Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

DKT. BITEKO AHIMIZA UTEKELEZAJI WA MAAZIMIO VIKAO VYA KIMKAKATI VYA WENYEVITI WA BODI NA WAKUU WA TAASISI

1000752480.jpg
1000752479.jpg
1000752478.jpg
1000752481.jpg
1000752484.jpg
1000752485.jpg

📌 Awakumbusha kuhusu dhamana waliyobeba ya kubadili maisha ya watanzania kupitia mtaji wa shilingi Trilioni 86 waliopewa


📌 Afunga Kikao kazi cha Tatu cha Wenyeviti wa Bodi, Wakuu wa Taasisi


📌 Asema Rais, Dkt. Samia anatambua mchango wa Taasisi za umma; ana matarajio makubwa kutoka kwao


📌 Awakumbusha kutekeleza Maagizo yaliyotolewa na Makamu wa Rais


📌 Kikao kazi chafanyika kwa mafanikio; chahusisha washiriki zaidi ya 600


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewahimiza Wenyeviti na Wakuu wa Taasisi za Umma nchini kusimamia utekelezaji wa maazimio ya kimkakati yanayofikiwa katika vikao kazi wanavyofanya kwa kutambua kuwa wamebeba dhamana ya kuboresha maisha ya Watanzania kupitia mtaji wa shilingi Trilioni 86 ambao Serikali imewekeza kwenye Taasisi na mashirika yake..


Dkt. Biteko ameyasema hayo tarehe 26 Agosti 2025 jijini Arusha wakati akifunga kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma (CEOs FORUM 2025).


“Watanzania wanawategemea ninyi kuwabadilishia maisha, kama tunazungumza kuhusu umaskini wa watu, Serikali inapaswa kuwa kiongozi wa kuwaondolea watu umaskini wao, hivyo hamna budi kutambua kuwa mnalo deni la kuboresha hali zetu na maisha yetu.” Amesema Dkt. Biteko


Dkt. Biteko amewahakikishia Watendaji hao kuwa Serikali katika ngazi zote inatambua mchango wa taasisi na mashirika katika ukuaji wa uchumi na pia inatambua mchango wa vikao kazi vya watendaji hao ambavyo vimepelekea mashirika kuongeza mchango wake katika mfuko mkuu wa Taifa.


" Vikao kazi hivi mnavyofanya vimeonesha mchango wake katika uchumi, mfano katika kikao kazi cha mwaka 2024 mliazimia mashirika ya umma yaboreshe utendaji na kuongeza uchangiaji katika mfuko mkuu wa Serikali na matokeo yameonekana mfano Shirika la Maendeleo ya Petroli ( TPDC) liliongeza uchangiaji wake kwa asilimia 100, shirika hili liliongeza uchangiaji wake kutoka shilingi bilioni 5.5 kwa mwaka 2023/2024 hadi shilingi bilioni 11.1 mwaka 2024/2025." Amesema Dkt.Biteko


Ameongeza kuwa, uchagiaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) umeongezeka kwa asilimia 363 katika mfuko mkuu wa Serikali ambapo NHC ilichangia shilingi bilioni 1.2 mwaka 2023/ 24 na mwaka 2024/2025 ilichangia shilingi bilioni 5.5.


Dkt. Biteko amewaeleza Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi kuwa “Rais Samia pamoja na kuthamini mchango wenu kwa Serikali anatarajia mengi kutoka kwenu na Watanzania wana matarajio makubwa hasa wakati tukielekea kwenye utekelezaji wa Dira 2050, endeleeni kuongeza mchango wenu kwenye ukuaji wa uchumi, mjitegemee na muwe mfano wa taasisi binafsi."


Katika.hatua nyingine, Dkt. Biteko ametaka viongozi hao kufanyia kazi agizo lililotolewa na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango la kudhibiti mianya ya uvujaji wa mapato.


Pia amempongeza Msajili wa Hazina kwa kuwa na maono ya kuratibu kikao kazi hicho ili kujadili masuala yatakayosukuma mbele utendaji wa taasisi.


Katika hafla hiyo, Dkt. Biteko hakuacha kukumbusha kuhusu ushiriki wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ambapo amesema uchaguzi huo uwe ni ajenda ya watu wote wakiwemo Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi hivyo waone kuwa wana wajibu wa kuwasisitiza watu kwenye taasisi zao kujitokeza kusikiliza wagombea na baadaye kupiga kura kwa amani kwani kukiwa na amani mashirika hayo pia yatafanya vizuri zaidi.


Naibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Mhe. Stanslaus Nyongo kwa upande wake, amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dira na muongozo katika kuendeleza mashirika ya umma ili yaweze kuwa na tija nchini.


Amesema katika siku tatu za kikao kazi washiriki wamejifunza na kubadilishana uzoefu kupitia watoa mada wa ndani na nje ya nchi waliobobea.


Amesema Wizara ya Mipango na Uwekezaji itahakikisha maazimio ya kikao kazi hicho yanatekelezwa ipasavyo, pia Wizara itasimamia mageuzi ya kuhakikisha mashirika ya umma yanachangia ukuaji wa pato la taifa hadi kufikia Dola za Marekani trilioni 1 ifikapo 2050 ambapo kwa sasa pato la taifa ni dola za Marekani bilioni 85.


Kwa upande wake Salim Kali, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema wilaya 6 za Mkoa wa Arusha zimefikiwa na umeme hadi ngazi ya vijiji, pia miradi ya maji imefanyika pamoja na miundombinu ya Barabara ambayo imewezesha maisha bora kwa watu wa aina zote wakiwemo watalii.


Awali, Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu alisema kuwa katika kikao kazi hicho kampuni zaidi 300 zimeshiriki huku washiriki wakiwa ni zaidi ya 650.


Alisema kikao kilikuwa na majadiliano mbalimbali ya kina yanayolenga kusukuma mbele uchumi wa nchi na kusimamia uwekezaji wa Serikali kwa taasisi za umma wa zaidi ya shilingi trilioni 86.


Mkutano huo wa Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma uliongozwa na kaulimbiu ya "Ushirikiano Endelevu wa Kibiashara katika Mazingira Shindani Kimataifa - Nafasi ya Mashirika ya Umma."


Mwisho

AHADI YA SERIKALI KUFIKISHA UMEME WA GRIDI KAGERA YATEKELEZWA

1000749074.jpg
1000749075.jpg
1000749076.jpg
1000749077.jpg
1000749078.jpg
1000749079.jpg
1000749080.jpg
1000749081.jpg
1000749082.jpg
1000749083.jpg



📌 Dkt.Biteko ashuhudia utiaji saini mikataba itakayowezesha Wilaya zote Kagera kupata umeme wa Gridi


📌 Awali umeme mwingi ulikuwa ukitoka nchini Uganda hivyo kufanya Mkoa kutokuwa na umeme wa uhakika na wa kutosha


📌 Asema Rais.Dkt. Samia alishatoa maagizo ya mradi huo kutekelezwa kwa wakati na kwa usahihi


📌 Aagiza wananchi 1,014 waliopisha mradi kulipwa fidia kuanzia mwezi Septemba 2025



📌 Apongeza Wizara ya Nishati na TANESCO kwa ufanisi katika.usimamizi wa miradi



Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati




Ahadi ya Serikali ya kufikisha umeme wa gridi ya taifa katika Wilaya zote za Mkoa wa Kagera imetekelezwa baada ya Serikali kusaini mikataba ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Benako, Ngara hadi Kyaka wilayani Misenyi na kituo cha kupoza umeme cha Benako cha msongo wa kilovoti 220/33, hatua inayotoa uhakika kwa Mkoa huo sasa kupata umeme wa gridi badala ya kutegemea umeme kutoka Uganda kwa kiasi kikubwa.


Akizungumza baada ya kushuhudia utiaji saini kwa mikataba hiyo jijini Dodoma tarehe 25 Agosti, 2025, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa kuanza kutekelezwa kwa mradi huo ni moja ya maelekezo ya Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa na kiu ya kutekeleza ahadi ya Serikali kwa wananchi wa Kagera ya kupata umeme wa uhakika muda wote ili kutekeleza shughuli zao za kiuchumi na kijamii.


" Kupitia mradi huu, Mkoa wa Kagera kwa mara ya kwanza na wenyewe unaingia kwenye gridi ya Taifa hasa na hivyo kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme hususan katika Wilaya za Bukoba, Muleba, Misenyi, Karagwe, Kyerwa na maeneo mengine ya jirani, nawahakikishia watu wa Kagera kuwa Serikali imeshaamua mradi huu ufanyike kwa wakati kwa miezi 24 tu" Amesema Dkt. Biteko


Dkt. Biteko amesema, Kagera ambayo mahitaji yake ya umeme hayazidi megawati 47 baada ya muda itakuwa na uhakika mkubwa wa upatikanaji umeme kwani kutakuwa na njia mbalimbali za kufikisha umeme mkoani humo ikiwemo Benako- Karagwe hadi Kayaka, Nyakanazi- Biharamulo hadi Muleba na kuna mradi mwingine mkubwa unaotarajiwa kujengwa kutoka Ibadakuli hadi Mbarara Uganda wa kV 400. Vilevile kuna mradi wa uzalishaji umeme wa Kakono wa megawati 87 ambao upo katika hatua za mwisho za kutafuta Mkandarasi.


Ameongeza kuwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan pia anaendelea kutekeleza miradi mingine ya umeme katika maeneo mengine ikiwemo mradi wa usafirishaji umeme wa kV 400 wa Tanzania- Zambia, mradi wa Usafirishaji umeme wa kV 400 Chalinze-Dodoma , mradi wa usafirishaji umeme wa Mkuranga -Pwani ambao utapeleka umeme kwa wananchi wa Kusini, pia mradi wa usafirishaji umeme wa gridi imara wa Tunduru- Masasi- Mahumbika ambao pia unaenda kutoa uhakika wa umeme katika mikoa ya Kusini.


" Utekelezaji wa miradi hii yote ya umeme ni kielelezo kuwa, Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshaonesha njia ya kuwafikishia wananchi umeme wa uhakika sasa kinachohitajika kwa watendaji ni kukimbia badala ya kutembea kwani kinachotakiwa ni matokeo na siyo kusema sana." Amesisitiza Dkt. Biteko


Pia Dkt. Biteko amewashukuru wafadhili wa mradi ambao wametoa Dola za Kimarekani takriban milioni 105.6 ambazo ameagiza kuwa zitumike kwa usahihi ili kuwapa sababu wafadhili wengine kuendelea kusaidia miradi mbalimbali.


Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko ameagiza TANESCO kuhakikisha wananchi 1,014 wanaopisha mradi wanalipwa fidia yao mapema iwezekanavyo yaani kuanzia mwezi septemba mwaka huu.


Aidha, amempongeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga na watendaji wa TANESCO kwa kuendelea kusimamia kwa umakini Sekta ya Nishati.


Vilevile, ameipongeza TANESCO kwa kuendelea kuboresha utendaji wake na kwa kusimamia haki hasa pale zabuni zinapotangazwa. Aidha ametaka mipango iliyowekwa kwenye mradi huo iheshimiwe ili thamani ya fedha ionekane na wananchi wapate huduma kwa wakati.


Dkt. Biteko ameomba wananchi mkoani Kagera kuchangamkia fursa kutokana na kuwepo kwa umeme wa uhakika mara baada ya miradi itakayofikisha umeme mkoani humo kukamilika.


Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fatuma Mwassa amepongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kutekekeza mradi huo wenye gharama kubwa ikiwa ni kuonesha kwa vitendo jinsi inavyowajali wananchi hao.


Amesema wilaya zote mkoani Kagera zitaunganishwa na gridi kwani kwa sasa no wilaya tatu tu ndio zimeunganishwa na Gridi ya Taifa.


Ameahidi kuwa, Wananchi katika mkoa huo watakuwa watumiaji wazuri wa umeme na walipaji bili wazuri iili TANESCO iendelee kupata mapato ya kutekeleza miradi mingine l.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mikoa minne ambayo haijaunganishwa kwenye gridi ya Taifa ikiwemo Rukwa, Lindi na Mtwara.


Amesema tukio la leo ni la kihistoria kwani kukamilika kusainiwa kwa mikataba hiyo kunafanya mikoa yote iliyo nje ya gridi kuwa kwenye mpango wa kupelekewa umeme gridi hivyo kwa sasa hakuna mkoa ulio nje ya gridi ambao hauna mradi wa kupelekewa umeme.


Amesema kwa sasa Mkoa wa Kagera unapata umeme wa megawati 40 kutoka nchini Uganda kupitia kituo cha Kyaka na megawati 7 kutoka mwekezaji binafsi wa mradi wa Mirongo/ Kikagati.


Amesema wakati Serikali ya Awamu ya Sita inaingia madarakani jumla ya mikoa sita kati ya 26 haikuwa imeunganishwa kwenye gridi ya Taifa ila kwa kipindi cha minne Serikali imefanikiwa kuunganisha umeme Kigoma na Katavi huku mingine iiliyosalia ikiwa miaradi inayoendelea kutekekelezwa.


Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania ( TANZANIA), Lazaro Twange mradi huo una umuhimu mkubwa mkoani Kagera kwani wilaya za Kyerwa, Karagwe, Misenyi, Muleba, Bukoba Vijijini na Manispaa ya Bukoba kwa muda mrefu sasa zimekuwa zikiitumia umeme kutoka nchini Uganda takribani megawati 40 kupitia kituo cha kupoza umeme cha Kyaka ambacho kinapokea umeme kutoka Masaka, Uganda kupitia njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 132 kufuatia mkataba wa makubaliano baina ya Tanzania na Uganda.



Pia, kukamilika kwa mradi huo kutawezesha kuunganishwa kwa kituo cha kuzalisha umeme cha Kakono katika Gridi ya Taifa.



Amesema gharama za mradi ni shilingi bilioni 262.5 na utatekelezwa kwa muda wa miezi 24.


Amesema.Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ambapo Mfuko wa Maendeleo wa Shirika la Wauzaji Mafuta Duniani (OPEC) utachangia dola za Marekani milioni 60, Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi utachangia dola za Marekani milioni 30, Mfuko wa Maendeleo wa Saudia utachangia dola za Marekani milioni 13 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itachangia dola za Marekani milioni 2.6 kwa ajili ya fidia kwa wananchi watakaopisha mradi.


Amesema Wakandarasi watakaotekeleza mradi huo ni kampuni ya M/s. TBEA Co. Ltd kutoka nchini China ambayo itahusika na ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Benako, na Kampuni ya M/s. Transrail Lighting Limited kutoka India itahusika na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Benako hadi Kyaka.

TANZANIA KUWA KINARA WA UTOAJI WA HUDUMA ZA KIMAABARA AFRIKA MASHARIKI NA KATI



▪️Waziri Mavunde aweka jiwe la Msingi wa Ujenzi wa Maabara ya kisasa


▪️Ni maabara kubwa ya uchunguzi wa sampuli za madini Afrika Mashariki


▪️Kugharimu Tsh Bilioni 14.3


▪️Rais Samia atajwa kinara wa mageuzi sekta ya madini



📍 Kizota, Dodoma


Tanzania imeanza ujenzi wa maabara kubwa na ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini ambayo itakuwa ni kubwa kuliko zote kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati na ambayo itatoa huduma ya kimaabara kwa ubora na kwa uharaka kwa wadau wa sekta ya madini nchini.


Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa maabara ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini katika eneo la Kizota,Jijini Dodoma.


“Tunamshukuru Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa kuwa kinara wa mageuzi makubwa ya sekta ya madini na kwa kuandika historia ya ujenzi wa maabara hii ya kisasa miaka 100 baadaye tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa madini(GST) mwaka 1925.


Leo tunaandika historia kuanza kwa ujenzi wa maabara kubwa ambayo itafungwa mitambo na vifaa vya kisasa katika kutoa huduma za kimaabara ndani na nje ya nchi.


Huu ni ukombozi mkubwa kwa wadau wa sekta ya madini katika kupata taarifa sahihi za kimaabara kwa wakati na zenye ubora wa hali ya juu.


Ni imani yangu maabara hii itachochea ukuaji na maendeleo ya sekta ya madini”Alisema Mavunde


Naye Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini(*GST*) Dkt. Notka Huruma Batenze amesema Maabara hiyo ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini utaleta tija kwa wadau wa sekta ya madini na kurahisisha upatikanaji wa huduma hii muhimu kwa maendeleo ya sekta ya madini.


Gharama za ujenzi wa maabara hii unatarajiwa kuwa Tsh Bilioni 14.3 na muda wa ujenzi wa kukamilika maabara ni siku 690.

CHEREHANI EMMANUEL ACHUKUA FOMU YA UTEUZI KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA USHETU KUPITIA CCM



1000746074.jpg
1000746075.jpg
1000746076.jpg
1000746077.jpg
1000746078.jpg

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ushetu, Wilaya ya Kahama, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Cherehani Emmanuel , leo Agosti 24, 2025, amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.


Cherehani ambaye aliteuliwa na Kamati Kuu ya CCM Taifa kupeperusha bendera ya chama hicho amepokelewa na kukabidhiwa fomu hiyo na Afisa Uchaguzi katika Jimbo hilo Charles Mburu.


Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu, Cherehani amekishukuru Chama chake na wananchi kwa imani waliompa huku akisisitiza mshikamano ndani ya chama na kuondoa makundi ya makambi ili kujenga Ushetu yenye mshikamano na maendeleo kwa manufaa ya wananchi wote.

DC NKINDA AAGIZA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU MWIME WAREJESHEWE FEDHA ZAO

 .

1000745588.heic

DC Nkinda asisitiza makubaliano badala ya kutumia nguvu kwa makato ya wachimbaji
Aagiza wachimbaji wa Mwine warejeshewe zaidi ya milioni 7 walizokatwa kwa ajili ya ulinzi.
Aonya kuwa vitendo hivyo vinapunguza imani kwa serikali.
Ahimiza mazungumzo ya hiari kujenga mahusiano bora kazini.


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Frank Nkinda, ametoa agizo kwa kampuni zinazojihusisha na uchimbaji wa dhahabu wilayani humo kuhakikisha hazitumii nguvu katika kufanya makato ya fedha kwa wachimbaji wadogo. Badala yake, amesisitiza umuhimu wa maelewano na elimu baina ya pande zote ili kuondoa malalamiko.

Akizungumza katika eneo la Mwine wakati wa kikao cha kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji wadogo, Mhe. Nkinda ameagiza zaidi ya shilingi milioni saba (7,000,000) zilizokatwa kutoka kwenye malipo ya wachimbaji kwa ajili ya kulipia huduma za ulinzi wa mgodi, zirejeshwe kwa wachimbaji hao mara moja.

Ameeleza kuwa vitendo kama hivyo vinavunja imani ya wananchi kwa serikali, na kusisitiza umuhimu wa kuweka misingi ya maelewano nje ya mifumo rasmi ya kiserikali, ili kuimarisha uhusiano kazini na kuzuia migogoro kati ya waajiri na waajiriwa.

Mkuu huyo wa wilaya ameonyesha nia ya dhati ya kulinda maslahi ya wachimbaji wadogo na kuendeleza sekta ya madini kwa haki na usawa.



1000745587.heic
1000745585.heic
1000745584.heic
1000745586.heic

BENJAMIN LUKUBHA NGAYIWA AKABIDHIWA FOMU YA UTEUZI KUGOMBEA UBUNGE KAHAMA MJINI KUPITIA CCM

 1000746618.webp


Bw. Benjamin Lukubha Ngayiwa (Kushoto) mapema leo amekabidhiwa rasmi Fomu ya Uteuzi kugombea kiti cha Ubunge Jimbo la Kahama Mjini na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo Bw. Sadick Kigaile kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

1000746620.webp
1000746619.webp
1000746619.webp


MKUTANO WA SABA WA KIMATAIFA SEKTA YA MADINI KUFANYIKA NOVEMBA, 2026

 1000745173.jpg

1000745121.jpg


*Yaelezwa Sababu ni kupisha maandalizi ya Maandalizi ya Uchaguzi Mkuu*


*Dodoma*


Wizara ya Madini imetangaza kusogeza mbele Mkutano wa Saba (7) wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliokuwa ufanyike mwezi Novemba 2025 na badala yake mkutano huo utafanyika tarehe 19 hadi 21 Novemba 2026, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar EsSalaam.


Taarifa iliyotelewa na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Eng. Yahya Samamba imeleza sababu za kusogezwa kwa mkutano huo kuwa ni kupisha maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa nchini uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba, 2025.


‘’Wizara ya Madini inaomba radhi kwa wadau wote wa ndani na nje ya nchi waliokuwa wanatarajia kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini ambao ulipangwa kufanyika Novemba 2025,’’ imeeleza taarifa hiyo.


Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini nchini unaofanyika kila mwaka tangu 2019 ukibebwa na kaulimbiu mbalimbali, hutumika kama jukwaa la kujadili kwa pamoja mstakabali wa Sekta ya Madini, kubadilishana ujuzi, maarifa na uzoefu pamoja na kuangazia fursa mpya zinazojitokeza katika Sekta ya Madini nchini.


Vilevile, mkutano huo hutumika kuimarisha mazingiraya uwekezaji, kuendelea kuvutia uwekezaji mpya kutoka ndani na nje ya nchi, wadau kupata fursa ya kujifunza Sera, Sheria na mikakati mipya ya Serikali na kujadili kwa pamoja masuala ya kisheria na uchumi yanayohusiana na Sekta ya Madini.


Mbali na hayo, kupitia hafla ya Usiku wa Madini ambayo huambatana na mkutano huo, hutumika kutoa tuzo kwa wadau waliofanya vizuri katika Sekta ya Madini kupitia vipengele mbalimbali ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wao kwa Sekta ya Madini nchini.


Aidha, mkutano huo huyakutanisha makundi mbalimbali wakiwemo mawaziri wa madini kutoka nchi nyingine za Afrika, watendaji wakuu wa kampuni kubwa za madini duniani waliowekeza nchini, watafiti, mabalozi wanao ziwakilisha nchi zao hapa chini na nje ya tanzania, mashirika ya kimataifa.


Makundi mengine ambayo hushiriki mkutano huo ni pamoja na wachimbaji, wafanyabiashara wa madini, taasisi za fedha, vyuo vikuu na vya kati, taasisi za umma, taasisi binafsi zinazojishughulisha na madini, viongozi mbalimbali kutoka wizara, taasisi za umma, mikoa na halmashauri ambazo shughuli za madini zinafanyika.



#Vision 2030:


*Madini ni Maisha na Utajiri*

HAYA HAPA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE CCM UCHAGUZI MKUU 2025 MKOA SHINYANGA

 




Mkoa wa Shinyanga :


Patribas Katambi- Shinyanga Mjini


Benjamin Lukubha Ngayiwa -Kahama Mjini


Mabula J. Magangila - Msalala


Ahmed Salum - Solwa


Azza Hillal Hamad - Itwangi


Emmanuel Cherehani - Ushetu


Lucy Mayenga - Kishapu