Injira

Ubusobanuro: Kiswahili (sw): User Content: WI000E63A0BB0BC000000852:content

« Inyuma   ·   Ahakurikira »
Base (Igiswayire) Kiswahili
MRADI WA HAKI ZA MWANANCHI

NURU CLUB

TAARIFA YA TAMASHA LA UELIMISHAJI JAMII `JUU YA UPIMAJI WA HIARI , UNYANYAPAA,UNYANYASAJI PAMOJA NA HAKI ZA WATU WAISHIO NA VVU/ UKIMWI


MAY 2010

YALIYOMO uk:

1. Utangulizi……………………….…3

2 Lengo kuu la mradi…………….…3

3 Madhumuni………………………4

4 Walengwa. ………….……………4

5 Shughuli zilifanyika… …….……..4

6 . Mbinu zilizotumika………..…..…5

8. Waelimishaji……………….……..5

9 Mafanikio………………….……..6

10 Matatizo………………………..…7

11. Mambo tuliyojifunza ………...….8

12 Matarajio…………..……………8




NURU CLUB

MRADI WA HAKI YA MWANANCHI

TAARIFA YA TAMASHA LA UELIMISHAJI JAMII JUU YA UPIMAJI WA HIARI , UNYANYAPAA,UNYANYASAJI PAMOJA NA HAKI ZA WATU WAISHIO NA VVU/ UKIMWI. MAY 2010.

NURU CLUB ni asasi ya watu wanaoishi na VVU/UKIMWI,asasi hii ni mdau kwenye kutekeleza mradi wa haki za mwananchi unaoisimamiwa na shirika la AMREF chini ya ufadhili wa shirika la nchini Uingereza lijulikanalo kama DFID.

Mradi huu unafanyika katika kata tatu ambazo ni Kiwalani iliyopo Ilala , Tandale na Manzese zilizopo katika wilaya ya Kinondoni.

LENGO KUU LA MRADI WA HAKI ZA MWANANCHI:
Ni kuboresha upatikanaji wa huduma za afya ,matibabu pamoja na matunzo kwa watu wanaoishi na VVUna UKIMWI na wale wanaoathiriwa na UKIMWI hasa wanawake ,viziwi pamoja na wale wanaofanya biashara za ngono.

Katika kutekeleza mradi huu asasi ya NURU iliendesha mafunzo ya siku mbili ya jinsi ya kuishi kwa matumaini kwa watu 75. Mafunzo haya yalifanyika katika kata tatu ambapo mradi unalenga.Tuliweza kuwafundisha wanawake 53 na wanaume 22.

LENGO LA MATAMASHA YALIYO FANYIKA:.
Kwanza kabisa ni kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa kupima afya hasa tukilenga upimaji wa hiari wa VVU.
Pili kuelimisha jamii juu ya athari na madhara yanayoweza kusababishwa na unyanyapaa na unyanyasaji wa aina yeyote kwa mtu yeyote lakini tukitia msisitizo zaidi kwa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI ,
Tatu kuelimisha juu ya haki na wajibu kwa jamii juu ya suala la ukimwi pia kuwafahamisha juu ya sheria mpya ya UKIMWI ya mwaka 2008

MADHUMUNI YA TAMASHA:-
Kuchangia Kuondoa / kupunguza / kutokomeza unyanyapaa na ubaguzi miongoni mwa wanajamii ili kuboresha upatikanaji wa haki hasa kwa watu wanaoishi na VVU NA UKIMWI.

WALENGWA
Wananchi wa kata za Kiwalani ,Manzese na Tandale pamoja na watu wanaoishi na VVU na UKIMWI waliopo katika eneo la mradi.

SHUGHULI ZILIZOFANYIKA:-
A.Kutoa elimu kwa jamii

MADA ZILIZOFUNDISHWA.
1.Umuhimu wa kupima VVU, hapa tulielezea faida na hasara zake.
Hapa mafunzo yalilenga zaidi ukweli kuhusu swala zima la ugonjwa wa ukimwi kuanzia njia za maambukizi,njia za kujikinga,tulifundisha haya ili kumpa mtu nafasi ya kufanya maamuzi yaliyo sahihi

2.Madhara ya unyanyapaa /unyanyasaji.
Hapa tuelezea maana ya unyanyapaa pamoja na aina za unyanyapaa.

3. Tulizungumzia suala la haki na wajibu kwa jamii pamoja na kwa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.
Hapa tulifundisha haki za msingi za watu wanaoishi na VVU / UKIMWI,tulieleza kwamba kupata maambukizi ya VVU hakuzuii haki za msingi kwa binadamu yoyote.
Tunaposema haki za binadamu ni pamoja na haki ya kuishi, kuheshimiwa , kupata watoto , kuoa na kuolewa,kumiliki mali,kwenda kokote unakota,kuishi popote,haki ya kupata matibabu, pamoja na kushiriki kwenye mambo yote yanayohusu jamii bila kubaguliwa au kuvunja sheria.

4. Tuliangalia sheria ya UKIMWI ya mwaka 2008 sehemu ya 7 na ya 8 sehemu ambazo zinazungumzia juu ya unyanyapaa pamoja na haki na wajibu kwa jamii pamoja na watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.

Mbinu zilizotumika kufundishia ;
1. Kuwezesha, kuelezea mada
2. Kuuliza na kuulizwa maswali.
3. Mashindano ya kucheza kiduku ambapo yalivutia watu wengi sana.
4. Watu wanaoishi na VVU kutoa shuhuda kuelezea historia zao tangia walipotambua afya zao.

Waelimishaji kwenye tamasha

1. Elizabeth sangu Mshauri /TOT
2. Msafiri thomas Mshauri /TOT

Wawezeshaji hawa wamepatiwa mafunzo mbalimbali kupitia program za AMREF,PASADA, HPI(health policy initiative) ambapo hawa ni TOTs kwenye mambo ya HIV/AIDS.

B. Upimaji wa VVU wa hiari.
Tulifanya matamasha mawili makubwa moja katika Wilaya ya Ilala kata ya Kiwalani na tamasha lingine lifanyikia Wilaya ya Kinondoni likihusisa kata za Tandale na Manzese. Shuguli hii ilitoa mafanikio yafuatayo hapa chini:-
Kiwalani tulitoa elimu kwa watu wapatao 1000.
Waliopima ni watu 232, Wanawake 92 na Wanaume 140.
Waliokutwa wana maambukizi ya VVU ni wanawake 11 na wanaume 12 ambapo idadi yao ni watu23.
Tandale na Manzese tulitoa elimu kwa watu takriban 1500 na kati yao 206 walipima VVU ambapo wanaume walikua 127 na wanawake 79.Maambukizi ya VVU yalikuwa kama ifuatavyo :-Wanawake 7 na wanaume 6 walioonekana wana maambukizi ya VVUna kufanya idadi ya wenye maambukizi kuwa 13.
Kwa ujumla kwenye matamasha yote mawili tulitoa elimu kwa watu 2500. Waliopima ni 438 wakiwemo wanawake 171 na wanaume 267. Waliokutwa wana maambukizi ni 36 wakiwemo wanawake 18 na wanaume 18.

WALIOKUWA WANATOA HUDUMA YA UPIMAJI NI :-
Washauri nasaha wawili kutoka Angaza Zaidi wakishirikiana na washauri wawili kutoka NURUCLUB ambao ni :-Elizabeth Sangu na Fortunatha Lyuki.

Mafanikio / Changamoto / matatizo
MAFANIKIO
1.Kwa Kupitia matamasha haya tumeweza kuamsha hisia za wengi ambao walikuwa hawaelewi lolote kuhusu haki na wajibu walionao katika jamii,hivyo wameweza kujitokeza na kuuliza maswali mengi na hatimaye kufikia maamuzi ya kwenda kupima afya zao.

2.Mafanikio mengine ni pamoja na mwitikio wa watu kuja kupima ambapo kwa matamasha yote mawili tuliweza kutoa elimu kwa watu 2500 ambapo waliopima ni 438 wakiwemo wanawake 171 na wanaume 267. Waliokutwa wana maambukizi ni 36 wakiwemo wanawake 18 na wanaume 18.

3.Watu waliohudhuria walipata elimu mbalimbali iliyotolewa hivyo wakaweza kutambua mambo ambayo hawakuwa wanayaelewa ikiwemo haki na wajibu wa jamii ,unyanyapaa na unyanyasaji kuhusiana na masuala ya ukimwi.

4.kiongozi wa serikali ya mtaa wa Yombo Kiwalani Ndugu Ignas Maembe alipata nafasi ya kuzungumza na wananchi na kuwaasa kuhusu kuzingatia elimu iliyotolewa pia akawaomba wajitunze kwani hali ya maambukizi inazidi kuongezeka.Pia aliwaonya wale ambao wanawaambukiza wenzao kwa makusudi waache tabia hiyo mara moja kwani kufanya hivyo ni kurudisha nyuma harakati za mapambano dhidi ya UKIMWI.

MATATIZO YALIYOJITOKEZA

1.Wenzetu wa wilaya ya Temeke waliweza kudai kushiriki kwenye mafunzo kwani wote ni wanachama wa NURU.

2.Tulishindwa kufanya shughuli kulingana na mpango kazi kutokana na kucheleweshewa fedha na mfadhili

3.Kulikuwa na mfumuko wa bei hivyo kulitikisa kidogo bajeti yetu.

4.Baadhi ya washauri nasaha wa Angaza zaidi walikataa kusaidiana na NURUCLUB kwenye zoezi la upimaji kwa sababu malipo yalikuwa ni madogo.

4.Baadhi ya viongozi wa serikali hawakutoa ushirikiano wa kutosha hata baada ya kuwapatia taarifa rasmi ya shughuli zilizokuwa zinatekelezwa ndani ya mitaa yao kuhusu mradi wa haki za mwananchi..

MAMBO TULIYOJIFUNZA / KUGUNDUA.

1.Tumegundua kwamba katika eneo la Kiwalani,Manzese na Tandale kuna watu wanaofanya biashara ya ngono na wasenge.

2.Tumegundua kwamba jamii ikipelekewa huduma ya elimu na upimaji wa VVU karibu hujitokeza kwa wingi zaidi kuliko kufuatilia huduma hiyo kwenye vitu maalumu.

3.Masuala ya imani za dini zinakwamisha harakati za mapambano dhidi ya UKIMWI.

MATARAJIO YETU/MAPENDEKEZO.
Kutokana na uzoefu tulioupata tungependa kurudia baadhi ya shughuli tulizotekeleza kwenye mradi mwaka huu kwenye mwaka ujao kutokana matokeo yake kuwa na manufaa makubwa na wanajamii kuomba turudi tena kwa ajili ya huduma kama hiyo.
(Not translated)

Kugirango ugire icyo uhindura kubyo wasemuye, ugomba kwinjira mu rubuga Injira · Iyandikishe