Wajibu na majukumu ya mkutano Mkuu wa kijiji ni pamoja na:
.kupokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli mbalimbali;
.Kupokea na kujadili mapato na matumizi ya fedha;
.Kupokea na kujadili taarifa za makusanyo ya fedha;
.Kupokea na kujadili taarifa za makusanyo ya fedha yakiwawamo ya ushuru,ada na mapato mengine yanayopaswa kukusanywa ndani ya kijiji kwa mujibu wa sheria;
.Kupokea na kujadili taarifa za watu walioomba kupewa ardhi;
.Kupokea na kujadili mapendekezo ya takayotolewa na halmashauri ya Kijiji au kitongoji;
.Kupokea maagizo(kama yapo) kutoka ngazi za juu za utekelezaji;
.Kufanya maamuzi yanayozingatia demokrasia;
.Kuchagua Mwenyekiti na Wajumbe wa Hamashauri ya kijiji;
.Kujadili na kupitisha bajeti na mipango ya maendeleo ya kijiji.
|