Log in
The Foundation for Human Health Society.

The Foundation for Human Health Society.

KAHAMA, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

MBIO ZA KUKINADI CHAMA CHA MAPINDUZI MKOANI GEITA ZAANZA KWA KISHINDO

1000772438.jpg
1000772440.jpg
1000772439.jpg
1000772441.jpg
1000772442.jpg



📌 Majimbo 7 kati ya 9 yapita bila kupingwa


📌 Kata 92 kati ya 122 zapita bila kupingwa


📌 Maelfu wakusanyika kusikiliza Ilani ya CCM 2025-2030


📌 Dkt. Biteko awasisitiza wananchi kujitokeza kwa wingi kumpigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan


📌 Asisitiza mshikamano kabla na baada ya uchaguzi


Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Geita leo Septemba 2, 2025 kimezindua kwa kishindo kampeni za kuinadi Ilani ya CCM 2025-2030 kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ambapo imeelezwa kuwa mpaka sasa tayari Majimbo 7 kati ya 9 ya Ubunge yamepita bila kupingwa huku kata 92 kati ya 122 zikipita bila kupingwa.


Mgeni rasmi katika uzinduzi huo uliofanyika katika Kata ya Uyovu Wilaya ya Bukombe, Mkoani Geita ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa huo, Nicholaus Kasendamila amesema Chama cha Mapinduzi kinaingia kwenye kampeni kikiwa na mtaji mkubwa wa uadilifu, uaminifu, uchapakazi na busara ya mgombea Urais wa kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Amesema kupitia kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, CCM inazo sababu za kuomba ridhaa ya wananchi kuendelea kuongoza nchi akisema kuwa amefanya maendeleo mengi ikiwemo uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam ambayo ni lango kubwa la biashara kwaTanzania na nchi jirani, amejenga daraja refu la Busisi, amekamilisha ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere (MW 2,115) na reli ya kisasa imeshaanza kufanya kazi.


Kasendamila amesema kuwa katika Mkoa wa Geita, Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020-2025 imetekelezwa kwa mafanikio ambapo ameeleza kuwa shule mpya za msingi 151 zimejengwa, Shule za sekondari mpya 118 zimejengwa, zimejengwa hospitali mbili za rufaa, hospitali za wilaya mpya 4 na vituo vya afya 17 vipya vimejengwa.


Ameongeza kuwa, kupitia Ilani ya CCM 2020-2025, zahanati 69 zimejengwa, leseni za madini 7600 zimetolewa kwa wachimbaji wadogo na kuhusu umeme, kabla ya kuingia kwa Serikali ya Awamu ya Sita kulikuwa na vijiji 362 tu vyenye umeme lakini sasa vijiji vyote 486 mkoani Geita vina umeme.


Kuhusu miundombinu ya Barabara amesema Barabara za lami na changarawe zimeendelea kujengwa mkoani Geita ili kurahisisha usafiri wa wananchi.


Ametaja vipaumbele vya CCM katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuwa ni pamoja na kuongeza fursa za wananchi kujiimarisha kiuchumi, kuendeleza sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, madini, umeme n.k


Mwenyekiti huyo wa CCM, ameomba wananchi waipigie kura CCM kwani kura zao zitafanyiwa kazi kupitia maendeleo.


Akizungumza kwa niaba ya Wagombea nafasi ya Ubunge mkoani Geita, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambaye ni Mbunge Mteule wa Jimbo la Bukombe, amewashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi wa kampeni akieleza kuwa ni ishara ya Wananchi kukipenda Chama cha Mapinduzi na kuridhika na kazi zinazofanywa na Dkt. Samia suluhu Hassan.


Amesema uchaguzi wa mwaka huu utapeleka salaam ndani ya nchi na kimataifa kuhusu uwepo wa demokrasia nchini hivyo amewaasa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura akiahidi kuwa maendeleo wanayoyaona sasa ni rasharasha tu kwani maendeleo makubwa zaidi yanakuja.


Amesema Mkoa wa Geita unazidi kukua ambapo kwa sasa umekuwa ni moja ya mikoa mitano yenye uchumi mkubwa nchini ni mkoa namba moja kwa kuzalisha dhahabu, umekuwa ni mkoa kiungo kwa maeneo mengine nchini na watu wake ni wachapakazi hivyo watampigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kupata maendeleo zaidi.


Kuelekea uchaguzi Mkuu 2025, Dkt. Bitelo amesisitiza kuwa uchaguzi huo uunganishe wananchi badala ya kutenganisha, kuwe na kampeni za kistaarab na Chama cha Mapinduzi kuendelea kufanya kazi kwa umoja.


"Uchaguzi huu ni kwa ajili ya maendeleo yetu, tunataka barabara bora, umeme, afya, mitaji ya biashara, tusiuchukulie poa uchaguzi huu kwani maana kubwa kwenye maisha yetu," Amesisitiza Dkt.Biteko


Akizungumzia maendeleo mbalimbali yaliyofanywa katika Jimbo la Bukombe, Dkt. Biteko amesema, chini ya uongozi wa Dkt.Samia Suluhu Hassan Bukombe sasa kunajengwa Chuo cha VETA ambacho kitawezesha vijana kupata ujuzi wa aina mbalimbali pia Chuo cha Uhasibu Arusha kimeanzisha tawi wilayani Bukombe.


Ameongeza kuwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan amezigusa sekta zote kimaendeleo akitolea mfano Shule za msingi sasa zimefikia 104, shule za sekondari zimefikia 25 na shule za sekondari kidato cha tano na sita zimefikia 5 huku umeme ukifika kwenye vijiji vyote.


Ameongeza kuwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewezesha ujenzi wa kituo kikubwa cha kuzalisha umeme wa jua wa megawati 5 wilayani Bukombe, kikiwa ni cha pili kwa ukubwa ukiacha kituo cha namna hiyo kilichopo Kigoma pia anajenga barabara ya lami kutoka Ushirombo hadi Katoro.


Katika hatua nyingine Dkt. Biteko amewaasa wananchi kujitokeza kwa wingi kumpokea mgombea mwenza wa Kiti cha Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye anatarajiwa kuanza ziara mkoani Geita tarehe 5 Septemba 2025.


Awali, Katibu wa CCM Mkoa wa Geita, Alexandarina Katabi amesema Mkoa wa Geita una mtaji wa wapiga kura waliojiandikisha takriban 1,532,408 huku Wanaccm waliojiandikisha wakiwa ni 524,000 ikiwa ni mtaji wa nusu ya wananchi waliojiandikisha.


Amesema katika Mkoa wa Geita, Majimbo yanayogombewa ni 9 na kata ni 122.


Ameongeza kuwa katika Majimbo hayo 9 majimbo 7 tayari yamepita bila kupingwa na katika kata 122 tayari kata 92 zimepita bila kupingwa na zilizobaki ndizo zenye wapinzani.


Mwisho.

MGOGORO WA MIPAKA YA CHUO CHA MAENDELEO MWAMVA WAPATIWA UFUMBUZI

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif









Na Neema Nkumbi

Mgogoro wa muda mrefu kuhusu mipaka ya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mwamva kilichopo Manispaa ya Kahama, sasa umepatiwa ufumbuzi.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Deogratius Ndejembi, amewataka wananchi waliokuwa wamesahaulika katika takwimu alizopewa hayati Dkt. John Magufuli kuwa eneo la ekari 40 ndilo litakalobaki katika mipaka ya chuo hicho, waendelee na shughuli zao za ujenzi na maendeleo kwenye maeneo yao, huku akisisitiza kuwa wale waliovamia eneo hilo baada ya kauli ya hayati Magufuli, sheria itachukua mkondo wake.

Akizungumza kwa njia ya simu kupitia Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, Waziri Ndejembi amesema atatuma timu ya wataalamu kuja kuhakiki ili kila mwenye haki apate haki yake.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa Mhita amewataka wananchi kuwa na amani kwani changamoto hiyo sasa imepata mwarobaini, na akawahakikishia kuwa wako huru kuendeleza maeneo yao.

Wananchi waliozungumza mara baada ya maelekezo ya waziri wametoa shukurani na pongezi zao kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Mmoja wa wananchi, Paul Andrea, amesema: "Tunamshukuru sana Rais Samia, zamani tulikuwa tunaitwa matapeli, sasa tuko huru."

Aidha, mstaafu wa Jeshi la Magereza, Mzee Gregory Kachemba, ameonyesha furaha yake kwa hatua hiyo, akisema alimaliza mafao yake ya kustaafu kwa kujenga nyumba na kuanzisha maendeleo katika eneo hilo, hivyo kupata suluhisho la mgogoro huo ni faraja kubwa kwake.




transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif

transparent.gif


SERIKALI YAAHIDI TAA ZA BARABARANI KUPUNGUZA AJALI KAHAMA

vlcsnap-2025-09-01-15h32m30s076.png


Na Neema Nkumbi - Huheso Digital Kahama


Serikali wilayani Kahama kupitia Jeshi la Polisi imejipanga kusimika taa za kuongozea magari katika maeneo ya Lumambo, Bijampora na Phantom, ili kupunguza msongamano na ajali zinazochangiwa na ukosefu wa mwongozo rasmi wa vyombo vya moto.


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika majengo manispaa ya Kahama, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda, amesema hatua hiyo ni sehemu ya mpango mpana wa serikali kutatua changamoto za miundombinu ya barabara katika kata 18 za Manispaa ya Kahama, huku akiongeza kuwa serikali pia imejipanga kuweka tuta katika eneo la Shunu, ambalo limekuwa likigharimu maisha ya wananchi kutokana na ukosefu wa alama za barabarani.


Hata hivyo, baadhi ya wananchi wameeleza kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa barabara hizo ambapo Hidaya Melkiory, mkazi wa Kahama, alihoji juu ya kusuasua kwa mradi huo, akieleza hofu kuwa mvua zinakaribia kuanza mwezi Septemba barabara na mitaro iliyopo inaweza kuharibika zaidi.


“Mvua zikianza je barabara zitakuwa zimekamilika? Wanaenda polepole sana, hii italeta kero zaidi ya mwanzo,” amesema.


Dc Nkinda amesema Serikali imejizatiti kukamilisha ujenzi wa barabara za mjini Kahama kwa kiwango cha lami zenye urefu wa kilometer 12 kifikia Novemba 2025 licha ya kuwepo kwa changamoto za kiutekelezaji katika mradi huo mkandarasi ameahidi kukamilisha mradi



“Mheshimiwa Rais ametuletea fedha mwaka wa fedha uliopita na tukafuata taratibu za kumpata mkandarasi, Ni kweli kulikuwa na malalamiko kuwa ujenzi unasuasua, lakini tumekutana na mkandarasi na ametuhakikishia kufikia Novemba barabara zitakuwa zimekamilika,” amesema Nkinda.


Kwa upande wake, Aman Omary ameeleza kero za barabara zinazopitika kwa shida wakati wa mvua katika maeneo ya shule za Nyashimbi, Mama Samia na Majengo, akisema mitaro inayoendelea kujengwa tayari imeanza kukatika kabla ya mradi kukamilika.


Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilayani Kahama, Mhandisi Joseph Mkwizu, amesema marekebisho yanaendelea kulingana na bajeti za kila mwaka na kueleza kuwa maandalizi ya kazi ya lami yameshaanza.



“Ni matarajio yetu kuwa mitaro yote itajengwa kwa viwango vinavyohitajika na tutaingia kwenye hatua ya lami, Mitambo ya lami tayari imefungwa na kokoto zimeanza kuzalishwa,” amesema Mkwizu.



vlcsnap-2025-09-01-15h30m39s502.png
vlcsnap-2025-09-01-15h30m53s209.png
vlcsnap-2025-09-01-15h31m28s756.png

vlcsnap-2025-09-01-15h32m55s271.png
vlcsnap-2025-09-01-15h35m36s137.png
vlcsnap-2025-09-01-15h36m10s249.png
vlcsnap-2025-09-01-15h37m43s594.png
vlcsnap-2025-09-01-15h38m46s074.png
vlcsnap-2025-09-01-15h39m10s571.png
vlcsnap-2025-09-01-15h40m11s899.png
vlcsnap-2025-09-01-15h41m30s297.png
vlcsnap-2025-09-01-15h42m30s405.png
vlcsnap-2025-09-01-15h43m21s896.png
vlcsnap-2025-09-01-15h43m40s409.png
vlcsnap-2025-09-01-15h52m27s767.png
vlcsnap-2025-09-01-15h53m57s795.png


MTHIBITI UBORA WA SHULE AWATAKA WAZAZI KUFUATILIA MAENDELEO YA WATOTO SHULENI


IMG_3162.JPG


Na Neema Nkumbi - Huheso Digital Kahama

Mthibiti Ubora wa Shule wilayani Kahama Athuman Abeid amewataka wazazi kutotupilia mbali jukumu lao la kufuatilia maendeleo ya kielimu na malezi ya watoto, akisisitiza kuwa dunia ya sasa inakabiliwa na changamoto kubwa za maadili.

Akizungumza kwenye mahafali ya darasa la saba katika shule ya Greenstar, Mthibiti huyo alisema kuwa wazazi wengi wamekuwa na shughuli nyingi kiasi cha kutojua mustakabali wa watoto wao shuleni.


“Dunia imechafuka sana kimaadili. Ukimkabidhi mtoto shule kuanzia awali hadi anahitimu darasa la saba, ni miaka zaidi ya nane. Kama hukufuatilia maendeleo yake, na iwapo walimu waliteleza, kazi ya kurekebisha itabaki kwako mzazi. Hivyo nawasihi tusijisahau, tushirikiane na walimu kwa manufaa ya baadaye ya watoto wetu,” alisema.

Kwa upande mwingine, aliwataka wahitimu wa darasa la saba kutambua kuwa safari ya elimu ndio kwanza inaanza. Alisisitiza kuwa licha ya sherehe za mahafali, wajibu mkubwa wa mtihani unaowakabili unapaswa kupewa kipaumbele.

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa shule za Greenstar Daniel alitangaza kuwa taasisi hiyo kwa sasa inamiliki shule mbili za sekondari – ya wavulana na ya wasichana. Alitoa ombi kwa ofisi husika kubadilisha jina la shule ya sekondari ya Sister Irene na kuifanya Greenstar Boys, akieleza kuwa mchakato huo unapaswa kukamilika kabla ya Januari.


“Naomba wazazi muwe mstari wa mbele kuhakikisha watoto wenu wanarudi kuendelea na masomo yao hapa. Tunataka jina jipya lifahamike mapema,” alisema Mkurugenzi.

Aidha, mmoja wa wazazi waliohudhuria alitoa shukrani kwa walimu kwa kusimamia vyema taaluma na malezi ya watoto wao.


“Tunawashukuru walimu kwa juhudi kubwa za kuwalea na kuwafundisha watoto wetu. Tumewaona watoto wetu wakibadilika na kukua kielimu na kimaadili,” amesema.
IMG_3376.JPG
IMG_3162.JPG
IMG_3173.JPG
IMG_3200.JPG
IMG_3206.JPG
IMG_3221.JPG
IMG_3256.JPG
IMG_3285.JPG
IMG_3310.JPG
IMG_3315.JPG
IMG_3364.JPG
IMG_3205.JPG

TUME YAKUTANA NA VYAMA KUFANYA MABADILIKO MADOGO YA RATIBA YA KAMPENI


1002271568.jpg
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ndugu. Kailima Ramadhani leo tarehe 30 Agosti, 2025 ameongoza kikao cha wawakilishi wa vyama vya siasa kupitia na kufanya mabadiliko madogo kwenye ratiba ya mikutano ya hadhara ya kampeni za wagombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais.


Mikutano hiyo iliyoanza tarehe 28 Agosti, 2025 inaendelea hadi tarehe 28 Oktoba, 2025 kwa Tanzania Bara na tarehe 27 Oktoba, 2025 kwa Tanzania Zanzibar.


Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano na Madiwani kwa Tanzania Bara utafanyika tarehe 29 Oktoba, 2025.


1002271552.jpg

1002271586.jpg

1002271560.jpg

1002271574.jpg

1002271563.jpg

1002271579.jpg

1002271594.jpg

INEC YAONDOA FOMU ZA UTEUZI ZA WAGOMBEA KITI CHA RAIS NA MAKAMU WA RAIS KATIKA UBAO WA MATANGAZO


3Z7A4754.JPGMkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima (kulia) ameongoza watumishi wa Tume kuondoa fomu za uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ubao wa matangazo wa Tume ikiwa zimepita saa 24 za kubandikwa fomu hizo ikiwa ni utekelezaji wa masharti ya sheria. Fomu hizo za wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilibandikwa ili kutoa fursa ya kuweka pingamizi dhidi ya uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais ambapo pingamizi hilo linaweza kuwekwa na mgombea mwingine, Msajili wa Vyama vya Siasa au Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Fomu hizo zilibandikwa na Tume Saa 10:00 jioni ya Agosti 27, 2025 ambayo ilikuwa ni siku ya uteuzi na kuondolewa leo Agosti 28, 2025 Saa 10: 00 jioni.
3Z7A4728.JPG


3Z7A4742.JPG



3Z7A4783.JPG

3Z7A4765.JPG

3Z7A4749.JPG

3Z7A4779.JPG

3Z7A4788.JPG