Envaya

Mkakati wa sasa wa asasi yetu ni kuanza shughuli za utoaji tena ellimu kwa watoa huduma za wagonjwa majumbani na kwa watu wanaoendesha shughuli za jando na unyago. Hii ni kwa sababu kipindi hiki kwa mikoa ya kusini ya tanzania ya Mtwara na Lindi ni kipindi cha shughuli hizo za kimila. Hii itasaidia sana kuwafanya watoa huduma hao kuwa na uelewa na tahadhari katika shughuli zao. Miongoni mwa stadi zitakazowezeshwa ni; VVU katika Tanzania, Tohara na faida zake, kuepuka mafundisho yanayochochea vitendo vya ngono kwa wasichana wadogo na namna wazee wanavyopaswa kusikilizwa katika jamii. Wadau wengine watakaoshirikishwa ni viongozi wa kimila, viongozi wa kidini na washauri wa kijadi.

4 Juni, 2012
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.