Envaya

Translations: English (en): User Content: dMFIJBXoGL9sZo3FIrxEkrqZ:content

Base (English) English
Nashukuru kwa ujumbe wako mzuri ambao kwa kiwango kikubwa umenifunza mengi
na kunionesha njia. Nikweli kabisa tatizo la vijana katika nchi yetu
halitotatuliwa kwa propaganda za kisiasa ama maneno matupu bali linahitaji
kujitoa mhanga na kuonesha moyo wa kipekee wa uzalendo wa
kuwafunza/kuwaelimisha vijana na kuibadili mitazamo hasi ambayo ni mitazamo
funge ya fikra na kupandikiza mitazamo chanya ambayo inazaa matunda ya heri
na fanaka. Vijana wa tanzania wanahitaji msaada wa kifikra ambao utawaondoa
pangoni na kuwaleta kwenye mwanga, tunahitaji kujitolea kwa hili na
kuonesha ushirikiano na jamiii itatufuata baada ya kuona mafanikio. Sisi
wana AUVITA tuko tiari kabisa kushiriki nanyi katika ukombozi huu wa vijana
kwani ndiyo dhamira yetu kuanzisha asasi hii hivyo kwa hili tuko pamoja na
wala hatutarudi nyuma. Pia umesema kuwa mumeshafanya mafunzo mbalimbali na
matini munayo naomba utusaidie matini hayo ili tuyatumie pia kuwakomboa
vijana wa mtwara ambao kweli dunia inaonesha kuwatupa mkono maana hofu
waliyonayo vijana inahitaji jitihada kuwakomboa kifkra.

Wako,

Simba Mramba.


2014-06-11 15:36 GMT+03:00 Envaya :
(Not translated)

In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register