa wapo katika maisha yenye changamoto nyingi.

"kuzaa sio kosa,ila tatizo ni umri wenu kuwa mdogo pamoja na hayo mlipaswa kuwa katika uangalizi wa familia na waliowapa  mimba"alisema Bi. Marium.

Kwa mujibu wa Bi. Marium alieleza kuwa wasichana wa nchini ,Madagaska hawana programu kama hii zaidi ya progammu za kusaidia vijana hasa eneo la stadi za maisha na stadi za ujasiriamali.

Tatizo la wanajamii hasa vijana wa Madagaska ni kudai pesa kwa kila shughuli inayofanyika hata kama ina lengo la kuwasaidia wao wenyewe dhana ambayo anaishangaa sana kutoikuta kwa vijana wa Tanzania.

Marium alipongeza sana juhudi za TEYODEN na kusema kuwa wasichana wanatakiwa kutokata tamaa na kujichanganya kufanya hata kazi za kiume kama kuendesha bodaboda,kuosha magari na kazi nyingine ambazo zitawafanya kujipatia kipato na kupunguza umasikini.

Mwisho alimpongeza Bw. Mabara kwa kazi zake nzuri ambazo pia zimewasaidia vijana wa Madagaska.

 

TEYODEN YAFANYA MAFUNZO REJEA KWA MENTORS MRADI WA KUJENGA UWEZO WA KINAMAMA WADOGO WALIOSAHAULIKA.

TEYODEN imefanya mafunzo rejea ya siku 3 kwa mentors(walimu wa wasichana) 16 kutoka kata za Azimio,Kibada,Vijibweni na Mtoni.Mentors hawa hapo awali walipatiwa mafunzo ya satdi za maisha,elimu ya ujasiriamali na mafunzo ya uwezeshaji ili waweze kuwa walimu,waangalizi lakini kama walezi kwa wasichana 80 katika kata 4 za mradi kama zilizokwisha taja hapo juu.

katika tathimini ya TAMASHA iliyofanywa na mwakilishi wa TAMASHA katika Mradi huu bi Aziza ulikuta mapungufu kidogo kwa walimu hawa ikiwemo uwezo usiridhisha katika utoaji wa masomo kwa wasichana ngazi ya kata za mradi.Hivyo ufumbuzi wa haraka ulionekana ni kuwarusha katika mafunzo ya hatua ya pili ili kukazia hasa katika eneo la mbinu za uwezeshaji.

Mwisho wa mafunzo haya ya siku 3  wawezeshaji rika(mentors) walijiwekea mipango kazi yao ili kuwezesha kufanya kazi kwa urahisi na kwa mwelekeo wa pamoja.

Mategemeo ya TEYODEN ni kwamba wasichana wataboresha shughuli zao ili tuwawezeshe kupata mitaji ya kuanzisha na kuboresha shughuli zao za  kiuchumi.

TEYODEN inategemea kuwapa kiasi cha sh 8,000,000/= sawa na sh 1,000,000 kwa kila kikundi.Kila kata inavikundi 2 vya wasichana 10 kila kimoja.

Apply to the YouthActionNet Global Fellowship Program!

Launched in 2001 by the International Youth Foundation, YouthActionNet strengthens, supports, and celebrates the role of young people in leading positive change in their communities. Each year, 20 exceptional young social entrepreneurs are selected as YouthActionNet Global Fellows following a competitive application process.  The year-long Fellowship program includes:

Skill-building:

  • A seven-day leadership      retreat for twenty selected Fellows which offers dynamic peer-to-peer      learning, collaboration, and sharing among young visionaries 
  • Focus on the personal growth      and leadership abilities of Fellows, in addition to providing instruction      in specific skills required to manage innovative, world-changing organizations 
  • Year-round learning      opportunities based on Fellows' individual needs and the six dimensions of      leadership highlighted in the YouthActionNet® Global Curriculum: Personal,      Visionary, Political, Collaborative, Organizational, and Societal.

Networking and Resources:

  • Membership in the      YouthActionNet® global network of fellows and alumni
  • Grant opportunities
  • Opportunities to network and      collaborate with IYF projects and partners

Advocacy:

  • Training in areas such as      communications planning, media outreach, message development, presentation      skills, and innovative uses of new media technologies
  • Access to global advocacy      platforms and media coverage

Eligibility

  • Open to all young people aged      18-29 (as of October 7, 2012)
  • Applicants should be founders      of existing projects/organizations, or leading a project within an      organization.
  • Proficiency in English is      required; applications must be submitted in English
  • Must be available to attend      full retreat (all expenses paid) in the second week of October 2012.

Key Dates

  • March 12: Applications      must be submitted by 11:59pm on this day.
  • March 28: All      applicants will be contacted regarding the status of their application.
  • May 22: Finalists will      be notified 

 

The 2012 retreat will take place during the second week of October 2012 inTurkey.

For more information visit:

http://www.youthactionnet.org/index.php?fuse=aboutfellowship

 

Kwa habari na taarifa kuhusu wilaya ya Temeke kama vile idadi ya watu kata na mgawanyo wa rasilimali na mengine mengi unaweza kutembelea website hapo chini ili kupata habari za kina na majibu ya maswali unayotaka kuyapatia majibu.

http://sw.wikipedia.org/wiki/Wilaya_ya_Temeke

MDAHALO WA VIJANA WARUDI KWA KASI MPYA NA MAARIFA ZAIDI.

Timu iliyoundwa kufanya uzinduzi wa mdahalo wa vijana uliobadilisha vikao vyake kutoka kila jumamosi na kuwa mara moja kwa mwezi ilifanya vizuri kwa kufikia 60% ya malengo yaliyowekwa katika kikao cha kamati ya utendaji cha TEYODEN cha hivi karibuni.Mdahalo huu uliohudhuriwa na vijana wapatao 70 na kuwezeshwa na bwana Ismail Mnikite ulifana sana ingawa ulichelewa kidogo kuanza.Mada ya mdahalo ilikuwa ni Ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika masuala ya kijamii na kimaendeleo na mada ndogo juu ya masuala ya katiba.Katika mada ya ushirikishwaji vijana waliweza kubungua bongo,kukubaliana na kujifunza maana ya ushiriki,ushirikishwaji na maana ya uwajibikaji.Pia walifunza masuala ya msingi ambayo vijana wanapaswa kushiriki ipasavyo,stadi za kujenga ili kuimarisha ushiriki wenye tija na wenye matokeo.

Mwisho wa Mada washiriki na mwezeshaji walikubaliana kuhairisha mada ya katiba ili irudiwe katika mdahalo wa mwezi wa 3(machi)

mdahalo ulitanguliwa na ufunguzi wa mwenyekiti taratibu za kushiriki na masuala ya utangulizi kutoka kwa kamati ya maandalizi na katibu wa TEYODEN.

 

Pichani juu:Wanajamii wakipata maelezo kutoka kwa mweka hazina msaidizi wa TEYODEN bi Prisca Moses juu ya V.V.U/UKIMWI Katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika viwanja vya Zakhiem mbagala Charambe.Pichani chini:mama mwenye kofia Mgeni rasmi wa maadhimisho ya Ukimwi duniani Naibu Meya wa Manispaa ya Temeke akipata maelezo ya shughuli za TEYODEN kutoka kwa afisa habari wa TEYODEN bwana Hamphrey Shao.

Vijana washiriki maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika tarehe 2 disemba 2011 viwanja vya Zakhiem Mbagala Charambe

Takribani vijana 60 wanachama  na Viongozi wa mtandao wa vijana Manispaa ya Temeke wameshiriki maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani ambayo mwaka huu yamefanyika katika viwanja vya Zakhiem kata ya Mbagala.Maadhimisho hayo yaliyopambwa kwa vikundi mbalimbali vya sanaa za ngoma na maigizo yanayolenga kuhimiza jamii dhidi ya hatua za kudhibiti maambukizi,kutoa hudua kwa waathiriwa na waathirika wa ukimwi,upimaji kwa hiari,matumizi ya kondom na hatua za uboreshaji wa sera zinazohusu ukimwi yalianza kwa maandamano mafupi yaliyopokelewa na mgeni rasmi Naibu meya wa Manispaa ya Temeke.

Kazi za TEYODEN

TEYODEN katika banda lake ilifanya kazi zifuatazo:-

  • Kuelimisha jamii hasa vijana juu ya umuhimu wa stadi za maisha kama nyenzo ya kubadili tabia hatarishi kwa vijana.
  • Kutoa huduma ya kondom bure
  • Kuhamasisha ushiriki wa vijana katika shughuli za upunguzaji wa maambukizi na utoaji huduma kwa wagonjwa.
  • Kuhamasisha jamii juu upingaji wa unyanyasaji wa wanawake hasa vijana na kujenga uwezo wa kina mama wadogo kukabiliana na changamoto zitakazo wapelekea katika maambukizi ya ukimwi.

Mafanikio

  • Wanajamii 78 wakiwemo vijana 56 walitembelea banda na kujifunza masuala muhimu ya upunguzaji wa maambukizi na utoaji huduma kwa waathirika na waathiriwa wa ukimwi
  • Idadi ya kondom 371 zilisambazwa kwa vijana na wanajamii walioudhulia maadhimisho
  • vijarida 217 vilisambazwa kwa vijana na wanajamii waliohudhuria maadhimisho

Mwisho wa maadhimisho haya ni mwanzo wa michakato na mipango mipya juu ya uthibiti wa maambukizi mapya na huduma kwa waathiriwa na waathirika wa Ukimwi.Kila mtu achukue nafasi yake sasa hivi na hapo hapo alipo.Tusiufundishe ulimwengu kuimba tuonyeshe kwa vitendo.

Vijana kutoka TEYODEN wakiwa katika picha ya pamoja katika kikao cha Climate change Don Bosco upanga Dar-es-salaam

Vijana TEYODEN washiriki maadhimisho ya Climate Change Don Bosco,Upanga Dar-es-salaa.

Vijana 20 TEYODEN ( wanaume 10 na wasichana 10) washiriki katika Maadhimisho ya climate change Tanzania yaliyofanyika katika viwanja vya

Don Bosco Upanga   tarehe 8/11/2011

Lengo la mkutano wa Mabadiliko ya hali ya mazingira

  • Kuwaaga vijana wa kitanzania ambao wataambatana na vijana wenzao kutoka nchi 13 duniani kote na nchi zitakazo wakilishwa ni ;-Tanzania, Bangladesh,Botswana,Kenya, Uganda, Kongo drc, Zambia,South Africa,Norway, England, Nigeria, Senegar na Malawi.
  • Kukusanya matamko ya vijana wa kitanzania na yale yajumuiya ya dini ya kikristo pamoja na baraza kuu la waislam tanzania BAKWATA.
  • Kutiwa saini matamko au makubaliano hayo na makamu wa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Mohamed Gharib Bilal ambaye pia ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika shughuli hizo.
  • Kuwatambulisha vijana wengine walio katika safari inayojukana kama Road to Durban watakaohudhulia mkutano mkuu wa climate change utakao fanyika Durban nchinia africa ya kusini .

Katika hotuba yake mgeni rasmi makamu wa raisi Dr Bilal alisema “ Wanadamu tumechafua nyumba zetu sisi wenyewe, hivyo basi nasisitiza kwamba kama tunataka mabadiliko ya kweli ni lazima tuanze kwa kusafisha nyumba zetu tulizo zichafua ndipo tusafishe mazingira yetu.”

Mkutano huu au maazimio uliudhuriwa na vikundi mbalimbali vya burudani navyo ni kikundi mcha sanaa za monesho ya jukwaani na televisheni cha FATAKI kikundi cha vijana wa kusheki mwanamuziki kutoka kenya anayejulikana kama Juliani ambao ni mmoja wa vijana walio katika safari ya road to Durban mwanamuziki wa Tanzania anayeimba mziki wake katika maadhi ya bongo flavour Mwasiti kikundi cha muziki kinacho julikana kama 10 Norway nacho pia kipo katika road to durban na kundi la ngoma ama muziki wa asili kutoka Botswana nao pia wapo katika Road to Durban