Injira
chama cha wazazi wa watoto wenye ulemavu wa mtindio wa ubongo, akili  na viungo Tanzania

chama cha wazazi wa watoto wenye ulemavu wa mtindio wa ubongo, akili na viungo Tanzania

msasani-kinondoni, Tanzania

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

UTAMBULISHO

 Chama cha Wazazi wa Watoto wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo, Akili na Viungo Tanzania (CHAWAUMAVITA) ni chama kilichoanzishwa mwezi Aprili 2012,Tumefanikiwa kupata usajili mwezi april 2013 namba S.A 18732.

Tunaamini-“Umoja daima ndio suluhisho kwa changamoto”

Dira ya CHAWAUMAVITA ni kuwa CHAMA cha mfano kitachochangia upatikanaji wa huduma bora na endelevu kwa watoto wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo, akili na Viungo Tanzania ili kuhakikisha watoto wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo, akili na Viungo wanasaidiwa kukabiliana na changamoto zilizopo na kuandaa mazingira bora ya makuzi na maisha yao kwa ujumla

Malengo ya CHAWAUMAVITA ni

  • Kuwaleta pamoja watu/familia zinazolea watoto wenye ulemavu wa mtindio wa Ubongo,akili na viungo ili kubadilishana uzoefu, kupata elimu ya namna ya kuwatunza watoto wenye ulemavu wa Mtindio wa Ubongo akili na viungo.
  • Kutoa elimu ya ulemavu wa Mtindio wa Ubongo na Viungo ili Kupunguza athari na maumivu yatokanayo na Mtindio wa Ubongo ,akili na viungo.
  • Kukusanya, kuchapisha na kusambaza taarifa zinazohusu matatizo yatokanayo na ulemavu wa Mtindio wa Ubongo,akili na viungo.
  • Kuwasaidia wanachama/wazazi katika kuwatunza na kutetea na kupata haki zao kwa mujibu wa sheria.

Tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwako.Pamoja na salaam, zetu za

Kwa pamoja tukishikamana tutashinda”

large.jpg

meza kuu kazini.......

large.jpg

makamu akikagua maandalizi ya vitafunwa

large.jpg

m/kiti anatoa maelezo

large.jpg

meza kuu makamu m/kiti,wajumbe

large.jpg

wagombea nafasi ya ujumbe kamati ya utendaji chawaumavita,

large.jpg

mjumbe mkuano mkuu akitia msisitizo..........

large.jpg

m/kiti akifungua mkutano mkuu chawaumavita akiwa na meza kuu,shoto ni mhazini.makamu mwenyekiti,na wajumbe

large.jpg

wajumbe mkutano mkuu chawaumavita 18/5/2013

large.jpg

mwenyekiti(aliyesimama)makam mwenyekiti(aliekaa)wakati wa mkutano mkuu