Fungua
The Foundation for Human Health Society.

The Foundation for Human Health Society.

KAHAMA, Tanzania

TUME YAKUTANA NA VYAMA KUFANYA MABADILIKO MADOGO YA RATIBA YA KAMPENI


1002271568.jpg
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ndugu. Kailima Ramadhani leo tarehe 30 Agosti, 2025 ameongoza kikao cha wawakilishi wa vyama vya siasa kupitia na kufanya mabadiliko madogo kwenye ratiba ya mikutano ya hadhara ya kampeni za wagombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais.


Mikutano hiyo iliyoanza tarehe 28 Agosti, 2025 inaendelea hadi tarehe 28 Oktoba, 2025 kwa Tanzania Bara na tarehe 27 Oktoba, 2025 kwa Tanzania Zanzibar.


Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano na Madiwani kwa Tanzania Bara utafanyika tarehe 29 Oktoba, 2025.


1002271552.jpg

1002271586.jpg

1002271560.jpg

1002271574.jpg

1002271563.jpg

1002271579.jpg

1002271594.jpg

INEC YAONDOA FOMU ZA UTEUZI ZA WAGOMBEA KITI CHA RAIS NA MAKAMU WA RAIS KATIKA UBAO WA MATANGAZO


3Z7A4754.JPGMkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima (kulia) ameongoza watumishi wa Tume kuondoa fomu za uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ubao wa matangazo wa Tume ikiwa zimepita saa 24 za kubandikwa fomu hizo ikiwa ni utekelezaji wa masharti ya sheria. Fomu hizo za wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilibandikwa ili kutoa fursa ya kuweka pingamizi dhidi ya uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais ambapo pingamizi hilo linaweza kuwekwa na mgombea mwingine, Msajili wa Vyama vya Siasa au Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Fomu hizo zilibandikwa na Tume Saa 10:00 jioni ya Agosti 27, 2025 ambayo ilikuwa ni siku ya uteuzi na kuondolewa leo Agosti 28, 2025 Saa 10: 00 jioni.
3Z7A4728.JPG


3Z7A4742.JPG



3Z7A4783.JPG

3Z7A4765.JPG

3Z7A4749.JPG

3Z7A4779.JPG

3Z7A4788.JPG

DKT. BITEKO AZINDUA TEKNOLOJIA YA KUONDOA UVIMBE MWILINI BILA UPASUAJI

1000755915.jpg



πŸ“Œ Ni kwa mara ya kwanza kufanyika Afrika Mashariki na Kati


πŸ“Œ Aipa kongole Hospitali ya Kairuki kwa kutoa punguzo la asilimia 50 kwa wagonjwa 50 wa kwanza


πŸ“Œ Asema Serikali itaendelea kuweka msukumo ushirikiano na Sekta binafsi


πŸ“Œ Awaasa Watendaji Wizara ya Afya kutoogopa kujifunza pale Sekta binafsi inapofanya vizuri


πŸ“Œ Wagonjwa 300 wanufaika na teknolojia ya utoaji uvimbe bila upasuaji


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameziindua teknolojia ya kuondoa uvimbe mwilini bila upasuaji inayofahamika kama High-Intensity Focused Ultrasound (HIFU) katika Hospitali ya Kairuki ikiwa ni mara ya kwanza kwa huduma hiyo kuzinduliwa katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.


Akizindua huduma hiyo Agosti 27, 2025 jijini Dar es Salaam, Dkt. Biteko amepongeza Watendaji wa hospitali ya Kairuki pamoja na muasisi wake Hubert Kairuki na Mkewe kwa uthubutu wao katika masuala mbalimbali ikiwemo utoajiwa huduma hiyo ya HIFU ambayo imeiweka Tanzania katika rekodi ya kutoa uvimbe bila kufanya upasuaji barani Afrika suala ambalo pia litaongezea nchi mapato.


Ameeleza kuwa awali huduma ya HIFU barani Afrika likuwa ikipatikana katika nchi tatu tu ambazo ni Misri, Nigeria na Afrika Kusini.


Aidha, ameipongeza Hospitali ya Kairuki kwa kutoa punguzo la asilimia 50 la gharama za matibabu ya utoaji uvimbe bila upasuaji kwa wagonjwa 50 wa kwanza ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuanzia leo ikiwa ni kielelezo cha Watendaji wa hospitali hiyo kuonesha utu kwa Watanzania, kuacha alama njema na kuunga mkono dhamira ya Serikali ya kutoa huduma kwa watanzania kwa gharama nafuu.


Dkt. Biteko amesema kuwa kufanyika kwa tukio hilo muhimu ni kielelezo cha Serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuipa msukumo sekta binafsi na kuikuza ili kutoa huduma za matibabu kwa wananchi kwa ufanisi na kusogeza karibu huduma ambazo hapo awali zilikuwa hazipatikani ndani ya nchi hivyo ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono Sekta binafsi.


Β·Aidha, ameipongeza Hospitali ya Kairuki kwa kuanzisha Idara ya huduma za dharura ambayo ina uwezo wa kuhudumia wagonjwa zaidi ya 9,000 kwa mwaka.


Katika hatua, nyingine, Dkt. Biteko amewataka Watendaji katika Wizara ya Afya kutoogopa kujifunza kutoka Sekta binafsi pale inapofanya vizuri na wawape ushirikiano wakati wote siyo nyakati za ukaguzi tu kwani lengo la Serikali ni kufikisha huduma bora kwa wananchi kwa ushirikiano wa Serikali na sekta hiyo.


Kuhusu ombi la Hospitali ya Kairuki la kujengewa barabara ya lami ya mita 300 kuelekea kwenye hospitali hiyo ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi ameelekeza Manispaa ya Kinondoni kufanyia kazi ombi hilo.


Dkt. Mwinyikondo Amir, kutoka Wizara ya Afya akimwakilisha Waziri wa Afya, amesema kuwa tukio hilo ni ishara ya ushirikiano uliopo kati ya sekta binafsi na Serikali katika kutoa huduma bora kwa wananchi.


Amesema Wizara ya Afya imekuwa na ushirikiano mkubwa na Hospitali ya Kairuki katika masuala mengi ikiwemo matumizi ya Bima ya Afya na kwamba pande zote mbili zinatambua kuwa zina wajibu wa kutekeleza dira ya maendeleo ya 2050 inayoelekeza uwepo wa jamii yenye afya bora.


Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Afya na Elimu Kairuki, Kokushubila Kairuki ameishukuru Serikali kwa kutambua mchango wa sekta binafsi katika kuboresha huduma za afya nchini.


Amesema sekta ya afya imekuwa na maendeleo makubwa chini ya uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba hospitali hiyo itaendelea kuunga mkono juhudi hizo hasa ikiwa ni utekelezaji wa Dira 2050 inayolenga kujenga Taifa lenye uchumi imara na afya bora.


Amesema gharama za kuweka teknolojia hiyo ya HIFU ni shilingi Bilioni 12 na milioni 300.


Aidha amesema kutoka huduma ya HIFU ianze kutolewa tayari wananchi 300 wamepata huduma za uchunguzi huku 298 wakipata matibabu.


Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kairuki,Β Dk. Onesmo Kaganda alisema uzinduzi wa HIFU ni tukio la kihistoria kwakuwa ni mara ya kwanza kwa huduma hiyo kuzinduliwa katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.


Amesema teknolojia hiyo barani Afrika imeanzishwa katika nchi tatu tu ambazo ni Misri, Nigeria na Afrika Kusini.


Ameeleza kuwa HIFU ni Teknolojia ya kisasa inayotumia Mawimbi Sauti (Sound Waves) b kutibu aina mbalimbali za uvimbe mwilini bila upasuaji, ikiwemo uvimbe wa saratani na usiokuwa wa saratani katika maeneo kama Matiti, Kongosho, Kizazi kwa Wanawake, na Tezi Dume kwa wanaume.


Ameeleza faida za huduma hiyo kuwa ni pamoja na kutokuwa na kovu kwa kuwa hakuna upasuaji, mgonjwa hawekewi nusu kaputi na mgonjwa hupona kwa muda mfupi na kurejea katika shughuli zake, matibabu hayahitaji kumwongezea damu mgonjwa hata kwa wagonjwa wenye upungufu wa damu, pia kupunguza gharama za kwenda nje ya nchi kutafuta matibabu.


Ameongeza kuwa, faida nyingine ya HIFU ni pamoja na tiba shufaa ambayo husaidia dawa za saratani kufanyakazi vizuri mwilini, kufubaza kukua kwa saratani mwilini (slowdown disease progression) na kupunguza maumivu kwa wagonjwa wa saratani.


Amesema mtambo huo ulianza kufanya kazi desemba 2023 ambapo mpaka sasa wagonjwa 303 wamefanyiwa uchunguzi na 298 kupatiwa matibabu na kumekuwa na matokeo chanya ya wagonjwa hao.


Amesema kuwepo kwa teknolojia hiyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya za kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utalii Tiba Kusini mwa jangwa la Sahara.


Pia, amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka mazingira wezeshi ya ushirikiano kati ya Serikali na Taasisi Binafsi.


Kuhusu Idara ya Huduma za Dharura iliyozinduliwa katika Hospitali ya Kairuki amesema itakuwa na uwezo wa kuhudumia wagonjwa zaidi ya 9000 kwa mwaka na pia imejizatiti kwa magonjwa ya dharura pindi yatakapotokea.


Mwisho
1000755915.jpg
1000755914.jpg
1000755916.jpg
1000755917.jpg
1000755918.jpg
1000755919.jpg
1000755920.jpg
1000755921.jpg
1000755922.jpg
1000755924.jpg
1000755923.jpg
1000755925.jpg
1000755926.jpg
1000755927.jpg
1000755928.jpg

MGOMBEA UDIWANI KATA YA NGOGWA ABEL MABAO AREJESHA FOMU




1000756741.jpg


Mgombea udiwani wa Kata ya Ngogwa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Abel Mabao,Β  agosti 27, 2025 ameweka historia baada ya kurejesha fomu za kugombea nafasi hiyo katika ofisi za kata hiyo.

Mabao, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mabao Investment, amewasili katika ofisi za kata akiwa na wafuasi wake na kupokelewa na mtendaji wa kata Pendo Shirima ambaye amepokea fomu hizo kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi.

Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu, Mabao ameshukuru wafuasi wake na wananchi wa Ngogwa kwa mshikamano waliomuonesha, akiahidi kampeni zenye maadili na kujikita katika maendeleo ya jamii.

Zoezi la urejeshaji fomu za wagombea udiwani limetamatika leo nchini kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi.


1000756742.jpg
1000756752.jpg
1000756749.jpg
1000756741.jpg
1000756735.jpg
1000756737.jpg
1000756744.jpg
1000756732.jpg
1000756761.jpg
1000756759.jpg
1000756718.jpg
1000756721.jpg


KAILIMA AFUNGA KIKAO CHA UPANGAJI WA RATIBA YA KAMPENI ZA WAGOMBEA URAIS


INEC3266.jpg

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ndugu Kailima R.K, amefunga kikao cha siku mbili cha Tume na Vyama vya Siasa 18 vyenye usajili kamili na ambavyo vimependekeza wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais, kwa lengo la kujadili na kupanga kwa pamoja ratiba ya kampeni za vyama hivyo.


Kikao hicho kilichoketi Agosti 25 na 26, 2025 kilishirikisha vyama vya Civic United Front (CUF), National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi), Union for Multiparty Democracy (UMD), Chama cha Mapinduzi (CCM), National League for Democracy (NLD), United Peoples’ Democratic Party (UPDP) na National Reconstruction Alliance (NRA), African Democratic Alliance Party (ADA-TADEA).

Vyama vingine ni Tanzania Labour Party (TLP), United Democratic Party (UDP), Madini Kilimo Nishati (MAKINI), Democratic Party (DP), Sauti ya Umma (SAU), Alliance for African Farmers Party (AAFP), Chama cha Kijamii (CCK), Alliance for Democratic Change (ADC),Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) na Alliance for Change and Transparency (ACT-Wazalendo).


Kampeni za Uchaguzi zinatarajiwa kuanza Agosti 28, 2025 hadi Oktoba 28, 2025 nchini kote ambapo wagombea watakaoteuliwa na Tume watafanya kampeni za kunadi sera za vyama vyao kutafuta ridhaa ya wananchi kuwapigia kura Oktoba 29, 2025 katika uchaguzi mkuu.
INEC3262.jpg

INEC3255.jpg

INEC3254.jpg
INEC3278.jpg


INEC3273.jpg

DKT. DOTO BITEKO ACHUKUA FOMU KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA BUKOMBE





πŸ“Œ Wanachama zaidi ya 1000 wajitokeza kumdhamini




πŸ“Œ Dkt. Biteko ahimiza Kampeni za kistaarabu, mshikamano na upendo




πŸ“Œ Awaomba Wana Bukombe kumchagua Dkt. Samia, Biteko na madiwani wa CCM




Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati




Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Bukombe, Zedekiah Solomon Osan amemkabidhi fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Bukombe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Doto Mashaka Biteko leo Agosti 26, 2025 katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bukombe - Mkoani Geita.




Makabidhiano hayo ya fomu ni utekelezaji wa ratiba kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka 2025 Aidha, Maelefu ya wana CCM na wapenzi wa chama hicho wamemsindikiza mgombea kwa ajili ya kuchukua fomu kwa ajili ya kuomba kuteuliwa na Tume huru ya Uchaguzi.




Katika hali isiyo ya kawaida, zaidi ya wanama 1000 wamejotokeza kumdhamini Dkt. Biteko ikilinganishwa na mahitaji ya wadhamini 31 waliohitajika kisheria.




Akizungumza na wanaCCM katika viwanja Ofisi ya CCM Wilaya ya Bukombe, Dkt. Biteko amewataka wananchi kudumisha mshikamano na upendo miongoni mwao na kuwachagua viobgozi bora.




β€œ Utakapofika wakati tuwaxhague viongozi tunaowapenda, nawaomba mmchague Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais, Mnichague mimi kuwa mbunge na niwaaombe mbiletee madiwani wa CCM kwa tuendeleze kazi tuliyokwisha ianza,”




Awali, Katibu wa CCM, Wilaya Bukombe Leonard Mwakalukwa amesema wana CCM zaidi ya 3500 wamejitokeza kumsindikiza mgombea katika Ofisi za tume huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kuchukua fomu.




Amesema wadhamini 31 kutoka Kata zote 17 za Bukombe wamewawakilisha wenzao 969 waliojitokeza kumdhamini mgombea.




MWISHO