Injira
Wasaidizi wa kisheria Masasi

Wasaidizi wa kisheria Masasi

Masasi, Tanzania

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Icyongereza. Edit translations

Asasi kwa kushirikiana na wanaasasi wae imeandaa mafunzo ya sheria ya malezi ya mtoto 

kwa wanajamii wa kata ya Mpeta. Mafunzo hayo yamelengwa kuwasaidia wanajamii kuweza kufahamu umuhimu wa malezi kwaa mtoto na sheria zinazohusu masuala hayo. Mafunzo hayo

yatafanyika kati tarehe 10-14 za mwezi wa Septemba mwaka huu wa 2105 kwenye zahanati ya Mpeta. Wawezeshaji watakuwa ni Yakobo Mchopa, Mwanaafa Malenga, Anjelina Saidia na Thecla Mbawala.

Ni matumaini yetu kuwa wananchi wa kata hiyo na vijiji jirani wataweza kuhudhuria na kupata elimu hiyo itakayotolewa bure.

kwa kuwa harakati za kampeni za uchaguzi mkuu zimeanza wakihabima imejipanga kufanya ufuatiliaji. basi kila mwanachama anapaswa kuwa tayari pale alipo kujiwekea ratiba itakayomsaidia kuona shughuli zinafanyika kwa misimgi ya haki na sheria
Asasi ilihudhuria warsha ya mafunzo ya siku 5 huko Morogoro iliyoandaliwa na LHRC. Waliokwenda huko walikuwa ni; Mr Tanmoza Fungafunga-M/kiti, Bi Irene Liumba- M/hazina na wajumbe Edna Ngasiwa, Yakobo Mchopana Maurice Nghitu.
Washema imetakiwa kubadili jina lake na kuwa WAKIHABIMA kufuatia ushauri wa kisheria toka kwa msajili ili kuepuka mgongano wa jina na asasi nyingine yenye jina kama hilo kwenye daftari la msajili wa Ngo's.Hivyo asasi hii sasa inatambuliwa kwa jina hilo.
Asasiya Washema ipo kwenye mchakato wa kupata usajili wa kudumu. Katiba imepele kwa msajili wizara ya Maendeleo ya jamii, jinsia na watoto.
Washema kwa sasa inaendesha mikutano ya kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.Mikutano hii pia inafanya shughuli za kubaini changamoto zinazoweza kujitokeza katika zoezi hilo.Kata husika ni Lukuledi, Nanganga na Chiungutwa na imeanza Machi 1na kuendelea hadi mwezi Juni.

Washema imeendelea na shughuli zake za kutoa huduma za usaidizi wa kisheria na haki za binadamu. Wanachama wake wamesaidia jamii kwa kutoa elimu juu yamasuala ya kisheria katika kata za Nanganga, Chiungutwa, Mchauru, Namalenga, Mkomaindo na Lukuledi. Aidha kwa sasa inafanya utafiti wa kubaini makundi ya wanawake, vijana na walemavu ambao wanakosa fursa ya kugombea katika chaguzi mbalimbali. Utafiti na uibuaji huo umelenga kata za Chiungutwa, Nanganga na maeneo ya Mji wa Masasi. Baada ya utafiti huo kutaandaliwa mpango mkakati wa kuwezesha walengwa hao kujengewa uwezo ili waweze kushiriki na kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa Dec 2014 na udiwani na ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 na kuongeza idadi ya wale wachache waliopo. Katika mradi huo Washema itahusisha asasi zingine zinazoshiriki katika masuala ya kujengea uwezo na utoaji wa elimu ya uraia.

Washema ilipata mwaliko wa kuhudhuria tamasha la Kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC ambapo washiriki 2 walihudhuriatoka23hadi24 Septemba2014.