Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

Christina Shusho Tena

shusho.jpg
Christina Shusho
Kwa muda mrefu sasa media nyingi za Tanzania zimekuwazikiplay nyimbo za kundi la Christ Ambassadors Choir. Album ya kundi hilokutoka Kigali Rwanda iliyopewa jina laKWETU PAZURI (Video na Audio) kwa takribani miezi mitano toka August 2011 imekuwa ikisikika sio tukwenye media bali hata majumbani, mitaani na sehemu mbalimbali. Kitendo chaChristina shusho kuingiza sokoni album yake ya VIDEO iitwayo NIPE MACHO mnamotarehe tarehe 23/dec/2011 imeonekanakuteka hisia za wengi kwa utukufu wa Mungu.
Katika Video Album hiyo ya Shusho iliyofanywa tena nakampuni ya MBC HOTMEDIA, nyimbo ya kuabudu iitwayo NATAKA USHIRIKA NA WEWEndiyo inayoongoza kuchezwa katika media mbalimbali ambapo jumapili iliyopita yatar 1jan 2011 nyimbo hiyo pamoja na Nyingine iitwayo NINA WIMBO zilichezwa kwamara ya kwanza na katika kituo acha Television ya CITIZEN cha nchini Kenyakatika kipindi cha RAUKA Kinachotayariswha na K-KREW.
Wakati Christina Shushu ameuanza Mwaka huu wa 2012 kwakishindo kwa album yake hiyo ya Video, nguli mwingine wa Muziki wa injilinchini ROSE MUHANDO na yeye Mwaka huu wa 2012 anatarajia kuingiza sokoni albumyake ya Video iitwayo” UTAMU WA YESU” baada ya ile ya Audio aliyoitoa mapemamwaka jana. Kufanya Vizuri kwa Video album hii ya NIPE MACHO ni hatua ya kwanzakabla hajaachia Video album yake nyingine iitwayo KWA KANISA LA KRISTO.
shusho+dvd.jpg
kutoka hosannac ink

Amri ya kutotembea yawekwa Nigeria

Amri ya kutotoka nje wakati wowote ule imetangazwa katika jimbo la Adamawa, Nigeria, baada ya mashambulio kadha dhidi ya Wakristo.

Mashambulio dhidi ya makanisa, Nigeria

Jeshi limeshika zamu mabarabarani, na taarifa kutoka mji mkuu wa jimbo, Yola, zinaeleza kuwa maduka na maofisi yote yamefungwa, na huduma za lazima tu ndio zinaruhusiwa.

Wafuasi wa kikundi cha Waisalmu wenye siasa kali, Boko Haram, wameshambulia kanisa, kituo cha jamii, na duka la msusi katika siku za karibuni, na kuuwa watu kama 29.

Sheria za dharura zilianzishwa katika majimbo kadha mengine ya kaskazini mwa Nigeria juma lilopita, ambako Boko Haram wamefanya mashambulio piya.

Kikundi hicho kimeuwa watu zaidi ya 500 katika muda wa mwaka.

BBC

Nyoni: Hakuna daktari aliyefukuzwa MNH

SERIKALI imesema haijawafukuza madaktari walio katika mafunzo ya vitendo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) waliogoma hivi karibuni na wala haina mpango wa kama huo.

Hayo yamesema na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni.

Katibu huyo amelazimika kutoa ufafanuzi huo kutokana na vyombo kadhaa vya habari kuripoti kuwa, madaktari 229 walio katika mafunzo ya vitendo katika hospitali ya Muhimbili wamefukuzwa kutokana na kufanya mgomo wa nchi nzima kwa lengo la kushinikiza serikali kuwalipa malimbikizo ya posho zao yanayofikia Sh milioni 176.

Aliongeza kusema kuwa, ingawa madaktari hao walikiuka maadili ya weledi kwa kufanya mgomo, hakuna daktari aliyerudishwa nyumbani wala kufutiwa mkataba kutokana na ukweli kuwa siku zote serikali inatumia busara na njia sahihi kutatua matatizo bila kumuumiza mtu.

“Hakuna daktari aliyefukuzwa, bali serikali inafanya utaratibu wa kuwaita makao makuu ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupokea maelekezo ya mkataba mpya ili waweze kufanyakazi kwa kuzingatia kanuni na maadili na kurudisha nidhamu katika fani ya udaktari.

Wakati huo huo, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda amesema Taifa linakabiliwa na uhaba mkubwa wa madaktari na watenda kazi katika sekta ya afya hivyo serikali haikusudii kupunguza idadi yao.

Akizungumza na HABARILEO Jumapili kwa njia ya simu, Dk Mponda alisema baada ya mgomo huo kutokea serikali ilichukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha kuwa wagonjwa wanaendelea kupata huduma ili kuzuia madhara ambayo yangeweza kusababishwa na mgomo huo.

Alisema hatua mojawapo iliyochukuliwa na serikali ni kuchukua madaktari 50 waliokuwa katika orodha ya madaktari waliokuwa wakisubiri kupata nafasi ya kufanya mafunzo kwa vitendo na kuwajumuisha na madaktari wengine 25 ambao hawakujihusisha na mgomo huo.

“Kwa kuwa tulikuwa na akiba ya madaktari ambao walikuwa wanasubiri fursa ya kufanya mafunzo kwa vitendo tuliwaita na kuwapa fursa iliyoachwa na wenzao waliogoma. Tulifanya hivyo kuzuia athari za mgomo hivyo serikali haina mpango wa kufukuza wala kupunguza wafanyakazi wa seta ya afya.

Anafafanua kuwa lengo la kuwaita wizarani madaktari waliopo kwenye mafunzo kwa vitendo ni kuwapangia vituo vipya vya kazi na kuwapatia mkataba ambao utasaidia kuboresha nidhamu katika sekta ya afya.

Baadhi ya magazeti ya kila siku nchini (siyo HABARILEO), katika matoleo ya jana yalipamba kurasa zao za mbele kwa habari za kufukuzwa kwa madaktari 229 kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa madai ya kujihusisha na mgomo uliodumu kwa siku mbili wakishinikiza kulipwa malimbikizo ya posho.

Source: Habarileo

ATTENTION..! ATTENTION..! ATTENTION...!

Did you know you can now listen to all this channels from your celphone or house phone within the UNITED STATES for free..? If you are on unlimited phone plan DIAL any of this numbers 212-419-4655 or 712-432-2370 or 312-523-0813, once your call goes through dial *1 to *19 to choose your favourite channel. We are the leading phone application in the States..Have questions call us on 202-361-5970 Radio Stations List Dial star *1 - East-Africa Radio-usa Dial star *2 - West fm Bungoma (Kenya) Dial star *3 - Homeboyz Radio (Kenya) Dial star *4 - 1fm (Kenya) Dial star *5 - Pride fm (Mtwara, Tanzania) Dial Star *6 - Ebony fm (Tanzania) Dial star *7 - Hope fm (Kenya) Christian Dial star *8 - Kass fm (Kenya) Vernacular Dial star *9 - Kameme fm (Kenya) Vernacular Dial star *10 - Radio Maria (Tanzania) Christian Dial star *11 - Tellstream Radio (Kenyan-uk) Reggae Dial star *12 - CBS (Uganda) Dial star *13 - Radio Salaam (Mombasa, Kenya) Dial star *14 - African Radio online (Soukous) Dial star *15 - Radio Simba (Uganda) Luganda Dial star *16 - Radio Maria (Uganda) Christian Dial star *17 - Kross Radio Dial star *18 - Sagal Radio (Somalia) Dial star *19 - Radio Maria (Mozambique) Christian The following stations will be coming soon. 1-Classic 105 Kenya 2-Kiss 100 Kenya 3-Radio Citizen (Royal media stations) 4-Radio maisha 5-Qfm 6-Star fm 7-Clouds fm 8-Minto fm 9-KBC (All its stations) You can also request or list your favourite station by sending us an email to info@eastafricaradiousa.com or call us on +1 202 361 5970 and ask for Denzel E. Musumba We take you back home because we know you are busy or you have no internet..Share with friends.
cleardot.gif
ZwYH19uMxE8

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUFUNG

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUFUNGULIWA KESI: MWANASHERIA wa kujitegemea wa jinini Mwanza Stephen Magaigwa amekusudia kufikisha hati yake ya mashitaka kuwafungulia kesi Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Mahakama kuu Maalum ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na wanasheria hao kuruhusu makosa muhimu manne yanayokinzana yaliyomo katika katiba ya Jamhuri na ile ya Mapinduzi.Mwanasheria Stephen Magaigwa. Amesema kuwa Kupitia marekebisho ya katiba ya mwaka 1977 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ya Zanzibar ya mwaka 1984 tangu nchi hizi mbili zilipoungana kuna mambo walikubaliana kwamba haya ni ya Muungano lakini yamekiukwa kupitia marekebisho yaliyofanywa ya katiba ya Zanzibar. "Baada ya kutumia taaluma yangu kifungu baada ya kifungu nimegundua kuwa marekebisho hayo yameingilia mambo ya Muungano na kuleta mkinzano au mkanganyiko katika shughuli za kila siku za utendaji wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania". "Nilitegemea kuwa wanasheria wa serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wangechukuwa hatuwa maalum kurekebisha hali hii tangu awali kabla ya kuipeleka katika utekelezaji lakini walikaa kimya kama wataalamu wa sheria wasiojuwa kazi yao. Mambo manne aliyogundua" Mbele ya wandishi wa habari. 1.Haki za binadamu:- "Katika marekebisho ya katiba ya Zanzibar suala la Haki za Binadamu katiba hiyo imezua kwamba haliwezi kuja katika Mahakama ya Rufaa –Wakati Ukisoma katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jedwali la 1 unagundua kuwa suala la Mahakama ya Rufaa ni suala la Muungano" "Lakini Haitoshi linapokuja suala la haki za binadamu nchi inayohusika ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"2.Ukisoma Marekebisho ya Katiba ya Zanzibar kifungu cha 2A Rais wa Zanzibar anaweza akaigawa Zanzibar katika mikoa, wilaya na maeneo mengine kadri atakavyojisikia – Lakini kifungu cha katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2(2) Suala la Mipaka ya nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni suala la Muungano hivyo Rais akitaka kuigawa sehemu ya Jamhuri ya Muungano (Tz bara na Tz visiwani) ni lazima awasiliane na Rais wa Zanzibar  Lakini ya Zanzibar inasema anaweza kugawa bila kuwasiliana na Rais wa Tanzania, sasa tuna nchi moja ambayo imeungana kwenye mipaka lakini watu wawili wanaohusika kuigawa. 3.Majeshi ya Ulinzi:- "Katiba ya Jamhuri inasema kuwa nchi pekee ambayo imepewa mamlaka ya kuunda majeshi ya ulinzi au vikosi vya aina yeyote ile ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lakini Marekebisho ya kumi ya sheria namba 9 ya mwaka 2010 ya katiba ya Zanzibar yanasema sasa wanaweza kuunda vikosi kama KMKM na kadhalika … Swali ni nani Amri Jeshi Mkuu wa majeshi hayo? Kwani yanapoundwa lazima yawe na mtoa amri wake mkuu"Katiba zinazokinzana. 4.Wakuu wa nchi wawili:- "Ukisoma katiba ya Zanzibar 26(1) na ile ya Muungano kifungu cha 33(2) utagundua kuwa sasa tuna wakuu wa nchi wawili, sasa tunapokuwa na wakuu wawili ile hali katika katiba hatua ruksa ya kuwa na ‘two head of state in one country’ hali hii inamaanisha nini?" "Nimefungua kesi hii Mwanza kwa mujibu wa Kifungu cha katiba ya Jamhuri 126-127 na 128, hivyo shauri langu litakapo sajiliwa na kupatiwa hati ya Mashitaka, Rais atapewa taarifa kuteuwa majaji wa kusikiliza kesi hii maalum ya katiba kwenye mahakama maalum ya katiba" Lengo kuu:- Nitaomba Mahakama hiyo iamuru katiba ya Zanzibar irekebishwe kuondoa kasoro hizo haraka iwezekanavyo ili kuleta sifa ya Muungano.

IPC NA UTPC YAWAKUTANISHA WADAU WA HABARI IRINGA

zzz%2B3.JPG
zzz.JPG
zzz%2B1.JPG
zzz%2B2.JPG
Na Francis Godwin,Iringa MKUU wa chuo kikuu cha Tumaini Iringa Profesa Nicholaus Bangu ameitaka wizara ya elimu nchini kuangalia uwezekano wa kuboresha zaidi mitaala ya elimu kwa kuongeza somo la usomaji wa magazeti kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili kuwawezesha vijana wengi zaidi kuipenda taaluma hiyo na kuongeza nguvu zaidi ya usomaji wa magazeti. Prof.Bangu alitoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano wa wadau wa habari ulioandaliwa na chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) kwa ufadhili wa muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kufanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Iringa. Alisema kuwa pamoja na kazi nzuri inayofanywa na wahabari katika kuibua mambo mbali mbali ila bado vyombo vya habari vinapaswa kufanya tathimini na kujua habari zinazoandikwa zinasomwa kwa kiwango gani . Hivyo alisema kuwa njia pekee ya kuongeza nguvu ya usomaji wa magazeti hapa nchini ni vyombo vya habari kujenga mahusiano zaidi na wizara ya elimu ili kuangalia uwezekano wa kuingiza somo la usomaji wa magazeti katika vipindi mashuleni. Prof.Bangu alisema kuwa kwa mtazamo wake usomaji wa magazeti nchini umeendelea kushuka zaidi pamoja na kuwepo kwa ongezeko kubwa la magazeti hayo na kuwa iwapo wasomaji wa magazeti itapungua kuna uwezekano wa waandishi wa habari kuendelea kununuliwa na watu wachache wenye pesa ili kuendelea kuwaandikia habari zao. Hata hivyo alisema kuwa mwenendo wa uandishi wa habari wa magazeti kwa sasa unatia kichefu chefu kutokana na baadhi ya magazeti kila linapotoka kuandika habari za kuishambulia serikali kwa mabaya pekee huku mazuri yakiachwa hali inayopelekea wasomaji kuchukia magazeti hayo . Katika hatua nyingine Profesa Bangu alitaka vyombo vya habari nchini kubadilika kwa kujikita kuandika habari za uchumi na zile za kijamii kwa ngazi ya chini zaidi badala ya kuendelea kuandika habari za kitaifa pekee. Alisema kuwa iwapo wanahabari nchini watajikita kuandika habari za uchumi upo uwezekano wa maslahi yao pia kuweza kuboreshwa kutokana na kazi wanayoifanya. Kwa upande wake Rais wa UTPC Keneth Simbaya aliwataka wanahabari nchini kuweza kubadilika kwa kujikita kuandika habari zenye kulijenga Taifa na sio kulibomoa Taifa. Alisema kuwa hakuna ubishi kuwa Taifa limeweza kufika hapa tulipo kutokana na kazi nzuri ya vyombo vya habari na kuwa kazi hiyo nzuri inapaswa kuendelea kuenziwa na wanahabari nchini kwa kufanya kazi zenye maadili zaidi. Pia alitaka wadau wa habari kuendelea kusaidia vilabu vya waandishi wa habari nchini ili kuweza kusonga mbele zaidi. Akizungumzia mahusiano kati ya waandishi wa habari na viongozi mdau wa habari Mzee David Butinini alisema kuwa bado vyombo vya habari nchini vimeendelea kunyimwa ushirikiano na viongozi wa serikali . Huku akitaka waandishi wa habari kuendelea kuandika habari za vijijini zaidi badala ya kuandika habari za semina na zile za watu wanaowalipa posho ili kuweza kuziandika habari zao. Butinini alisema kuwa itapendeza kuona waandishi wa habari wakiandika habari za kilimo zaidi na kuona kuwa sera ya kilimo kwanza inatekelezwa kwa vitendo badala ya ilivyo sasa ambapo kilimo kwanza kimekuwa kikizungumziwa katika vyombo vya habari pekee badala ya kuandika utekelezaji. "Nawaombeni sana waandishi wa habari kuacha kuogopa katika kuendelea kuwatumikia wananchi katika tasnia ya habari ....kwani iwapo waandishi wa habari watashindwa kutumikia vema wananchi

MAZISHI YA ASKARI ALIYEUAWA NA JAMBAZI MWANZA

Baadhi+ya+polsi+wakiwa+wamebeba+jeneza+l
Baadhi ya Polisi wakiwa wamebeba jeneza la mwili wa marehemu Kijanda wakielekea kuzika huko Kahangara Magu,
pi+Askari+wakitoa+heshima+za+mwisho+kwa+
Askari wa Jeshi la Polisi wakitoa heshima wakati wa mazishi ya askari mwenzao marehemu PC Kijanda Mwandu, katika makaburi ya kifamilia eneo la Kahangara, wilayani Magu, Mwanza juzi, Mwandu aliuawa kwa kupigwa risasi shingoni na jambazi wakati akiwa katika harakati za kumkamata.( PICHA NA NMASHAKA BALTAZAR)
pix+3+polisi+wakiweka+chini+jeneza+la+ma
Polisi wakiweka chini jeneza la marehemu kabla ya mazishii
pix+4+Jeneza+la+mwili+wa+PC+Kijanda+liki
Jeneza lenye mwili wa marehemu Kijanda
pix+6+Heshima+za+mwisho+kwa+marehemu+PC+
pix+8+Maaskari+wakiushusha+mwili+wa+mare
Maaskari wakiushusha mwili wa maremhu PC Kijanda kaburini ,mazishi yaliyofanyika Kahangara Magu
pix+10+Badhi+ya+ndugu%252C+jamaa+wa+mare
Baadhi ya ndugu, jamaa wa marehemu wakiweka mashada juu ya kaburi la PC kijanda
pix+14+Robert+Manumba+%2528DCI%2529+akit
Robert Manumba (DCI) akitoa salamau za jeshi la polisi baada ya mazishi ya PC Kijanda aliuawa na jambazi kwa risasi
pix+20+askari+polisi+wakitoa+heshima+za+

Ajali Ya Basi La Taqwa na Moro Best

TRAFIKI+AKIMSINDIKIZA+MTOTO+ALIYERUHIWA+
TRAFIKI AKIMSINDIKIZA MTOTO ALIYERUHIWA KATIKA BASI LA MORO BEST PIX NO 4
Mtoto Pascal (4) akiwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, alipofikishwa kupata tiba baada kujeruhiwa katika basi la Taqwa T 478 BBJ.
MAJERUHI+WA+AJALI+MBILI+ZA+BASI+LA+TAQWA
MAJERUHI WA AJALI MBILI ZA BASI LA TAQWA MAGDALENA LEVIRIAN (18) KULIA NA ELIZABERTH PATRICK (15) PIX NO 6
Askari wa JWTZ akimwangalia mmoja wa majeruhi wa ajali ya mabasi ya Taqwa na Moro Best iliyotokea baada ya kulikwepa Lori lililokuwa limeegeshwa katika Barabara Kuu ya Dar-Moro, eneo la Mikeshe, Morogoro.
MKUU+WA+USLAMA+BARABARANI+MKOA+WA+MORO%2
MKUU WA USALAMA BARABARANI MKOA WA MORO, LEORNAD GYINDO KUSHOTO AKIMSIKILIZA DEREVA BASI LA MORO BEST T 846 BCU
DSC_0124.jpg
Askari akimhoji abiria ambaye pamoja na mwanawe walinusurika katika ajali hiyo.

PILIKAPILIKA ZA UJENZI WA MAKAZI MAPYA YA WAATHIRIKA WA MAFURIKO MABWEPANDE

_MG_0524.jpg
Mhandisi wa Mradi wa makazi mapya watakakohamia waathirika wa mafuriko, Ismail Mafita (kulia), akimuelezea Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mabanda ya waathirika leo katika eneo la Mabwepande, Dar es Salaam.
_MG_0522.jpg
Mmoja wa maofisa wlioko kwenye mradi huo, akiwaeleza baadhi ya waathirika wa mafuriko kutoka eneo la Hannanasif, walipokwenda kuangalia eneo hilo watakalohamia kuanza maisha mapya.
_MG_0530.jpg
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Rugimbana (kulia)akimpongeza mmoja wa askari wa JKT, wakati wa ujenzi wa mahema ya waathirika leo
_MG_0535.jpg
Rugimbana akisaidia kuweka sawa hema wakati wa ujenzi wa mabanda ya waahtirika
_MG_0544.jpg
Baadhi ya waahtirika wa mafuriko wakitembezwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, kuona maendeleo ya ujenzi wa mahema watakamohamia
_MG_0547.jpg
_MG_0552.jpg
JKT wakiendelea kuenga mahema
_MG_0554.jpg
Baadhi ya Askari wa JKT, wakihudumiwa maji baada ya kupata mlo wa mchana
_MG_0561.jpg
Askari wa Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wakiendelea na ujenzi wa mahema kwa ajili ya makazi ya muda kwa waathirika wa mafuriko,katika eneo la Mabwepande, wilayani Kinondoni, Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)
Choo kikiandaliwa na fundi wa Msalaba Mwekundu
_MG_0590.jpg
_MG_0597.jpg
Mfumo wa maji wa muda ukiwa umetengenezwa KUTOKA KWA MTAA KWA MTAA