Envaya

ELIMISHA

Habari

Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri

large.jpg

Shirika la ELIMISHA pia linajihusisha na uhifadhi wa mazingira na rasilimali za maji.


ELIMISHA
NON GOVERNMENTAL ORGANIZATION
P.O. Box 220, Mbeya Tanzania.
Web:   www.elimishatz.org
Email: elimishatz@yahoo.com
Cell:    +255 754 350 377
Fiscal address:
Sabasaba Road.
Ujenzi area Mbeya City.

BRIEF  DETAILS ABOUT “ELIMISHA”

 


Introduction

 


ELIMISHA is non-governmental organization founded by journalists in Mbeya Region In 2009 for carrying out activities in mainland Tanzania. ELIMISHA was registered in April  vide registration number ooNGO00003744. The purpose for which it was founded is to help the community with a focus on women, children and youth to have good Good health and quality education, participate and be involved in national activities, to reap the fruits of their efforts and to be given diverse opportunities including leadership and administration in order to have good life, sustainability and meets their  dreams. For attaining their dreams, ELIMISHA will use techniques like media and other means and will do the following:
Educate the community about their rights, responsibility and tasks of civilians and leaders  as spelt out in the country’s constitution through debates, workshops and seminars, including how to use media organs at large.


To explore sources of the increase of sub-standard services of education, poverty and disease.
To carry on research in order to determine the sources of poverty, poor health, women problems, children and youth problems for their own development and the nation at large.
To collaborate with the community in building the power of knowing policies and laws pertaining to women, children and youth.
To sensitize women and youth in order to participate in analyzing their problems and their needs through meetings and come up with resolutions that will be used to chart out strategies for their solutions.
To capacitate women and youth on preparation, execution, follow-up and evaluation of their community/economic  projects that are geared towards supporting special groups such as orphans and those most vulnerable, people with disabilities and the elderly.
To conduct campaigns on stopping habits of dependence, self-unconsciousness, lack of self starting in doing activities that are geared towards helping women, and youth through education and other trades.
To cooperate with other stakeholders in a bid to promote and to foster to be bona-fide and responsible of local authorities for providing quality services to its people, especially special groups and those living in villages in un-reachable areas.


Establishment of the Organization
ELIMISHA was established through the efforts of journalists in Mbeya caused by issues pertaining to women, children, youth, disabled and the elderly found by them while executing their daily duties. In a bid to accomplish their duties of searching and distribution of media issues the Founders of this organization get an opportunity of reaching other areas in which are villages where they witness a multitude of community problems. Through this they found that there was a gap that could not be filled through writing issues for the media only and therefore found that it was important to establish this organization. Among the challenges that forced the establishment of this organization were:
• The perpetuation of poverty due to poor quality of education amongst citizens
• those living in villages despite the government having set a side a budget for development projects for poverty alleviation.
• This confirms that there has been irresponsibility on the part of the community and the government leaders.
• Services provided by organizations(NGOs and CBOs) focus on urban areas
• leaving men ,women, youth and children needs unattended in rural areas (villages).
• Due to lack of good governance, the citizens have failed to participate effectively
• In carrying out developmental  programmes and in making their leaders accountable.
• In other rural areas, men domination has left women a side and therefore have deprived them
• opportunities of participating effectively in meetings and in village decision making
• and their arguments and upper ranking issues miss chance of being incorporated into development programmes. Equally the same women are left behind in contesting leadership posts even those for development in their villages such as water, education, and HIV and AIDS.
• Boys and girls become demoralized about life in villages thus resort to go to urban areas as a result of lack of classroom education and entrepreneurship skills that could remove them from poverty through investments that surround them such as land and other opportunities.
• A big group of children who are the future leaders have lost expectations. Some of them are missing opportunities for education due to their parents ignoring the importance of education; some are used employed in large estates, engage in carrying heavy loads, herding cattle, domestic employment which affects them psychologically. Likewise orphans whose numbers are increase due to effects of HIV and AIDS have been left unattended.
The way forward for the Organization.
ELIMISHA has prepared itself to be the pioneer for the community and other stakeholders in a bid to confront the challenges and determines to do the following:
To foster cooperation with stakeholders(Faith based Organizations, CBOs/NGOs) in our activities and District Councils, Wards and villages/hamlets in our activities for the purpose of providing services benefiting the community of the organization easily
To sensitize women and youth to take action in developing plans for development
and the utilization of their investments through legitimate meetings.
To elaborate, interpret different policies and laws that concern women, Children and youth so that they are easy to be understood, being used and implemented by the community.
To organize trainings, seminars, workshops for capacitating women and youth for development, build a culture of self reliance, health and family planning.
To use the services of journalists and other consultants in doing research work and to come up with findings about the problems facing women, children and youth for the purpose of giving assistance through community education via mass media organs such as TV, newspapers, Radio, journals, networks by e-mails, blogs and brochures.
To organize dialogues and various debates for the purpose of fostering faithfulness and accountability of the District Councils in order to improve their services.
Activities
• To do research concerning source poverty of the community with a focus in villages in Mbeya region for the purpose of looking for its solution.
• To sensitize the community in environmental conservation as a to priority.
• To go through other research work and find out areas that are affected by poverty for the purpose of helping those affected especially women and children and youth.
• To help children stricken by poverty for the purpose of making them perform better in schools.
• To provide services that prevents youth in schools to be discontinued due to lack of resources, involvement in criminal acts and incidences of pregnancies whose parents’ incomes are low.
• To  educate families that do not invest in education for their children for hazards that will come about due to lack of education of their children in terms of health, income.
• To identify and provide assistance to children in schools who shows signs of failing at the end of the school life for the purpose of making them improve in understanding what is taught and thereafter become able in classes for their future well being.
• To identify children and youth who need services for psychosocial education, food, health, shelter  for providing them with respective services and referrals.


Child Abuse
• Places where poverty is rampant, there are many child abuse cases. Due to this children are not regular in classes, loose urge for schooling due to having no certainty of getting food when they get home. This is a case that will be given priority in our programme.


Long-term  effects
• Effects of poverty to children include:
• Unhealthy  state during birth, malnutrition, improper care, susceptibility to contracting communicable diseases during birth such as asthma.
• Shortage of food for low income earners, divorce, death, and loss of jobs.
• School dropouts that forces labour for under 14 years, drug addiction, engaging in drinking.
• Havazard spending due to lack of budgets for expenditures in households.
• Increased effects caused by natural disasters and environmental conservation at all levels due to lack of skills to confront them.
• Increased number of orphans and vulnerable children.


EXECUTION.
All activities at present are financed by ELIMISHA through personal subscriptions and volunteering.

*************************    www.elimishatz.org   ************************

 

large.jpg

Ofisi ya shirika la ELIMISHA ipo Barabara ya Sbasaba eneo la Ujenzi jijini Mbeya S.L.P 220 Mbeya Tanzania E-mail: elimishatz@yahoo.com info@elimishatz.org Website:www.elimishatz.org Cell: +255 (0) 754 350 377

ELIMISHA

Tutatumia Elimisha kuokoa jamii

Makala hii imeandikwa na Joachim Nyambo, Mbeya.

MWANAHABARI yeyote ni tegemeo kubwa katika jamii inayomzunguka. Hii ni kutokana na mchango mkubwa wa kazi yake wa kufichua yanayoendelea katika eneo husika, kuelimisha na hata kuhabarisha na kuburudisha.

Kupitia kalamu yake jamii huweza kunufaika hasa kwa mwanahabari aliyeapa kuitumikia jamii. Lakini wapo wanaoona kuandika pekee hakutoshelezi kuitumikia jamii na hasa kutokana na mazingira magumu yanayomzunguka mwanahabari katika nchi zinazoendelea, ikiwamo Tanzania.

Festo Sikagonamo anayefanya shughuli za habari mkoani Mbeya ni mmoja wa wanahabari wa namna hiyo. Baada ya kuona amefanya kazi kwa muda mrefu huku akiona malengo ya kuitumikia jamii akiyafikia kwa kusuasua akaona ni lazima atafute njia mbadala.

Mwaka 2009 aliamua kuanzisha shirika lisilo la kiserikali la Elimisha. Shirika hilo lililo chini ya waandishi wa habari lililenga kufanya kazi mahali popote Tazania Bara.

Sikagonamo ndiye amekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Elimisha, anasema taasisi hiyo ilianzishwa kutokana na msukumo wa wanahabari uliosababishwa na mguso walioupata katika utendaji wao wa kazi za kila siku ambapo katika kutekeleza majukumu yao ya kutafuta na kusambaza habari, katika maeneo mbalimbali yakiwamo ya vijijini wanashuhudia matatizo mengi ya kijamii.

“Ni katika hali hiyo mimi na wenzangu tukaona uwepo wa changamoto, upungufu na pengo ambalo lisingeweza kuzibwa kwa kutafuta na kuandika habari peke yake, na hivyo kuona umuhimu wa kuanzisha shirika hili,” anasema.

Miongoni mwa changamoto na upungufu uliosukuma kuanzishwa kwa Elimisha kuendelea kwa umasikini na elimu duni miongoni mwa wananchi, hasa vijijini, licha ya Serikali kutenga fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya kupunguza umasikini hali inayothibitisha kuwepo na mdororo wa uwajibikaji miongoni mwa wananchi na viongozi kutotimiza wajibu.

Huduma za mashirika na asasi nyingi zinalenga maeneo ya mijini wakati makundi makubwa ya wahitaji yapo vijijini. Kutokana na ukosefu wa utawala bora, wananchi hawa wameshindwa kushiriki kikamilifu katika mipango ya maendeleo pamoja na kuhimiza uwajibikaji wa viongozi wao ili kuharakisha maendeleo.

Maeneo mengi ya vijijini, mfumo dume umewaacha pembezoni wanawake na hivyo kuwanyima fursa za kushiriki kikamilifu katika mikutano ya maamuzi ya vijiji na hivyo hoja zao na vipaumbele vyao kukosa nafasi katika mipango ya maendeleo.

Hali kadhalika, wanawake wanaachwa nyuma kuwania nafasi za uongozi hata za kwenye kamati za miradi ya maendeleo ya vijiji vyao kama miradi ya maji, elimu na Ukimwi na kusababisha kupungua kwa nguvu kazi.

Sikagonamo anasema jitihada za Serikali kuinua uchumi vijijini bado zinakwama hivyo vijana wavulana kwa wasichana wanakata tamaa ya maisha na kukimbilia mijini kwa kukosa elimu ya darasani na ya ujasiriamali ya kuwaondoa katika umaskini kupitia rasilimali zinazowazunguka ikiwemo ardhi nzuri na fursa zingine.

Kundi kubwa la watoto ambao ndiyo mustakabali wa taifa wamekosa matumaini kutokana na baadhi yao kukosa fursa za elimu kwa wazazi kutothamini elimu huku wengine wakitumikishwa kinyume cha sheria katika mashamba makubwa, kufanya vibarua vya kubeba mizigo, kuchunga mifugo, na kazi za ndani hali ambayo inawaathiri kisaikoloji maisha yao.

Anasema wapo yatima ambao idadi yao inazidi kuongezeka kutokana na ugonjwa wa Ukimwi wameachwa bila msaada.

“Kwa haya tukaona kuna ulazima wa kuwa na chombo cha kusaidia kuwezesha jamii hasa wanawake, watoto na vijana kuwa na Afya na Elimu bora, kujikinga na maambukizi mapya ya VVU/UKIMWI kushiriki na kushirikishwa katika shughuli za maendeleo ya nchi, kufaidi matunda ya jitihada zao na kupewa fursa zaidi katika nyanja mbalimbali zikiwemo za uongozi na utawala ili kuwa na maisha bora, endelevu na yenye kutimiza ndoto zao.”

Lakini haya yote yanawezaje kufanikiwa kupitia taasisi hii iliyo chini ya mwanahabari. Sikagonamo anasema ili kufikia ndoto yake hii, Shirika la Elimisha kwa kutumia vyombo vya habari na mbinu nyingine, limejifunga kufanya mambo mengi kwa hisani ya wadau mbalimbali watakaoguswa.

Anayataja mambo hayo kuwa ni pamoja na kuelimisha jamii juu ya haki, wajibu na majukumu ya raia na viongozi kwa mujibu wa katiba ya nchi kupitia midahalo, warsha na semina, sambamba na matumizi ya vyombo vya habari katika upana wake.

Kuibua vyanzo vinavyochangia kuongezeka kwa huduma duni, za elimu, umasikini na magonjwa, kufanya tafiti zinazohusu vyanzo vya umasikini, elimu duni, afya hafifu, athari za VVU/UKIMWI na matatizo ya wanawake, watoto na vijana kwa ajili ya maendeleo yao na taifa kwa ujumla ni jukumu pia la Elimisha.

Mkurugenzi Mtendaji huyu anasema kushirikiana na jamii katika kujenga ufahamu wa sera na sheria zinazohusu wanawake, watoto na vijana, kuhamasisha ushiriki wa wanawake na vijana katika kuainisha na kuchambua matatizo na mahitaji yao kupitia mikutano halali na maamuzi kwa lengo la kuandaa mikakati ya kutafutia ufumbuzi.

“Tumelenga pia kuwajengea uwezo wanawake na vijana juu ya uandaaji, utekelezaji, ufuatiliaji na ufanyaji tathmini wa miradi yao ya kijamii na kiuchumi, na kuhudumia makundi maalum, kama watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi, watu wenye ulemavu na wazee”. Anasema na kuongeza.

“Hatuishii hapo bali tunakwenba mbali zaidi na kuhakikisha tunaendesha kampeni ya kutokomeza tabia ya utegemezi, kutojiamini na ukosefu wa ari ya kutojituma kufanya kazi iliyojengeka miongoni mwa wanawake na vijana kwa njia ya elimu na stadi mbalimbali”.

Anasema shirika kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inanuia kukuza na kuhimiza uadilifu na uwajibikaji wa Serikali za Mitaa ili ziwe na ufanisi katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi, hususan makundi maalumu na walioko vijijini/pembezoni.

Akizungumzia shughuli zinazofanywa na shirika tangu kupata usajili wake mwaka 2010, Sikagonamo anasema Elimisha inafanya shughuli za utafiti kuhusu chanzo cha umasikini wa wananchi hasa vijijini katika mkoa wa Mbeya kwa lengo la kuisaidia kutafuta ufumbuzi.

Hii inatokana na ukweli kwamba licha ya mkoa wa Mbeya kuwa na rasilimali nyingi na jitihada nyingi za wadau mbalimbali, bado umasikini umeonekana kuzidi kuotesha mizizi.

“Hali kadhalika Elimisha haiko nyuma katika suala la uhamasishaji katika uhifadhi na utunzaji mazingira ambao unapewa msukumo mkubwa.

Baadhi ya tafiti tulizofanya maeneo mbalimbali hasa vijijini tumebaini kuwa wakati uchumi unapoyumba watoto wanaotoka katika jamii zenye kipato cha chini wanakumbana na tishio kubwa la kutofanya vyema katika masomo yao”.

Anasema mara nyingi, jambo hilo huanza kuwadhuru watoto hao wakiwa wangali katika kiwango cha shule ya msingi, katika mfumo wa elimu Tanzania na baadhi ya nchi za afrika, watoto hao hupata tishio kubwa zaidi, ikilinganishwa na watoto wengine, ya kutopata maadaraja mazuri shuleni na hata kukosa kumaliza masomo yao ya shule.

Kuna mambo kadhaa yanayoeleza sababu za wanafunzi kuwa na mazoea ya kuacha shule anasema. Anafafanua kuwa kwa watoto walio na rasilimali kidogo, tishio linatokana na sababu kama vile viwango vya watoto waliovunja sheria, viwango vya juu vya watoto waliopata mimba, wakiwa wadogo na kutegemea kiuchumi mzazi au wazazi wenye kipato cha chini.

Mwanahabari huyu aliyeamua kuisaidia jamii kwa njia mbadala ya uana habari anasema familia na jamii zisizotilia maanani uwekezaji katika elimu na maendeleo ya watoto masikini hupata matokeo yasiyo mazuri kwani baadaye watoto hao hukosa kazi na huwa na mapato madogo, Viwango vikubwa zaidi vya kuzaa mapema na hatari zake kwa familia, afya na maisha bora kwa ujumla ndiyo mambo muhimu yanayopaswa kuzingatiwa kwa kuwa elimu kutoka kiwango cha shule ya msingi hadi shule ya sekondari ina umuhimu mkuu maishani.

“Umasikini mara nyingi huathiri, kwa kiwango kikubwa cha kufaulu kwa watoto shuleni. Kwa hivyo, tunaweza kusema kuwa watoto wanaoishi katika hali ya umasikini au chini ya kiwango cha umasikini watakuwa na wakati mgumu zaidi kufaulu katika elimu kuliko watoto wanaoishi katika hali isiyo ya umasikini”.

“Watoto masikini hawapati huduma muhimu za afya na hii inawafanya wakose kwenda shuleni kwa siku nyingi katika kila mwaka. Pia, kuna uwezekano zaidi kwa watoto masikini kuteseka kwa njaa, uchovu, kukasirika hovyo, maumivu ya kichwa, maambukizi ya masikio, mafua na homa… Magonjwa haya yana uwezo wa kumzuia mtoto au mwanafunzi kuelewa yale anayofunzwa darasani”.

Yapo mambo mengi yanayotajwa na Sikagonamo kama matarajio ya kazi katikaa shirika la Elimika. Lakini jambo la msingi hapa ni kwa wanahabari nchini kujifunza namna ya kubadilika ili jamii izidi kunufaika zaidi na uwepo wao.

Ni vema wanahabari wakachukulia maamuzi kama haya ya Sikagonamo na wengine wengi walioonesha mabadiliko kwa kuchukua mikakati yao kama changamoto za wao kubadilika. Nayasema haya kutokana na uzoefu nilionao katika tasnia hii.

Yawezekana ni uzoefu mdogo lakini hakuna anayeweza kubisha kuwa wanahabari wengi wamebaki watu wa kuandika na kusambaza habari. Ni kutokana na kukosa ubunifu wengi maisha yao yamebaki mikononi mwa wahariri wanaoamua kazi zao zitoke ama zitupwe kapuni.

Matokeo ya kazi za wanahabari hawa kutupwa kapuni ni janga kubwa kwa vyanzo vya habari hizo hasa wale wananchi waishio katika maeneo ya pembezoni ambao sauti zao ni mara chache kusikika.

Iwapo wanahabari tukabadilika tukawa na ubunifu wa kuzisaidia jamii zaidi ya kuchukua habari zao kuziandika na kuzitangaza ni wazi jamii zitanufaika. Tuige mfano huu na wa wanahabari wengine walioona sababu ya kuzisaidia jamii kwa njia mbalimbali badala ya kuishia kuandika na kutegemea wahariri kuzipitisha habari zetu.

Mwandishi wa makala haya anapatikana kwa email nyambojoachim@gmail.com ukumwitu@yahoo.com simu 0756 40 95 97/0713 12 83 71.

large.jpg

Umasikini unavyo athiri maisha ya watoto.