Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri
SEKTA YA MADINI YAENDELEA KUNG’ARA SINGIDA, SERIKALI YATENGA BILIONI 115 KWA UTAFITI WA KINA
Na Neema Nkumbi – Iramba, Singida
Wachimbaji wadogo wa madini mkoani Singida wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa hatua madhubuti za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha sekta ya madini, zikiwemo ugawaji wa leseni mpya na kuondoa vikwazo vilivyokwamisha maendeleo ya wachimbaji wadogo.
Pongezi hizo zimetolewa Agosti 23, 2025, katika Kongamano la Wachimbaji Wadogo wa Madini wa Kanda ya Kati lililofanyika Sekenke One, Shelui Wilaya ya Iramba, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde.
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema Serikali imejipanga kuongeza kiwango cha utafiti wa kina wa madini kutoka asilimia 16 hadi kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2030, kupitia mkakati wa Vision 2030: Madini ni Maisha na Utajiri.
Kwa ajili ya utekelezaji wa mkakati huo, Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 115, ikiwa ni pamoja na ununuzi wa helikopta maalum kwa ajili ya upigaji picha za anga na ujenzi wa maabara za kisasa zitakazosaidia wachimbaji wadogo kufanya uchambuzi wa madini kwa ufanisi.
"Hatutaki tena kuuza mawe ghafi. Tunalenga kutoka kusafirisha mawe kwenda kuuza bidhaa za madini zilizoongezewa thamani, Hii ni kwa faida ya wachimbaji wadogo, vijana, wanawake na taifa kwa ujumla,” amesema Mavunde.
Waziri Mavunde ameongeza kuwa kampuni kubwa za madini zimeonesha nia ya kuwekeza katika mgodi mkubwa wa dhahabu utakaokuwa katika mikoa ya Singida na Dodoma, hatua ambayo inatarajiwa kuongeza ajira, mapato ya Serikali na kuchochea ukuaji wa uchumi wa kitaifa kupitia sekta ya madini.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amesema kuwa sekta ya madini ndiyo inayoongoza kwa kasi ya ukuaji wa uchumi mkoani humo, ambapo kwa mwaka wa fedha 2024/25, Singida imekusanya zaidi ya shilingi bilioni 26, ikizidi lengo la awali la bilioni 24.
“Zaidi ya tani 2.7 za dhahabu huzalishwa kila mwaka, ambapo tani 1.5 zinatoka kwa wachimbaji wadogo. Huu ni ushahidi kuwa sekta hii imekuwa mkombozi wa wananchi wetu,” amesema Dendego.
Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Mhandisi Sabai Nyansiri, amesema mafanikio hayo yamechangiwa na mazingira rafiki yaliyowekwa kwa wachimbaji wadogo pamoja na usimamizi madhubuti wa shughuli za uchimbaji.
Nyansiri amebainisha kuwa uzalishaji wa madini mkoani Singida umeongezeka mwaka hadi mwaka na kwa sasa sekta hiyo inachangia zaidi ya shilingi bilioni 6 kwa mapato ya Serikali kwa mwaka.
Kwa mujibu wa wachimbaji hao, hatua ya Serikali kufuta leseni 2,648 ambazo zilikuwa hazitumiki na kuzigawa upya kwa wachimbaji wadogo kumesaidia kupunguza migogoro ya maeneo na uchimbaji holela, hivyo kufungua ukurasa mpya wa tija na uwajibikaji katika sekta hiyo muhimu.
Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA), Bw. John Bina, amesema zaidi ya wachimbaji wadogo milioni 6 wanashiriki kikamilifu katika shughuli za madini nchini na kuchangia takriban asilimia 40 ya mapato ya sekta hiyo.
“Tunatambua dhamira ya dhati ya Rais Samia katika kuwatambua na kuwawezesha wachimbaji wadogo, Hii ni heshima kubwa kwetu, na ndiyo maana leo tunasherehekea mafanikio haya,” amesema Bina.
Bw. Bina, ametoa rai kwa serikali kutumia fursa ya amani na utulivu nchini kujenga soko kubwa la madini ndani ya Tanzania.
“Tunaamini tunaweza kupata Dubai yetu hapa nyumbani Tukijenga soko hapa, wachimbaji watanufaika zaidi na kodi zitabaki nyumbani,” amesema Bina.
Maoni (0)
WACHIMBAJI MKOA WA SINGIDA WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA MAFANIKIO MAKUBWA SEKTA YA MADINI
▪️Wapongeza ugawaji wa Leseni kwa wachimbaji wadogo Singida
▪️Singida wavuka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli
▪️Waziri Mavunde aeleza mkakati wa kuongeza eneo la utafiti wa kina madini nchini
▪️Kampuni za madini zajipanga kuanzisha Mgodi Mkubwa wa Dhahabu kanda ya Kati (Dodoma & Singida)
📍 Iramba – Singida.
Wachimbaji Wadogo wa Madini Mkoa wa Singida wamepongeza jitihada kubwa za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta ya madini, ikiwemo kugawiwa leseni na kuwekewa mazingira bora ya kufanya kazi zao kwa amani.
Pongezi hizo zimetolewa leo Agosti 23, 2025 wakati wa Kongamano la Wachimbaji Wadogo wa Madini wa Mkoa wa Singida na Kanda ya Kati, lililofanyika katika eneo la Sekenke One, Shelui – Wilaya ya Iramba, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde.
Wachimbaji hao wameleza kuwa, hatua ya Serikali kufuta na kurudisha Serikalini leseni na maombi 2,648 ambayo hayakuwa yakifanyiwa kazi, kisha kugawiwa upya kwa wachimbaji wadogo, imekuwa suluhisho la muda mrefu kwa changamoto ya kuvamia maeneo na kuchimba bila leseni.
Akizungumza katika Kongamano hilo, Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amesema mpango wa Serikali ni kuongeza kiwango cha utafiti wa kina wa madini kutoka asilimia 16 kilichopo sasa hadi kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2030, kupitia maono ya Vision 2030; Madini ni Maisha na Utajiri.
Amesema kuwa, Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 115 kwa ajili ya utafiti wa madini nchini, ikiwa ni pamoja na kununua helikopta maalum yenye vifaa vya kisasa kwa ajili ya upigaji picha na utafiti wa anga, sambamba na ujenzi wa maabara za kisasa za uchambuzi wa madini zitakazotumika na wachimbaji wadogo.
Wakati huohuo, Waziri Mavunde amebainisha kuwa Kampuni kubwa za madini zimeanza kujipanga kuwekeza katika Mgodi mkubwa wa dhahabu katika Kanda ya Kati (katika mikoa ya Dodoma na Singida), hatua inayotarajiwa kuongeza zaidi fursa za ajira, mapato ya Serikali na mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa.
Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA), Bw. John Bina, alisema zaidi ya wachimbaji wadogo milioni 6 wanashiriki kikamilifu katika shughuli za madini na wamefanikisha sekta hiyo kuchangia hadi asilimia 40 ya mapato yote ya madini nchini.
“Tunampongeza Rais Samia kwa maono yake ya kuendelea kuithamini sekta ya wachimbaji wadogo. Hii ni heshima kubwa kwetu na ndiyo maana leo tunasherehekea mafanikio haya,” alisema Bina.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, alisema sekta ya madini ndiyo inayoongoza kwa kasi ya ukuaji kiuchumi ndani ya mkoa huo na imewezesha Singida kuvuka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali.
“Madini ndiyo injini ya uchumi wa Singida, na kwa sasa mchango mkubwa unatoka kwa wachimbaji wadogo waliowekewa mazingira bora ya kufanikisha kazi zao,” amesema.
Awali, akizungumza katika kongamano hilo, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Mhandisi Sabai Nyansiri, amesema mkoa huo umefanikiwa kuvuka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali yatokanayo na sekta ya madini katika mwaka wa fedha 2024/25, baada ya kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 26 dhidi ya lengo la shilingi bilioni 24.

WAZIRI LUKUVI ATOA MAAGIZO YA RAIS SAMIA AJALI YA MGODI NYANDOLWA

Waziri wa nchi Ofisi ya waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge William Lukuvi akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa maagizo kwa viongozi wa Serikali waliopo maeneo ya ajali ya mgodini kushiriki taratibu zote za mazishi kwa walifariki ajali ya mgodini na kuwakilisha rambirambi zake kwa wahusika huku akisihii kuendelea kuratibu vyema shughuli ya uokoaji inayoendelea.
Ameyasema hayo wakati wa kikao na viongozi pamoja na ndugu wa waathirika wa ajali ya mgodini katika eneo la tukio la ajali ya mgodi unaomilikiwa na Kikundi cha Wachapakazi katika machimbo ya Nyandolwa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
![]() |
“Rais Samia kaniagiza kuwafikishia salamu za pole na rambirambi pia kanituma kuleta maagizo kwa viongozi wa serikali waliopo eneo hili kuhakikisha wanahudhuria misiba yote ya watu waliopoteza maisha katika ajali hii na kuwakilisha rambirambi alizotoa katika familia hizo” amesema Lukuvi.
Agosti 16, 2025 Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro alitoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Dk. Kalekwa Kasanga kufanya utaratibu wa kuweka ofisi ya muda ya mtendaji wa kijiji katika eneo la tukio la ajali ambayo itatumika kuwasajili wageni waliokuja kusubiri ndugu zao kwa ajili ya kuhudumiwa na serikali.
Mnamo Agosti 18, 2025 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita alitoa maelekezo kwa familia zilizokuja kusubiri ndugu zao, kuchagua wawakilishi wawili au watatu ambao watabaki ili iwe rahisi kwa serikali kuhudumia familia hizo na kupewa mahitaji muhimu.
Aidha, Agosti 11, mwaka huu watu 25 walifukiwa na Mgodi wa Kikundi cha Wachapakazi katika Machimbo ya Nyandolwa na hadi sasa watu 11 wametolewa huku watatu wakiwa hai na nane wakiwa wamefariki, na juhudi za kuendelea kuwatoa wengine 14 zinaendelea kwa kasi kwa kutumia mashine za utambuzi wa ardhini kujua maeneo waliopo.
HUHESO FOUNDATION IN ATTENDED THE TRAINING ABOUT FUND RISING AND PROJECT WRITING AT MBEZI GARDEN HOTEL.
On getting some of training we get more experience how to get Fund and project writing in different projects. You can view more photo for the training at Mbezi Garden Hotel in Dar es salaam.
Here are members who attended the training at Mbezi Garden Hotel.
Some of members who attended the training at Mbezi garden Hotel in Dar es salaam.