Fungua
Indaba Africa

Indaba Africa

Mbeya, Tanzania

Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri

GARI YA MH. DIWANI KATA YA SISIMBA MBEYA LAANGUKIWA NA MTI

DSC00155.JPG
Gari ya mheshimiwa diwani Geofrey Kajigili wa kata ya sisimba jijini mbeya likiwa limeangukiwa na mti ulioangushwa na mvua ilioambatana na upepo mkali
DSC00139.JPG
DSC00156.JPG
Mh. diwani Kajigili anaeongea na simu akiwa na mzee shariff na majirani wengine waliokuja mpa pole

AZRA VUYO JACK MTOTO ALIYEZALIWA MAHABUSU NA ANAENDELEA KUKULIA MAHABUSU WAZAZI WAKE WATUHUMIWA KUKUTWA NA MADAWA YA KULEVYA

Photo-0034.jpg
MTOTO AZRA VUYO JACK AKIWA AMELALA
Photo-0032.jpg
AZRA AKIWA AMEPAKATWA NA BABA YAKE VUYO JACK NJE YA MAHABUSU YA MAHAKAMA KUU MBEYA
Photo-0042.jpg
BABA NA MAMA AZRA WAKIWA NA MTOTO WAO WAKISUBIRI KUINGIA MAHAKAMANI JANA ASUBUHI
Photo-0043.jpg
ANASTAZIA CLOETE MAMA WA AZRA AKIFURAHI BAADA YA JOSEPH MWAISANGO WA MBEYA YETU KUMWAMBIA KWA UTANI KUWA ATAMCHUMBIA AZRA ILI ABAKI MBEYA
Photo-0045.jpg
WAKIWA NA NYUSO ZA FURAHA BAADA YA UTANI WA HAPA NAPALE NJE YA MAHABUSU YA MAHAKAMA KUU MBEYA
Photo-0037.jpg
MSAMARIA MWEMA EMILY MWAITUKA NDIYE ALIYEJITOLEA KUMHUDUMIA MTOTO AZRA HUKO MAHABUSU KWA KUMPELEKEA MAZIWA KILA SIKU
IMG00725-20101118-1355.jpg
HILI NDILO GARI LA WAZAZI WA AZRA
IMG00726-20101118-1355.jpg
Wakati Tanzania ikiwa imeridhia mkataba wa kimataifa wa kutekeleza na kulinda haki za watoto na kusimamia kwa karibu ulinzi wa haki za binadamu, sasa serikali ina kila sababu ya kuangalia haki za watoto walioko gerezani kwa makosa ya wazazi wao.
Miongoni mwa haki ambazo serikali inapaswa kuchunguza kwa undani na kubainisha kisa kilichosababisha mtoto mdogo wa kike wa miezi sita , Azra Vuyo Jack, ajikute yeye na wazazi wake wakiwa katika mahabusu ya gereza la Ruanda jijini Mbeya wakikabiliwa na tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya.
Azra ambaye kwa jina la utani, kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Mbeya yetu huko gerezani anaitwa Merryciana au bibi jela jina ambalo limezoeleka zaidi mbali ya jina lake halisi alilopewa na wazazi wake la Azra .
Mtoto huyo wa kike aliendelea kukua katika tumbo la mama yake akiwa gerezani, hatimaye alizaliwa salama Julai 15 mwaka jana katika hospitali ya wazazi meta.
Mama yake ni Anastazia Cloete (27) mwenye asili ya kizungu, raia wa Afrika ya kusini
Cloete alikamatwa mwaka juzi, Novemba katika mpaka wa Tanzania na Zambia , mji mdogo wa Tunduma akiwa mjamzito na kutupwa mahabusu katika gereza hilo hali iliyomfanya aendelee kulea ujauzito wake.
Uchunguzi wa kina uliendelea kufanywa na madaktari wa hospitali hiyo hadi alipojifungua salama.
Uchunguzi wa tukio la mtoto huyo hadi sasa umezusha mwendelezo wa harakati za kihabari na wanaharakati wa haki za binadamu kuona umuhimu wa kuondolewa kwa mtoto huyo ambaye kwa muda wote tangu azaliwe amekuwa akitumia maziwa ya kopo na hanyonyeshwi na mama yake mzazi.
Mmoja wa ya wasamaria wema aliyejitolea kuwahudumia watuhumiwa hao waliyokumbwa na tuhuma za kukutwa na dawa hizo ni Emily Mwaituka ambaye amekuwa akifanya kazi kubwa ili kuhakikisha mtpto anakuwa na afya nzuri kwa kununuliwa makopo mawili ya maziwa kila wiki tangu alipozaliwa julai, mwaka jana.
Mwaituka anasema amekuwa akinunua kopo moja la maziwa ya unga aina ya SMA 1 ambalo huuzwa sh 26000 na anapaswa kununua makopo mawili ili kuweza kumudu mahitaji ya mtoto huyo wa kike ambaye hanyonyi maziwa ya mama yake mzazi anayesubiri hatima ya kesi inayomkabili akiendelea kuwa mahabusu kwenye gereza la Ruanda jijini Mbeya.
Uchunguzi uliofanywa na Mbeya yetu umegundua kuwa Cloete aliyekuwa akisoma nchini kwao katika chuo cha Capetech alijifungua mtoto wa kike miezi sita iliyopita baada ya kushikwa uchungu akiwa mahabusu na kukimbizwa hospitali ya wazazi ya meta.
Cloete ambaye amekuwa akitumia majina mawili kwani alipolazwa katika hospitali hiyo aliandikishwa jina la Anastazia Elizabeth wakati alifikishwa hospitalini hapo kwa uchunguzi akiwa mjamzito Januari 14 mwaka jana na kufunguliwa jarada la matibabu lenye namba 46 – 26 – 83.
Uchunguzi umebaini kuwa raia huyo wa afrika ya kusini na mumewe , Vuyo Jack ( 31 ) waliokamatwa mpakani hapo, aligundulika kuwa mjamzito alipokuwa mahabusu na kuanza kupatiwa matibabu sahihi yaliyosaidia ujauzito wake kukua vizuri.
Habari za ndani zinadai kuwa kwa muda wote huo baada ya ujauzito wake kugundulika alikuwa akipatiwa matibabu chini ya uangalizi wa madaktari na alipofikia hatua za mwisho mjadala mzito ulifanywa na jopo la madaktari walioonyesha mashaka kuwa asingeweza kujifungua kwa njia ya kawaida na kutakiwa afanyiwe upasuaji.
Imeelezwa kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake katika hospitali hiyo Peter Msafiri , alipofanya uchunguzi alibaini kuwa raia huyo hapaswi kufanyiwa upasuaji kwa vile alikuwa na uwezo wa kujifungua bila matatizo.
Dk Msafiri alipohojiwa anasema Cloete alijifungua salama ingawa walitaka kumfanyia upasuaji lakini alipinga hatua hiyo na kudai kuwa anaweza kujifungua salama kwa njia ya kawaida.
Baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo ambao hawakutaka majina yao kutajwa walidai kuwa raia huyo wa Afrika ya Kusini alijifungua mtoto wa kike na kwamba mama yake akiwa mahabusu amekataa kumyonyesha kwa madai kuwa hapati mlo wa kutosha unaomuwezesha kutoa maziwa ya kutosha kwa ajili ya mwanae.
Cloete alilazwa hapo kwa ajili ya uchunguzi , hamnyonyeshi mtoto wake, kweli amejifungua mtoto mzuri wa kike, amesema kuwa hawezi kumnyonyesha na anamlisha maziwa ya kopo akidai kuwa akinyonyesha atakosa nguvu kwa kuwa mahabusu alikowekwa hapati lishe bora anadai muuguzi mmoja.
Miongoni mwa wanaharakati wa haki za binadamu walioguswa na habari za mtoto huyo kuendelea kukaa mahabusu na mama yake kulimgusa. Mchungaji William Mwamalanga, anasema kuwa kitendo cha mtoto huyo kuishi katika mazingira hayo hakuendani na haki za binadamu ambazo Tanzania imeridhia kwenye umoja wa mataifa.
Mwamalanga anasema yeye na wanaharakati wenzake wanaandaa mpango maalumu wa kupigania haki ya mtoto huyo na kuhakikisha kuwa anaondolewa mahabusu baada ya kubainika kuwa amekuwa hanyonyeshwi na mama yake mzazi tangu alipozaliwa kwa madai kuwa hawezi kumnyonyesha kutokana na lishe duni anayopata akiwa mahabusu.
Nakushukuru sana kuzisoma taarifa hizi, tunajiandaa ili kuona njia sahihi inayoweza kutusaidia kumtoa mtoto huyo mahabusu na kuiomba serikali iangalie kwa undani shauri hili kupitia kwa mwendesha mashtaka mkuu wa serikali ili kujua haki na stahili za mtoto huyo mchanga vinginevyo tunakiuka haki za watoto na binadamu ambazo Tanzania imeridhia kuzitekeleza, anasema Mwamalanga.
Kumbukumbu za tukio hilo tulizonazo zinaonyesha kuwa raia hao wawili wa Afrika ya Kusini, waliokuwa wakiishi mtaa wa 2A Valley Road – Schaapkraal – Capetown walikamatwa na kilo 42 .5 za dawa za kulevya Novemba 18 mwaka juzi katika mpaka wa Tunduma na kufunguliwa – jalada namba TDM/IR/1763/2010.
Katika tukio hilo ambalo Vuyo na Cloete walinaswa na dawa hizo walizozificha kwenye gari aina ya Nissana Hard body yenye namba za usajili CA – 508 – 656 lililokuwa likimilikiwa na Vuyo Jack waliokuwa wakitokea mkoani Morogoro kuelekea Afrika ya Kusini, Cloete alikuwa akisoma katika chuo cha Capetech.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani ambazo zimethibitishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali dawa hizo za kulevya ni paketi 26 za cocaine zenye uzito wa kilo 28.5 paketi tatu za Heroine zenye uzito wa kilo 3.25 na paketi nane aina ya Morphine zenye uzito wa kilo 3.25, madawa hayo yote yanathamani ya zaidi ya sh bilioni 1.2. picha na mbeya yetu Habari na Christopher Nyanyembe KUTOKA MBEYA YETU BLOG

Mbeya Yetu: AZRA VUYO JACK MTOTO ALIYEZALIWA MAHABUSU NA ANAEN...

AZRA VUYO JACK MTOTO ALIYEZALIWA MAHABUSU NA ANAEN...: MTOTO AZRA VUYO JACK AKIWA AMELALA AZRA AKIWA AMEPAKATWA NA BABA YAKE VUYO JACK NJE YA MAHABUSU YA MAHAKAMA KUU MBEYA BABA NA MAMA...

Boko Haram's threat letter to NLC/TUC; real or fake?

NLC-BH.png
According to the leadership of the NLC and TUC, they received a threat letter in their mail yesterday supposedly sent by Boko Haram. In the letter (above), the Islamic sect expressed their anger over the way the Labour leaders handled the fuel hike crisis. They asked the NLC president to resign and also threatened to bomb their HQ soon.
The letter reads 'I', 'AM' instead of 'WE'...probably a prank but the NLC people are taking it very seriously. They've handed the letter to security agencies. If this Boko Haram menace wasn't such a sad thing for Nigerians, I would have laughed at this letter. But....

GCx2N0qi4Zw

Photos from Kanu Nwankwo's wife's 25th birthday and graduation

amarakanu+lindaikejiblog.jpg1.jpgamarakanu+lindaikejiblog.jpg
This happened a while back (2011) but the photos only just hit the net. Kanu and Amara married in 2004 and have two boys together. Continue to see more photos...
amarakanulindaikejiblog.jpgamarakanu+lindaikejiblog.jpg1.jpg7.jpg
amarakanu+lindaikejiblog.jpg2.jpgamarakanu+lindaikejiblog.jpg4.jpg
amarakanu+lindaikejiblog.jpg3.jpg
amaralindaikejiblog.jpg
amara2lindaikejiblog.jpg

_j8p8Hq8duM

MTOTO AVUNJA MLANGO NA KUMBAKA MAMA YAKE MZAZI AKIWA AMELALA

Na Mwandishi Wetu, Songea ------------------------------------------------------------------------------------------------- JESHI la polisi Mkoani Ruvuma linamshikilia Frank Jota (26) mkazi wa kijiji cha Litisha Wilayani Songea kwa tuhuma za kumbaka mama yake mzazi mwenye umri miaka 54 ambaye jina lake limehifadhiwa wakati amelala nyumbani kwake majira ya saa za usiku. Kamanda wa Polisi Koa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amesema kuwa tukio hilo limetokea januari mosi mwaka huu huko katika kijiji cha Litisha kilichopo nje ya mji mdogo wa Peramiho. Amesema kuwa siku hiyo ya tukio majira ya saa za usiku Jota alikwenda nyumbani kwao ambako alimkuta mama yake mzazi akiwa amelala na baadaye alianza kutafuta namna ya kuingia kwenye nyumba hiyo ambayo mlango wake ulifungwa na komeo kwa ndani. Amefafanua zaidi kuwa Jota baada ya kuona mlango umefungwa kwa komeo kwa ndani aliamua kuuvunja mlango wa nyumba hiyo kisha aliingia ndani na kwenda moja kwa moja kwenye chumba alicholala mama yake mzazi ambaye jina lake limehifadhiwa. Amesema kuwa Jota akiwa kwenye chumba ambacho mama yake alikuwa amelala alianza kumtishia kwa kisu alichokuwa ameshika mkononi na baadaye alimkaba shingo na kufanikiwa kumvua nguo ya ndani aliyokuwa amevaa kisha alianza kufanya naye mapenzi. Amebainisha zaidi kuwa wakati Jota akiendelea kufanya mapenzi na mama yake watu waliokuwa jilani na tukio walisikia kelele za mtu akipiga mayowe na walipofika kwenye eneo hilo la tukio waliingia ndani ya nyumba hiyo na kumkuta Jota akitokea kwenye chumba alicholala mama yake na baadaye alipowaona watu alijalibu kukimbia lakini majirani hao walifanikiwa kumkamata na kumpeleka kituo kidogo cha polisi cha peramiho. Hata hivyo kamanda wa polisi Mkoa wa Ruvuma Kamuhanda ameeleza kuwa polisi baada ya kumuhoji mtuhumiwa amekili kutenda kosa hilo na anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara tu upelelezi utakapo kamilika. Mwisho.

MTOTO AVUNJA MLANGO NA KUMBAKA MAMA YAKE MZAZI AKIWA AMELALA

Na Mwandishi Wetu, Songea ------------------------------------------------------------------------------------------------- JESHI la polisi Mkoani Ruvuma linamshikilia Frank Jota (26) mkazi wa kijiji cha Litisha Wilayani Songea kwa tuhuma za kumbaka mama yake mzazi mwenye umri miaka 54 ambaye jina lake limehifadhiwa wakati amelala nyumbani kwake majira ya saa za usiku. Kamanda wa Polisi Koa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amesema kuwa tukio hilo limetokea januari mosi mwaka huu huko katika kijiji cha Litisha kilichopo nje ya mji mdogo wa Peramiho. Amesema kuwa siku hiyo ya tukio majira ya saa za usiku Jota alikwenda nyumbani kwao ambako alimkuta mama yake mzazi akiwa amelala na baadaye alianza kutafuta namna ya kuingia kwenye nyumba hiyo ambayo mlango wake ulifungwa na komeo kwa ndani. Amefafanua zaidi kuwa Jota baada ya kuona mlango umefungwa kwa komeo kwa ndani aliamua kuuvunja mlango wa nyumba hiyo kisha aliingia ndani na kwenda moja kwa moja kwenye chumba alicholala mama yake mzazi ambaye jina lake limehifadhiwa. Amesema kuwa Jota akiwa kwenye chumba ambacho mama yake alikuwa amelala alianza kumtishia kwa kisu alichokuwa ameshika mkononi na baadaye alimkaba shingo na kufanikiwa kumvua nguo ya ndani aliyokuwa amevaa kisha alianza kufanya naye mapenzi. Amebainisha zaidi kuwa wakati Jota akiendelea kufanya mapenzi na mama yake watu waliokuwa jilani na tukio walisikia kelele za mtu akipiga mayowe na walipofika kwenye eneo hilo la tukio waliingia ndani ya nyumba hiyo na kumkuta Jota akitokea kwenye chumba alicholala mama yake na baadaye alipowaona watu alijalibu kukimbia lakini majirani hao walifanikiwa kumkamata na kumpeleka kituo kidogo cha polisi cha peramiho. Hata hivyo kamanda wa polisi Mkoa wa Ruvuma Kamuhanda ameeleza kuwa polisi baada ya kumuhoji mtuhumiwa amekili kutenda kosa hilo na anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara tu upelelezi utakapo kamilika. Mwisho.

WABUNGE WA TANZANIA WATEMBELEA UINGEREZA

Mhe.+Balozi+Peter+Kallaghe+akiwakaribish
Mhe. Balozi Peter Kallaghe akiwakaribisha waheshimiwa wabunge
Katibu+wa+Chama+cha+wanawake+UK+%2528TAW
Katibu wa Chama cha wanawake UK (TAWA UK) Mariam Mungula akiwaeleza waheshimiwa machache kuhusu chama hicho
Afisa+wa+Bunge+Mrs+Justina+Shauri%252C+M
Afisa wa Bunge Justina Shauri, Mhe. Esther Matiku, Mhe. Beatrice Shelukindo na Mama Balozi Joyce Kallaghe wakiwa wanamsikiliza mhe. Balozi akitoa ukaribisho
Mwana+libeneke+Jestina+George+akiwa+kati
Mwana blogger Jestina George akiwa katika picha ya pamoja na waheshimiwa Al-Shaymaa J. Kwegyir, Agripina Z Buyogera na Susan Lyimo
Picha+ya+pamoja+na+waheshimiwa+baada+ya+
Picha ya pamoja na waheshimiwa baada ya chakula cha jioni
Wageni 11 wakiwemo Wabunge 11 na Afisa wa Bunge 1 waliotokea nyumbani Tanzania na kuja UK kwa Mualiko wa Commonwealth parliamentarians Group (CPA) walikaribisha chakula cha jioni na Mama Joyce Kallaghe Mke wa Balozi wa Uingereza akiwa na Viongozi wa Chama cha TA na TAWA nyumbani kwake.
Wabunge hao 11 wote wanawake na ambao miongoni mwao ni Viongozi wa wajumbe wa Tanzania Women Parliamentarians Group (TWPG) ,waliongozwa na Mwenyekiti wa TWPG Mheshimiwa Mama Anna Abdalla MP, na wakiwemo Mh.Susan Lyimo MP, Mh. Magdalena h. Sakaya (MP) , Mh. Angela Kairuki (MP), Mh. Esther matiko (MP, Mh. Beatrice Shelukindo (MP), Mh. Riziki Omari Juma (MP), Mh. Namalek Sokoine (MP), Mh . Faharia Hamisi (MP) ,Mh. Al-Shaymaa J. Kwegyir (MP), Mh. Agripina Z Buyogera (MP) na Afisa wa Bunge Mrs Justina Shauri.
Wageni walikaribishwa na Balozi Mheshimiwa Peter Kallaghe na Mama Balozi Joyce Kallaghe , Mheshimiwa Balozi aliongea machache ya Ukaribisho na kumpa nafasi Mh.Mama Anna Abdalla ambae alishukuru kwa mualiko huo na kuelezea kuhusu Umoja wa Wabunge Wanawake (TWPG) ambao kila Mbunge Mwanamke wa Bunge la Tanzania ni mwanachama wake na jinsi gani TWPG inavyofanya kazi kwa pamoja bila ya kujali itikadi za vyama vya kisiasa vya Waheshimiwa hao.
Usiku huo iliweza dhihirika kwa jinsi waheshiwa hao walivyokuja kujitambulisha kila mmoja alisimama na kujitambulisha na walilotilia msingi katika utambulisho wao ni kamati zao tofauti za Bunge ambazo wanahusika nazo na kuwa wnachama wa kikundi cha TWPG. Wageni waliokuwa pale walishuhudia zaidi ya nusu ya hawa wabunge waliongia na furaha bila ya kujali kuwa bado wana uchovu wa safari kutoka nyumbani wakisahau kutaja vyama vyao vya kisiasa. Mheshimiwa Mama Anna Abdalla alisisitiza kwamba ingawa vyama vya siasa ndio vilivyowapeleka wote bungeni lakini wakishaingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano ,wanawake bungeni hawaangalii vyama vyao vya siasa bali huwa wakiwa Bungeni kabla ya sera yeyote kupita Wanawake huwa wote kwa Umoja wanaangalia hii itamnufaisha vipi Mwanamke na Mtoto wa Kitanzania.
Maneno haya ya Mheshimiwa Mama Abdalla yalidhihirishwa na jinsi Waheshiwa wote walipokaa katika meza moja na kuongea na kucheka kwa pamoja na kwa furaha huku wakila chakula kitamu cha jioni bila ya kujali pale kwenye ile meza kuna CCM, NCCR, CUF wala CHADEMA.
Kitendo hiki kiliwavutia sana viongozi wa wanawake London ambao walikuwepo katika shuguli hii Bi. Nelly Msemwa (TA Taifa Deputy chair anaeshughulikia mambo ya wanwake ),Bi. Mariam Kilumanga(TAWA Chair ), BI Mariam Mungula (TAWA Secretary) , Bi Rose Kiondo (Afisa Ubalozi) na Bi Jestina George (TA London na Blogger), kiasi ambacho walipopewa nafasi ya kuongeza machache walimpa nafasi hii Bi Mariam Mungula ambae aliwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wa kitendo hicho na somo walilompa la kuwa hata Wakiwa Bungeni yeye akifikiri hakuna mashirikiano kati ya vyama tofauti kumbe sivyo kabisa wakiwa ndani na nje ya Bunge wanaweka wote ni kitu kimoja.
Bi Mariam Mungula vilevile alielezea kaazi za kikundi wa kina mama cha hapa UK ambacho yeye ni mmjoa wa viongozi wake Tanzania Women Association (TAWA) na kumalizia kwa kuwaomba waheshimiwa wabunge kupitia TWPG wasihau kuwa kuna wanawake wengine wa kitanzania hata kama ni nje ya nchi na ambao wako tayari kushirikiana nao kwa lolote katika kumuendeleza MWanamke wa KItanzania.
Kikundi hichi cha Waheshimwa kimekuja Uingereza kwa Mualiko wa CPA kwa siku chache katika majukumu yao ya kila siku ya kumpingania Mtanzania.
Mungu Ibariki Tanzania.
Na Jestina George wa www.jestina-george.com
cleardot.gif

N8LYvOe3UMY

BALOZI SEIF ALI IDDI AZUNGUMZA NA MABALOZI WAPYA WALIOTEULIWA HIVI KARIBUNI

270.JPG
MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKIZUNGUMZA NA MABALOZI SITA WAPYA WALIOTEULIWA KUIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MATAIFA MBALI MBALI DUNIANI.
278.JPG
MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MABALOZI WAPYA WA TANZANIA WALIOTEULIWA HIVI KARIBUNI.

UTAFITI: WAKAZI WA NCHI ZA BARIDI WANA MACHO NA UBONGO MKUBWA KULIKO WAKAZI WA NCHI ZA JOTO

brain.jpg
Matokeo ya utafiti yaliyochapishwa mwaka jana yanaonyesha kwamba watu wanaoishi katika ukanda wa nchi za baridi juu ya mstari wa Ikweta wana macho na ubongo mkubwa zaidi kuliko wenzao wanaoishi karibu na mstari huo.
Kwa vile nchi nyingi za baridi mbali na mstari wa Ikweta zipo Ulaya, Urusi, Asia na Amerika ya Kaskazini, hii inamaanisha kwamba wakazi wa nchi hizi wana macho na ubongo mkubwa.
Na kwa vile sote tunajua kwamba ubongo mkubwa unahusianishwa moja kwa moja na akili nyingi, swali la muhimu linalozushwa na utafiti huu ni hili: Wakazi wa nchi za baridi (wengi wao ni weupe) wana akili kuliko wakazi wa sehemu zilizo karibu na Ikweta (weusi)?
Japo watafiti wamekwepa kufanya jumuisho hili, inavyoonekana wamefanya hivyo ili kukwepa mitafaruku tu. Je, ugunduzi huu mpya unaweza kueleza tofauti za kimaendeleo na kisayansi kati ya watu wa “kaskazini” na “kusini”?
Mgunduzi mwenza wa “DNA” mwenyewe alipata matatizo makubwa alipotoa dai kama hili mwaka 2007, dai ambalo lilimfanya afukuzwe au kujiuzulu nyadhifa zake zote za kisayansi na kiuongozi alizokuwa akizishikilia
Kwa maoni ya kutatanisha kuhusu mkondo huu wa mawazo tazama maoni ya binti machachari wa Kichaga aitwaye Aika HAPA. Maoni haya yaliwasha moto mkubwa sana huku wengine wakimshambulia na wengine wakimuunga mkono.
Wewe una maoni gani? Ni kweli watu weusi tuna akili “pungufu” tukilinganishwa na weupe?