Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

DKT. BITEKO AMWAKILISHA RAIS SAMIA MAZISHI YA HAYATI ASKOFU SHAO

1000778707.jpg


📌 Awataka Watanzania kuacha alama katika utumishi wao


📌 Asema Serikali iko pamoja na wafiwa katika kipindi hiki cha majonzi


📌 Askofu Malasusa ataka waumini kumshuhudia Kristo kwa vitendo



Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ibada ya mazishi ya Askofu Mstaafu Dkt. Martin Fatael Shao aliyefariki Dunia Agosti 25, mwaka huu.


Akizungumza katika ibada ya mazishi Septemba 4, 2025 yaliyofanyika katika kijiji cha Lole, Wilaya ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro Dkt. Biteko amesema Hayati Askofu Shao wakati wa uhai wake alifanya mambo mengi mazuri ya kukumbukwa hata baada ya kifo chake.


“ Mzee wetu, Hayati Askofu Shao ameanza kazi za kanisa akiwa kijana na amefanya kazi kubwa ambayo kila mmoja anaishuhudia leo, ameacha alama inayotokana na kazi aliyoifanya, amesema


“Mheshimiwa Rais amenituma niwaletee salamu zake za pole nyingi sana Wanafamilia, Viongozi wote wa Kanisa KKKT pamoja na ndugu jamaa na marafiki wote kwa na msiba” amesema


Amesema Serikali itakumbuka mchango wa Askofu Shao ambaye ametumikia Kanisa katika maisha yake tangu ujana wake na hata baada ya kustaafu ameendelea kuwa mshauri.


Amewahimiza waombolezaji kuendelea kuwa karibu na kushirikiana na wafiwa katika kipindi hiki cha majonzi huku akiwahakikishia kuwa Serikali iko pamoja nao hasa katika kipindi hiki cha majonzi.


Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT, Dkt. Alex Malasusa amewataka waumini kutumia msiba huu kumshukuru Mungu kwa ajili ya mtu kama hayati Askofu Shao ambaye alikuwa kielelezo cha maisha bora kwa wanadamu.


Ameongeza kuwa Hayati Askofu Shao akikuwa mnyenyekevu na msikivu hali ambayo amesema imeanza kutoweka miongoni mwa wanajamii


“wanyenyekevu kama Dkt. Shao wameanza kuwa hadimu katika jamii na Viongozi waliomtengeneza Hayati Dkt. Shao walifaulu sana… amefanya mambo mengi ndani na nje ya usharika” amesema Askofu Dkt. Malasusa.


Amefafanua kuwa Askofu Shao enzi za uhai wake akifanya kazi kubwa ya uinjiliahaji ndani na nje ya mipaka ya Tanzania kwa umahiri mkubwa.



“ Tusizoee misiba, kila msiba utupe nafasi ya kutafakari maisha yetu,” amesema Askofu Malasusa.


Ibada ya mazishi imehudhuriwa na maelfu ya waombolezaji na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, Mkuu wa Mkoa wa Kilimajaro, Nurdin Babu na Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CHAUMMA, Salum Mwalimu.


1000778707.jpg
1000778704.jpg
1000778705.jpg
1000778706.jpg
1000778708.jpg
1000778709.jpg
1000778710.jpg
1000778711.jpg
1000778712.jpg
1000778713.jpg
1000778714.jpg


MWISHO

NCHIMBI AAHIDI KUANZISHA MASHAMBA DARASA YA KISASA KAHAMA, AJIRA NA HUDUMA BORA

1000777713.jpg


Na neema Nkumbi - Kahama, Shinyanga


Mgombea mwenza wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameahidi kuanzisha mashamba darasa 60 kwa ajili ya kufundisha wakulima na wafugaji mbinu bora za kilimo na ufugaji wa ng’ombe wa kisasa endapo chama hicho kitaaminiwa kuendelea kuongoza nchi.


Akihutubia maelfu ya wananchi katika kata ya Kagongwa, Manispaa ya Kahama, Dkt. Nchimbi amesema mashamba darasa hayo yatakuwa chachu ya kuongeza tija kwenye kilimo, kuimarisha mifugo na kuinua kipato cha wananchi hususan vijana na wakulima wadogo.


Mbali na mashamba darasa, alibainisha kuwa serikali ya CCM itatekeleza miradi mingine ya maendeleo ikiwemo skimu nne za umwagiliaji, ujenzi wa masoko ya mazao, vituo vinne vya afya, pamoja na shule sita za msingi na shule mbili za sekondari.


Nchimbi amesema serikali ya CCM itaajiri walimu 7,000 na watumishi wa afya 5,000 ili kupunguza changamoto ya upungufu wa watumishi kwenye sekta hizo muhimu huku akiongeza kuwa vijana na wajasiriamali watawezeshwa kupitia mikopo ya shilingi bilioni 2,00 kwa ajili ya kurasimisha biashara zisizo rasmi na kukuza uchumi wa wananchi.


Aidha, mgombea mwenza huyo ameahidi kuwa endapo chama chake kitaaminiwa kupewa uongozi ndani ya siku 100 za mwazo watahakikisha wanawake wajawazito, wazee, wenye ulemavu na watoto watapatiwa huduma ya bima pia kushughulikia kero ya muda mrefu ya Barabara ya Tabora.


Dkt. Nchimbi amewasili Kahama akitokea Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kufungua kampeni za CCM na kusisitiza kuwa chama hicho kitaendelea kuboresha maisha ya wananchi kupitia utekelezaji wa sera na ilani yake.

1000777713.jpg
1000777727.jpg
1000777735.jpg
1000777737.jpg
1000778115.jpg
1000777703.jpg
1000777723.jpg
1000777717.jpg
1000777743.jpg
1000777733.jpg
1000777731.jpg
1000777711.jpg
1000777719.jpg
1000777741.jpg
1000777721.jpg
1000777745.jpg
1000777685.jpg
1000777689.jpg

MBIO ZA KUKINADI CHAMA CHA MAPINDUZI MKOANI GEITA ZAANZA KWA KISHINDO

1000772438.jpg
1000772440.jpg
1000772439.jpg
1000772441.jpg
1000772442.jpg



📌 Majimbo 7 kati ya 9 yapita bila kupingwa


📌 Kata 92 kati ya 122 zapita bila kupingwa


📌 Maelfu wakusanyika kusikiliza Ilani ya CCM 2025-2030


📌 Dkt. Biteko awasisitiza wananchi kujitokeza kwa wingi kumpigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan


📌 Asisitiza mshikamano kabla na baada ya uchaguzi


Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Geita leo Septemba 2, 2025 kimezindua kwa kishindo kampeni za kuinadi Ilani ya CCM 2025-2030 kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ambapo imeelezwa kuwa mpaka sasa tayari Majimbo 7 kati ya 9 ya Ubunge yamepita bila kupingwa huku kata 92 kati ya 122 zikipita bila kupingwa.


Mgeni rasmi katika uzinduzi huo uliofanyika katika Kata ya Uyovu Wilaya ya Bukombe, Mkoani Geita ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa huo, Nicholaus Kasendamila amesema Chama cha Mapinduzi kinaingia kwenye kampeni kikiwa na mtaji mkubwa wa uadilifu, uaminifu, uchapakazi na busara ya mgombea Urais wa kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Amesema kupitia kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, CCM inazo sababu za kuomba ridhaa ya wananchi kuendelea kuongoza nchi akisema kuwa amefanya maendeleo mengi ikiwemo uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam ambayo ni lango kubwa la biashara kwaTanzania na nchi jirani, amejenga daraja refu la Busisi, amekamilisha ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere (MW 2,115) na reli ya kisasa imeshaanza kufanya kazi.


Kasendamila amesema kuwa katika Mkoa wa Geita, Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020-2025 imetekelezwa kwa mafanikio ambapo ameeleza kuwa shule mpya za msingi 151 zimejengwa, Shule za sekondari mpya 118 zimejengwa, zimejengwa hospitali mbili za rufaa, hospitali za wilaya mpya 4 na vituo vya afya 17 vipya vimejengwa.


Ameongeza kuwa, kupitia Ilani ya CCM 2020-2025, zahanati 69 zimejengwa, leseni za madini 7600 zimetolewa kwa wachimbaji wadogo na kuhusu umeme, kabla ya kuingia kwa Serikali ya Awamu ya Sita kulikuwa na vijiji 362 tu vyenye umeme lakini sasa vijiji vyote 486 mkoani Geita vina umeme.


Kuhusu miundombinu ya Barabara amesema Barabara za lami na changarawe zimeendelea kujengwa mkoani Geita ili kurahisisha usafiri wa wananchi.


Ametaja vipaumbele vya CCM katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuwa ni pamoja na kuongeza fursa za wananchi kujiimarisha kiuchumi, kuendeleza sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, madini, umeme n.k


Mwenyekiti huyo wa CCM, ameomba wananchi waipigie kura CCM kwani kura zao zitafanyiwa kazi kupitia maendeleo.


Akizungumza kwa niaba ya Wagombea nafasi ya Ubunge mkoani Geita, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambaye ni Mbunge Mteule wa Jimbo la Bukombe, amewashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi wa kampeni akieleza kuwa ni ishara ya Wananchi kukipenda Chama cha Mapinduzi na kuridhika na kazi zinazofanywa na Dkt. Samia suluhu Hassan.


Amesema uchaguzi wa mwaka huu utapeleka salaam ndani ya nchi na kimataifa kuhusu uwepo wa demokrasia nchini hivyo amewaasa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura akiahidi kuwa maendeleo wanayoyaona sasa ni rasharasha tu kwani maendeleo makubwa zaidi yanakuja.


Amesema Mkoa wa Geita unazidi kukua ambapo kwa sasa umekuwa ni moja ya mikoa mitano yenye uchumi mkubwa nchini ni mkoa namba moja kwa kuzalisha dhahabu, umekuwa ni mkoa kiungo kwa maeneo mengine nchini na watu wake ni wachapakazi hivyo watampigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kupata maendeleo zaidi.


Kuelekea uchaguzi Mkuu 2025, Dkt. Bitelo amesisitiza kuwa uchaguzi huo uunganishe wananchi badala ya kutenganisha, kuwe na kampeni za kistaarab na Chama cha Mapinduzi kuendelea kufanya kazi kwa umoja.


"Uchaguzi huu ni kwa ajili ya maendeleo yetu, tunataka barabara bora, umeme, afya, mitaji ya biashara, tusiuchukulie poa uchaguzi huu kwani maana kubwa kwenye maisha yetu," Amesisitiza Dkt.Biteko


Akizungumzia maendeleo mbalimbali yaliyofanywa katika Jimbo la Bukombe, Dkt. Biteko amesema, chini ya uongozi wa Dkt.Samia Suluhu Hassan Bukombe sasa kunajengwa Chuo cha VETA ambacho kitawezesha vijana kupata ujuzi wa aina mbalimbali pia Chuo cha Uhasibu Arusha kimeanzisha tawi wilayani Bukombe.


Ameongeza kuwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan amezigusa sekta zote kimaendeleo akitolea mfano Shule za msingi sasa zimefikia 104, shule za sekondari zimefikia 25 na shule za sekondari kidato cha tano na sita zimefikia 5 huku umeme ukifika kwenye vijiji vyote.


Ameongeza kuwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewezesha ujenzi wa kituo kikubwa cha kuzalisha umeme wa jua wa megawati 5 wilayani Bukombe, kikiwa ni cha pili kwa ukubwa ukiacha kituo cha namna hiyo kilichopo Kigoma pia anajenga barabara ya lami kutoka Ushirombo hadi Katoro.


Katika hatua nyingine Dkt. Biteko amewaasa wananchi kujitokeza kwa wingi kumpokea mgombea mwenza wa Kiti cha Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye anatarajiwa kuanza ziara mkoani Geita tarehe 5 Septemba 2025.


Awali, Katibu wa CCM Mkoa wa Geita, Alexandarina Katabi amesema Mkoa wa Geita una mtaji wa wapiga kura waliojiandikisha takriban 1,532,408 huku Wanaccm waliojiandikisha wakiwa ni 524,000 ikiwa ni mtaji wa nusu ya wananchi waliojiandikisha.


Amesema katika Mkoa wa Geita, Majimbo yanayogombewa ni 9 na kata ni 122.


Ameongeza kuwa katika Majimbo hayo 9 majimbo 7 tayari yamepita bila kupingwa na katika kata 122 tayari kata 92 zimepita bila kupingwa na zilizobaki ndizo zenye wapinzani.


Mwisho.

MGOGORO WA MIPAKA YA CHUO CHA MAENDELEO MWAMVA WAPATIWA UFUMBUZI

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif









Na Neema Nkumbi

Mgogoro wa muda mrefu kuhusu mipaka ya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mwamva kilichopo Manispaa ya Kahama, sasa umepatiwa ufumbuzi.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Deogratius Ndejembi, amewataka wananchi waliokuwa wamesahaulika katika takwimu alizopewa hayati Dkt. John Magufuli kuwa eneo la ekari 40 ndilo litakalobaki katika mipaka ya chuo hicho, waendelee na shughuli zao za ujenzi na maendeleo kwenye maeneo yao, huku akisisitiza kuwa wale waliovamia eneo hilo baada ya kauli ya hayati Magufuli, sheria itachukua mkondo wake.

Akizungumza kwa njia ya simu kupitia Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, Waziri Ndejembi amesema atatuma timu ya wataalamu kuja kuhakiki ili kila mwenye haki apate haki yake.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa Mhita amewataka wananchi kuwa na amani kwani changamoto hiyo sasa imepata mwarobaini, na akawahakikishia kuwa wako huru kuendeleza maeneo yao.

Wananchi waliozungumza mara baada ya maelekezo ya waziri wametoa shukurani na pongezi zao kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Mmoja wa wananchi, Paul Andrea, amesema: "Tunamshukuru sana Rais Samia, zamani tulikuwa tunaitwa matapeli, sasa tuko huru."

Aidha, mstaafu wa Jeshi la Magereza, Mzee Gregory Kachemba, ameonyesha furaha yake kwa hatua hiyo, akisema alimaliza mafao yake ya kustaafu kwa kujenga nyumba na kuanzisha maendeleo katika eneo hilo, hivyo kupata suluhisho la mgogoro huo ni faraja kubwa kwake.




transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif


SERIKALI YAAHIDI TAA ZA BARABARANI KUPUNGUZA AJALI KAHAMA

vlcsnap-2025-09-01-15h32m30s076.png


Na Neema Nkumbi - Huheso Digital Kahama


Serikali wilayani Kahama kupitia Jeshi la Polisi imejipanga kusimika taa za kuongozea magari katika maeneo ya Lumambo, Bijampora na Phantom, ili kupunguza msongamano na ajali zinazochangiwa na ukosefu wa mwongozo rasmi wa vyombo vya moto.


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika majengo manispaa ya Kahama, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda, amesema hatua hiyo ni sehemu ya mpango mpana wa serikali kutatua changamoto za miundombinu ya barabara katika kata 18 za Manispaa ya Kahama, huku akiongeza kuwa serikali pia imejipanga kuweka tuta katika eneo la Shunu, ambalo limekuwa likigharimu maisha ya wananchi kutokana na ukosefu wa alama za barabarani.


Hata hivyo, baadhi ya wananchi wameeleza kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa barabara hizo ambapo Hidaya Melkiory, mkazi wa Kahama, alihoji juu ya kusuasua kwa mradi huo, akieleza hofu kuwa mvua zinakaribia kuanza mwezi Septemba barabara na mitaro iliyopo inaweza kuharibika zaidi.


“Mvua zikianza je barabara zitakuwa zimekamilika? Wanaenda polepole sana, hii italeta kero zaidi ya mwanzo,” amesema.


Dc Nkinda amesema Serikali imejizatiti kukamilisha ujenzi wa barabara za mjini Kahama kwa kiwango cha lami zenye urefu wa kilometer 12 kifikia Novemba 2025 licha ya kuwepo kwa changamoto za kiutekelezaji katika mradi huo mkandarasi ameahidi kukamilisha mradi



“Mheshimiwa Rais ametuletea fedha mwaka wa fedha uliopita na tukafuata taratibu za kumpata mkandarasi, Ni kweli kulikuwa na malalamiko kuwa ujenzi unasuasua, lakini tumekutana na mkandarasi na ametuhakikishia kufikia Novemba barabara zitakuwa zimekamilika,” amesema Nkinda.


Kwa upande wake, Aman Omary ameeleza kero za barabara zinazopitika kwa shida wakati wa mvua katika maeneo ya shule za Nyashimbi, Mama Samia na Majengo, akisema mitaro inayoendelea kujengwa tayari imeanza kukatika kabla ya mradi kukamilika.


Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilayani Kahama, Mhandisi Joseph Mkwizu, amesema marekebisho yanaendelea kulingana na bajeti za kila mwaka na kueleza kuwa maandalizi ya kazi ya lami yameshaanza.



“Ni matarajio yetu kuwa mitaro yote itajengwa kwa viwango vinavyohitajika na tutaingia kwenye hatua ya lami, Mitambo ya lami tayari imefungwa na kokoto zimeanza kuzalishwa,” amesema Mkwizu.



vlcsnap-2025-09-01-15h30m39s502.png
vlcsnap-2025-09-01-15h30m53s209.png
vlcsnap-2025-09-01-15h31m28s756.png

vlcsnap-2025-09-01-15h32m55s271.png
vlcsnap-2025-09-01-15h35m36s137.png
vlcsnap-2025-09-01-15h36m10s249.png
vlcsnap-2025-09-01-15h37m43s594.png
vlcsnap-2025-09-01-15h38m46s074.png
vlcsnap-2025-09-01-15h39m10s571.png
vlcsnap-2025-09-01-15h40m11s899.png
vlcsnap-2025-09-01-15h41m30s297.png
vlcsnap-2025-09-01-15h42m30s405.png
vlcsnap-2025-09-01-15h43m21s896.png
vlcsnap-2025-09-01-15h43m40s409.png
vlcsnap-2025-09-01-15h52m27s767.png
vlcsnap-2025-09-01-15h53m57s795.png


MTHIBITI UBORA WA SHULE AWATAKA WAZAZI KUFUATILIA MAENDELEO YA WATOTO SHULENI


IMG_3162.JPG


Na Neema Nkumbi - Huheso Digital Kahama

Mthibiti Ubora wa Shule wilayani Kahama Athuman Abeid amewataka wazazi kutotupilia mbali jukumu lao la kufuatilia maendeleo ya kielimu na malezi ya watoto, akisisitiza kuwa dunia ya sasa inakabiliwa na changamoto kubwa za maadili.

Akizungumza kwenye mahafali ya darasa la saba katika shule ya Greenstar, Mthibiti huyo alisema kuwa wazazi wengi wamekuwa na shughuli nyingi kiasi cha kutojua mustakabali wa watoto wao shuleni.


“Dunia imechafuka sana kimaadili. Ukimkabidhi mtoto shule kuanzia awali hadi anahitimu darasa la saba, ni miaka zaidi ya nane. Kama hukufuatilia maendeleo yake, na iwapo walimu waliteleza, kazi ya kurekebisha itabaki kwako mzazi. Hivyo nawasihi tusijisahau, tushirikiane na walimu kwa manufaa ya baadaye ya watoto wetu,” alisema.

Kwa upande mwingine, aliwataka wahitimu wa darasa la saba kutambua kuwa safari ya elimu ndio kwanza inaanza. Alisisitiza kuwa licha ya sherehe za mahafali, wajibu mkubwa wa mtihani unaowakabili unapaswa kupewa kipaumbele.

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa shule za Greenstar Daniel alitangaza kuwa taasisi hiyo kwa sasa inamiliki shule mbili za sekondari – ya wavulana na ya wasichana. Alitoa ombi kwa ofisi husika kubadilisha jina la shule ya sekondari ya Sister Irene na kuifanya Greenstar Boys, akieleza kuwa mchakato huo unapaswa kukamilika kabla ya Januari.


“Naomba wazazi muwe mstari wa mbele kuhakikisha watoto wenu wanarudi kuendelea na masomo yao hapa. Tunataka jina jipya lifahamike mapema,” alisema Mkurugenzi.

Aidha, mmoja wa wazazi waliohudhuria alitoa shukrani kwa walimu kwa kusimamia vyema taaluma na malezi ya watoto wao.


“Tunawashukuru walimu kwa juhudi kubwa za kuwalea na kuwafundisha watoto wetu. Tumewaona watoto wetu wakibadilika na kukua kielimu na kimaadili,” amesema.
IMG_3376.JPG
IMG_3162.JPG
IMG_3173.JPG
IMG_3200.JPG
IMG_3206.JPG
IMG_3221.JPG
IMG_3256.JPG
IMG_3285.JPG
IMG_3310.JPG
IMG_3315.JPG
IMG_3364.JPG
IMG_3205.JPG