Tumeamua kujikita katika shughuli za kilimo hususani kilimo cha bustani na ufugaji wa kuku. Ni dhamira yetu kuhakikisha kuwa jamii inapata lishe bora na salama kwa afya, ni fahari kwetu kuona kuwa vijana wanaelimika na kuchagua mfumo wa maisha kiuchimi kupitia rasilimali zinazo wazunguka kama nyezo ya kuwainua kiuchumi, jamii inahitaji nyama ya kuku na mazao mengine ya kuku kama Mayai na mbolea ya kinyesi cha kuku. Mazao haya ya kuku ni frusa kwa vijana kwani wakielimishwa na wakawa tiari kuwekeza katika sekta ya ufugaji kupitia Ndege jamii ya kuku watakuwa wamekubali kutatua Matatizo yaliyopo katika jamii yatokanayo na uhaba wa mazao ya kuku. Sisi kama ASASI ya AUVITA tumejidhatiti kwa dhati kuwekeza kwa vijana wa Tanzania ili kuwawezesha kukabiliana na uhaba wa ukosefu wa ajira. Takwimu zonaonesha kuwa idadi ya watu inazidi kuongezeka kila leo na watu Hawa wanahitaji kula na wenyejukumu la kuwalisha ni sisi vijana kwa kuwekeza katika sekta ya kilimo. Hivyo tukiwa kama vijana tunatoa rai kwa watanzania vijana kuwekeza katika sekta ya kilimo ili kujikwamua kiuchumi na kukidhi nahitaji ya Chakula. Pichani ni kuku wa Kienyeji walioboreshwa kwenye asili ya India.
TANZANIA NA UZALENDO WETU TUMEKOSEA WAPI?
Uzalendo ni kitendo cha mtu kuipenda nchi yake, rasilimali zilizomo na watu wake kwa moyo wa dhati kwa kuilinda, kuithamini wakati wote na mahali popote.
Uzalendo katika nchi ndio chanzo cha maendeleo na usawa kwa watu wote nchini. Uzalendo unaleta haki, uzalendo unajenga misingi ya kujaliana, uzalendo ndio chachu ya matumizi ya rasilimali za nchi kwa usawa, uzalendo unatujengea undugu na amani, uzalendo unajenga na kudumisha upendo, uzalendo unajenga na kudumisha ushirikiano, uzalendo unajenga misingi ya uwajibikaji kwa wanajamii, uzalendo huondoa unyonyaji na matabaka katika jamii.
Uzalendo ni upendo na dhana ya hiari ya mtu binafsi uzalendo hujengwa kutoka moyoni mwa mtu, wakati mwingine uzalendo hujegwa na wanajamii kipitia misingi ya maisha wanayoyaishi na itikadi ya kisiasa miongoni mwa wanajamii. Hivyo mtu anaweza kuzaliwa akiwa mzalendo au itikadi ya kisiasa na misingi ya maisha katika jamii inaweza kumjenga mtu katika hali ya uzalendo.
Uzalendo unagawanywa katika aina mbili; a) uzalendo wa kihistoria ambao unatokana na maisha ya watu waliotangulia katika jamii. b) uzalendo wa kiutu. Huu ni uzalendo ambao huchukulia binadamu kama alivyo. Mfano katika Biblia maandiko yanasema mpende jirani yako kama nafsi yako.
Katika taifa letu dhana ya uzalendo imepotea miongoni mwa wanajamii. Historia inaonesha Tanzania imepitia vipindi mbalimbali; kipindi cha kabla ya ukoloni, wakati wa ukoloni, wakati wa kupigania uhuru na wakati baada ya uhuru. Kila kipindi kilijengwa na misingi yake ya uzalendo.
Kipindi kabla ya ukoloni historia inaonesha kuwa mababu zetu waliishi katika misingi ya umoja mshikamano na undugu, walifanya kazi kwa kushilikiana waliishi kama wamoja, rasilimali ziliwanufaisha wote watu wote walikuwa na haki sawa katika utumiaji wa rasilimali. Kipindi hiki kilitawaliwa sana na uzalendo wa kiutu.
Kipindi cha ukoloni. Historia inaonesha kuwa kipindi hiki wakoloni walitumia kila mbinu kuuvunja na kuundoa kabisa uzalendo miongoni mwa wanajamii. Walitujengea mioyo ya chuki, walituondolea umoja, walitujengea ubaguzi, walitugawa ili watutawale. Yote haya waliyafanya kwa manufaa yao binafsi ya kuzinyonya rasilimali za waafrika, walitumia Ardhi yetu kujinufaisha , walitumia udhaifu wetu kutufarakanisha, walitujengea matabaka katika jamii. walichonacho walikuwa nacho na wasiokuwa nacho waliendelea kukosa, elimu ilitolewa kwa misingi ya ubaguzi katika jamii, rasilimali za nchi zilitumika kuwanufaisha wachache wenye vyeo na madaraka tu. Hakika wakoloni walifanikiwa kutufarakanisha waafrika na kutuondolea uzalendo wetu.
Wakati wa kupigania uhuru. Hiki ni kipindi ambacho waafrika wenyewe tulianza kujijengea mioyo ya uzalendo tulioupoteza kupitia ukoloni, tulijijenga pamoja kushirikiana na kupambana dhidi ya ukoloni. Kipindi hiki mioyo ya uzalendo ilijegwa upya katika jamii ya watanzania. Baba wa Taifa alitumia juhudi zake kupitia Chama cha TANU kutuunganisha pamoja , tuwe wamoja , kutujengea upendo na baadae kushirikiana kudai uhuru wetu tukiwa kitu kimoja na wamoja.
Waasisi wetu walitumia juhudi zao kuujenga uzalendo na upendo katika jamii wakaiacha mizizi kwa mategemeo kwamba kizazi kilichofuata kingeendeleza hali ile.
Tanzania ya sasa si ile ya waasisi wetu, uzalendo tuliojengewa hatunao tena, umoja na mshikamano vimepotea sasa kila mtu akwenda kivyake nchi inapoteza mwelekeo , umasikini unakua kiuhalisia lakini unapungua kitakwimu, matabaka yanazidi kuongezeka makuadi wa kupoteza uzalendo wetu wanaongezeka kila siku, rasilimali sasa zinawanufaisha watu baadhi. Kwa mioyo migumu waliyo nayo sasa hata madaraka wanarithishana ili tu kujilinda. Taifa linahitaji jitihada za kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa tunautetea na kuuendeleza uzalendo wetu kwa maendeleo yetu . matabaka tuyaonayo leo ni matokeo ya kukosekana kwa uzalendo miongoni mwetu, misingi ya utu, ummoja, undugu sasa tumeipoteza kila mtu anafanya ajualo. Mabadiliko yanaletwa na mimi na wewe tumia nafasi yako vizuri kujenga usawa, utu, uwajibikaji, undugu katika jamii kwa maendeleo ya Taifa letu.
TUNAIENZIJE SIKU YA MAZINGIRA?Umepanda mti leo?
Leo ni siku ya mazingira duniani ambayo inatukumbusha kuwa uhai wetu inalindwa na mazingira yetu, hivyo tukiwa kama wadau katika sekta ya mazingira tunawakalibisha wadua na wahifadhi mazingira ili kuu tetea uhai wetu kwani kuishi kwetu kunategemea mazingira yetu.
Nikweli kabisa kuwa hatunabudi kuyalinda na kuyahifadhi mazingira yetu na kuienzi siku hii kwa fulaha kwani inatupa matumaini mapya ya kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi yanayo itikisa Dunia.
Mazingira yetu ni uhai wetu tuyalinde yatulinde. kama hatutaona umuhimu wa kuyalinda mazingira basi tunamtizamo wa kuyakatisha maisha yetu, Pamoja na uhifadhi wa mazingira tunayaweka mazingira ya uhai wa viumbe wengine katika hali safi yaani uhifadhi wetu wa mazingira unayaboresha si tu maisha ya binadamu bali na viumbe wengine.
Siku hii iwe chachu ya kutujengea misingi bora ya kuyaheshimu maeneo yaliyotengwa sehemu mbalimbali nchini kwa kuendelezwa kimazingira na kuyaheshimu maeneo haya, serikali hainabudi kushughulikia suala la mgawanyo wa maeneo yatuzungukayo kulingana na matumizi na kuzisimamia sheria kikamilifu.
Pia jamii ifahamu kuwa uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila mtu na inatupasa kushiriki wote kakamilifu juu ya suala zima la kuyahifadhi mazingira yetu.
Uhai wetu ni mazingira yetu tuyalinde yatulinde
MAANDIKO YA MWALIMU J. K. NYERER.
Kwa vijana kitabu hiki kinatufaa sana katika kutujengea misingi bora ya uongozi na maadali memea naomba tukisome.
1: Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (1994) - Mwl Nyerere
Download: http://dl.dropbox.com/u/52629254/dot...JK_Nyerere.pdf
2: Uongozi wetu na Hatma ya Tanzania - (Toleo la Kizazi Kipya)
Download: http://dl.dropbox.com/u/52629254/dot...wanakijiji.pdf
Ndugu Simba Mramba .
Mwanzilishi wa Asasi ya Ukombozi wa Vijana Tanzania (AUVITA) na ndiye mwenyekiti wa sasasi hiyo. Anawakaribisha vijana katika ukombozi mpya. Sikuzote huamini kuwa hamuna lisilowezekana Duniani na maisha ya mtu hupangwa na mtu mwenyewe, kwa ushirikiano na vijana kwa kuwapatia elimu mbalimbali maisha ya vijana yatabadilika na kuondokana na tatizo la ukosefu wa ajira.
Anasema kuwa.
Ni dhahili kabisa jamii ya watanzania inahitaji elimu mbadala tofauti na ya darasani ambayo itawajengea wanajiamii hususani vijana misingi ya kujiami, kupata utashi wa kuhoji,kudadisi na kujua nini kinaendelea katika jamii. vijana wanatakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika jamii washiriki katika shughuri za uzalishaji na maendeleo ya jamii zao kila mmoja, wafanye kazi kwa tija na kuwajibika popote walipo, waondoe mawazo mgando ya utegemezi na wajiajiri wenyewe kupitia rasilimali zinazo wazunguka, waondoe mtazamo hasi na wajenge fikra chanya juu ya maisha yao.
"umasikini si janga kama tetemeko la aridhi, njaa na mafuriko bali husababishwa na binadamu mwenyewe na anaweza kuuondoa mwenyewe kwa kutambua wajibu wake na kuwajibika" Simba Mramba.
"Ni bora ufanyekitu kwenyejamii ambacho sikumoja jamii itakukumbuka na kuishi kwako kutaonesha thamani katika jimii kuliko kuishi kusahaulika" Simba Mramba.